RC PAUL MAKONDA ASEMA WANAWAKE NDIO CHANZO CHA UFISADI NCHINI - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

demo-image

RC PAUL MAKONDA ASEMA WANAWAKE NDIO CHANZO CHA UFISADI NCHINI

1
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda akikagua machinjio ya Vingunguti baada ya kuzungumza na wananchi wa Kata ya Mnyamani Dar es Salaam leo asubuhi. Kushoto ni Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, Omari Kumbilamoto.
IMG_8540
Wananchi wa Kata ya Mnyamani Vingunguti wakiwa kwenye mkutano huo wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda (hayupo pichani)
IMG_8552
Makonda (kushoto), akisalimiana na wananchi na viongozi wakati akiwasili kwenye mkutano huo.
IMG_8571
Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala, Omari Kumbilamoto (wa pili kulia), akizungumza katika mkutano huo kabla ya kumkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuzungumza na wananchi. Kutoka kulia ni Diwani wa Kata ya Mnyamani, Shukuru Dege, RC. Makonda na Meneja wa Benki ya Wananchi Dar es Salaam (DCB), Tawi la Ukonga, Das Ndazi.
IMG_8578
Meneja wa Benki ya Wananchi Dar es Salaam (DCB), Tawi la Ukonga, Das Ndazi (kushoto), akizungumza katika mkutano huo kuhusu suala zima la utoaji wa mikopo.

IMG_8588
RC Makonda akizungumza na wananchi wa Vingunguti.
IMG_8589
Wananchi wakimsikiliza RC Makonda.
IMG_8595
Safari ya kwenda kukagua machinjia ya Vingunguti.
IMG_8601
Sehemu ya machinjio ya Vingunguti.
IMG_8610
RC Makonda akipatiwa maelezo kuhusu mitambo ya kuchinjia iliyopo kwenye machinjio hiyo.

Na Dotto Mwaibale

MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema wanawake wamekuwa ni chanzo cha ufisadi nchini kutokana na kupokea zawadi zitokanazo na fedha za kifisadi.

Makonda aliyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Mnyamani Vingunguti Dar es Salaam jana katika mkutano wa kujadili namna ya kupata mikopo mbalimbali kutoka Benki ya Wananchi Dar es Salaam (DCB).

" Ninyi wakina mama mmekuwa chanzo cha ufisadi kwa vile mmekuwa mkipokea fedha na zawadi mbalimbali kutoka kwa watoto wenu lakini mmekuwa hamuwahoji wanako zitoa fedha hizo kwani zingine zinakuwa za kifisadi" aliseama Makonda.

Makonda aliwaambia wanawake hao kuwa hata katika suala zima la usafi linaanzia na malezi ya usafi ya wakina mama kwa watoto wao tangu wakiwa wadogo jambo ambalo lingesaidia kipindi hiki ambapo kunachangamoto kubwa ya kusafisha miji yetu.

Katika hatua nyingine Makonda alitoa pongezi kwa Kaimu Meya wa Manispaa ya Ilala, Omari Kumbilamoto kwa kuwa jirani na wananchi wa kata yake kwa kufanya maendeleo bila ya kujali itikadi za vyama hasa katika kujipatia mikopo kutoka katika Benki ya Wananchi Dar es Salaam (DCB).

"Nimefurahishwa na diwani wenu Kumbilamoto kwa kushirikiana nanyi ili  kujiletea maendeleo ni jambo zuri na wakati huu ni wa kukutana kubuni na kuangalia jambo gani litawakwamua kiuchumi badala ya kuwaza maandamano yasiyo na tija" alisema Makonda.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Pages