Baadhi ya wa wafanyakazi wa TBL Group waliungana na viongozi wa serikali na wafanyakazi kutoka taasisi mbalimbali za umma na za binafsi katika matembezi ya hisani ya kilometa 5 kwa ajili ya kuchangisha fedha za kusaidia wahanga wa tetemeko la ardhi lililotokea hivi karibuni mkoani Kagera.
Matembezi hayo yaliyoongozwa na Rais Mstaafu wa awamu ya pili,Mheshimiwa Ali Hassan Mwinyi yalianzia katika viwanja vya Bwalo la Maofisa wa Polisi eneo la Oysterbay jijini Dar es Salaam na kumalizikia eneo hilo ambapo ahadi na michango mbalimbali ilitolewa.
Wakielezea ushiriki wao katika tukio hilo la kusaidia binadamu wenzao waliofikwa na baadhi ya wafanyakazi walisema kuwa wameguswa na tatizo la tetemeko la ardhi ambalo limesababisha vifo na hasara kubwa na kuongeza kuwa licha ya kampuni kutoa mchango wafanyakazi nao wameguswa na kuungana na wadau wengine kwenye matembezi hayo
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL Group wakisubiri kuanza kwa matembezi
Mh.Ali Hassan Mwinyi katika matembezi akiwa na viongozi wengine wa serikali na wafanyakazi wa taasisi mbalimbali walioshiriki
Baadhi ya wafanyakazi wa TBL Group katika matembezi hayo





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)