Wafanyakazi TBL Group washiriki September Fun run - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Wafanyakazi TBL Group washiriki September Fun run

Baadhi ya wafanyakazi katika picha ya pamoja baada ya kumaliza mashindano
 Baadhi ya wafanyakazi katika matembezi ya kujenga afya
Baadhi ya wafanakazi wakionyesha medali walizopewa kwa kufanikiwa kumaliza mashindano.

-Ni katika utekelezaji wa mpango wa Afya Kwanza
 
Matembezi ya kujenga afya ya September Fun run yalifanyika jijini Dar es salaam katika maeneo ya Oysterbay chini ya udhamini wa kinywaji cha Grand Malta ambapo yaliwashirikisha wafanyakazi kutoka taasisi mbalimbali pamoja na familia zao ambapo pia walipata fursa ya kufanya mazoezi mbalimbali kwa ajili ya kuimarisha afya .
 

Miongoni mwa washiriki wa matembezi haya ya kilometa 10 ni baadhi ya wafanyakazi wa kampuni ya TBL Group ambao wamekuwa na utamaduni wa kufanya mazoezi mara kwa mara kupitia programu ya kampuni yao inayojulikana kama Afya Kwanza ambayo inahamasisha ufanyaji wa mazoezi kwa wafanakazi na familia zao ambapo pia wamekuwa wakipimwa afya zao na kupatiwa elimu ya afya na umuhimu wa kupata lishe bora.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages