Grand Malt yafanikisha tamasha la kujenga afya - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Grand Malt yafanikisha tamasha la kujenga afya

 Mkuu wa Wilaya ya  Kinondoni akisalimiana na baadhi ya wanamichezo waliohudhuria katika bonza la kujenga Afya kwa wananchi lililofanyika  katika viwanja vya Leaders Club kwa Udhamini wa Kinywaji cha Grand Malt
 Mkuu wa wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi  akikabidhi zawadi ya kuku Neema Ndimbo wa klabu ya Jogging ya Kawe mara baada ya kuibuka mshindi wa kufukuza kuku kwa wanawake  wakati wa bonanza la Afya  kwa watanzania liliozishirikisha klab za Jogging za jijini Dar es Salaam, katika viwanja vya Leaders Club kwa Udhamini wa Kinywaji cha Grand Malt.Kushoto anaye shuhudia ni Meneja Matukio wa taifa wa TBL Group George Mwombeki .
Wakazi wa Dar es salaam wakishiriki kufanya mazoezika tamasha kubwa la mazoezi ya kujeng mwili lililofanyika katika viwanja vya Leaders jijini Dar es Salaam ambalo mmoja wa wadhamini wa tamasha hilo ni TBL Group kupitia kinywaji cha Grand Malt

Tamasha kubwa la mazoezi   ya kujenga mwili lilifanyika  katika viwanja vya Leaders Club na kuwahusisisha mamia ya wananchi wenye jinsia na  rika mbalimbali na yaliendeshwa na wataalamu mbalimbali wa fani ya mazoezi ya viungo na lilidhaminiwa na kampuni ya TBL Group kupitia kinywaji chake kisicho na kilevi cha Grand Malt chini ya mpango wa kampuni hiyo wa Afya Kwanza na mgeni wa rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni,Ally Hapi.

Tamasha hilo la aina yake kufanyika nchini lilijumuisha mazoezi na michezo ya aina mbalimbali ambayo ilitoa fursa kwa aliyefika eneo hilo kuchagua kushiriki mazoezi na mchezo wowote anaoutaka

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages