Airtel yatoa ofa kabambe maonesho ya sabasaba - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Airtel yatoa ofa kabambe maonesho ya sabasaba

 Meneja uhusiano wa Airtel Bw, Jackson Mmbando  (kulia)  na Afisa huduma kwa wateja wa Airtel Bi  Veronica Valentine (kushoto) wakionesha simu aina ya ZTE na Motorola katika banda la Airtel lililoko katika viwanja vya maonesho ya biashara maarufu kama sabasaba, simu hizo zitauzwa kwa bei ya ofa ya shilingi 16,000 tu na mteja ataunganishwa na kufurushi cha muda wa maongezi kwa mwezi mzima cha shilingi 10,000 BURE. katikati ni Afisa huduma kwa wateja wa Airtel Tumwidike Michael
Kutoka kulia ni Afisa huduma kwa wateja wa Airtel Digna Paul na Tumwidike Michael wakitoa huduma katika banda la Airtel lilipo katika  vya maonesho ya biashara maarufu kama sabasaba leo. katika banda hilo airtel itauza simu original kwa bei ya shilingi 16,000 ikiwa imeunganishwa na laini ya airtel na bando la mwezi mzima la shilingi 10,000 BURE.
·         Airtel kuuza simu kwa bei nafuu sabasaba
·         Simu ya Airtel kuuzwa 16,000 ikiwa na bando la 10,00 mwezi mzima BURE

Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel  imetangaza ofa kabambe wakati wote wa maonyesho ya biashara ya sabasaba mwaka huu zitakazowawezesha wateja wake na wale  wapya kuunganishwa na huduma za mtandao kwa gharama nafuu na pia kujipatia simu bomba kwa bei nafuu.

Akiongea na waandishi wa habari katika banda la Airtel lililopo viwanja vya sabasaba Meneja Uhusiano wa Airtel Jackson Mmbando alisema “dhamira yetu Airtel ni kuendelea kuunganisha jamii kwa bidhaa na huduma, hivyo kwa msimu huu maonesho ya saba saba tutatoa ofa nyingi sana ikiwemo  simu aina ya ZTE GS 500, Motorola C113, Motorola F3 na Motorola C117 kwa shilingi 16,000 tu na  mteja akishanunua ataunganishwa na bando la shilingi 10,000 litakalodumu kwa muda wa mwezi mmoja”

“Unaweza ukaona hapo gharama ya simu inakuwa nafuu na kisha  unaunganishwa na kifurushi cha mwezi mzima BURE kuongea na ndugu, jamaa, na marafiki huku ukifaidi huduma zingine za Airtel” alieleza Mmbando

Katika banda letu ndani ya saba saba mwaka huu pia huduma zitakazopatikana ni pamoja na   kubadilisha laini, huduma za Airtel Money, simu za smartphone za kisasa na origino, huduma ya Timiza Vicoba, kuelekezwa jinsi yakusoma masomo ya ufundi kwa njia ya simu VETA kupitia Vsomo pamoja na kujua jinsi yakufungua biashara ya Duka la Airtel popote na jinsi ya kupata faida yako”

Mmbando alisema kuwa “Airtel imekuwa ni desturi yetu kuleta huduma na bidhaa zetu katika maonyesho haya ya biashara kila mwaka na kukutana na wateja wetu ana kwa ana ili kutoa elimu zaidi kuhusu huduma zetu mpya na za kibunifu tunazozitoa kila mwaka”.

“Natoa wito kwa watanzania kutembelea banda letu na kujipatia simu huduma za kimtandao zote kwa  gharama nafuu na vilevile kukutana na watoa huduma wetu na kupata elimu juu ya huduma mbalimbali  ikiwemo Kupata maelekezo ya kupata mikopo ya vikundi kupitia huduma ya Timiza vikoba.    Kupata maelekezo ya kuweza kufanya biashara za Airtel kokote Tanzania kupitia mfumo wa Maduka ya Airtel AMSHA pamoja na huduma nyingine nyingi” aliongeza Mmbando.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages