PSPF YASAJILI WANACHAMA WmaAPYA LUKUKI KWENYE MAONYESHO YA 40 YA BIASHARA YA KIMATAIFA DAR ES SALAAM 2016 - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

PSPF YASAJILI WANACHAMA WmaAPYA LUKUKI KWENYE MAONYESHO YA 40 YA BIASHARA YA KIMATAIFA DAR ES SALAAM 2016

Wanafunzi wa chuo Cha Uhasibu (TIA), jijini Dar es Salaam, wakipatiwa maelezo ya huduma mbalimbali zitolewazo na Mfuko wa Pensheni wa PSPF walipotembelea banda la Mfuko huo lililoko jingo la Wizara ya fedha kwenye maonyesho ya 40 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam, 2016 viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam Julai 2, 2016. (PICHA NA K-VIS MEDIA/KHALFAN SAID)
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista Mhagama, (kulia), akizungumza jambo wakati alipotembelea banda la Mfuko wa Pensheni wa PSPF kwenye jingo la wizara ya fedha viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam Julai 2, 2016 ambako yanafanyika maonyesho ya 40 ya biashara ya kimataifa ya Dar es Salaam. Hapa waziri akipatiwa maelezo na Afisa Uendeshaji wa PSPF, Hadji Hamisi Jamadari
Afisa Kumbukumbu wa Mfuko Pensheni wa PSPF,  Lupakisyo J. Mwaipungu (kushoto), akimsikiliza Mwananchi huyu aliyetembelea banda la Mfuko huo na kuamua kujiunga na mpango wa uchangiaji wa hiari PSS Julai 2, 2016

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages