
Kupitia Katika Kipindi cha XXL Mtangazaji Mahiri katika Vituo kadhaa vya Radio hapa nchini, Gardner G. Habash ametangaza rasmi kurudi katika Kituo chake cha kazi cha Mwanzo cha Clouds FM, Gardner tayari kesha mwaga wino kwenye kituo hicho mbele ya Mkuu wa Vipindi wa sasa wa Radio hiyo, Shafii Dauda.
Akiongea katika KIpindi cha XXL kinachoendeshwa na B12, Adam Mchomvu na wengine Gadner amesema amefurahi kurudi katika familia yake ya mwanzo huku akisisitiza kuwa na mahusiano mazuri na timu yako ya zamani endapo utakuwa umesajiliwa timu mpya huku ukiendelea kuwasiliana vizuri na timu yako ya zamani. Gadner alikua mtangazaji wa Clouds radio katika Kipindi cha Jahazi na sasa kuendelea kuunguruma tena katika kipindi hiko hiko cha Jahazi, akiwa na swahiba wake, Ephrahim Kibonde pamoja na wengine.
Akiongea katika KIpindi cha XXL kinachoendeshwa na B12, Adam Mchomvu na wengine Gadner amesema amefurahi kurudi katika familia yake ya mwanzo huku akisisitiza kuwa na mahusiano mazuri na timu yako ya zamani endapo utakuwa umesajiliwa timu mpya huku ukiendelea kuwasiliana vizuri na timu yako ya zamani. Gadner alikua mtangazaji wa Clouds radio katika Kipindi cha Jahazi na sasa kuendelea kuunguruma tena katika kipindi hiko hiko cha Jahazi, akiwa na swahiba wake, Ephrahim Kibonde pamoja na wengine.





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)