Semina ya kujadili masuala ya kodi kwenye sekta ya vinywaji vyenye kilevi yafanyika Dar - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Semina ya kujadili masuala ya kodi kwenye sekta ya vinywaji vyenye kilevi yafanyika Dar

 Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Dkt.Adelhelm Meru, (kushoto) akibadilishana mawazo na  Mkurugenzi  Mkuu wa TBL Group ,Roberto Jarrin  wakati  wa semina ya kujadili masuala ya kodi kwenye sekta ya vinywaji iliyofanyika  jana katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam.
 Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Kilimo,Maji na Mifugo Dk.Mary Nagu (kushoto) akibadilishana mawazo na   Mkurugenzi  Mkuu wa TBL Group ,Roberto Jarrin  wakati  wa semina ya kujadili masuala ya kodi kwenye sekta ya vinywaji iliyofanyika  jana katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam.
 Katibu Mkuu Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Dkt.Adelhelm Meru, (kushoto)  akizungumza  wakati wa uzinduzi wa   semina hiyo ambapo alikuwa mgeni rasmi. Kutoka kulia ni  Mkurugenzi  Mkuu wa TBL Group ,Roberto Jarrin , wa pili ni Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya bia ya Serengeti Breweries Tanzania (SBL) Kalpesh Mehta na Mkurugenzi Mkuu wa Heineken Tanzania, Michael Mbungu.
 Baadhi ya wadau mbalimbali waliohudhuria  kwenye mkutano wa Alcoholic Drinks and  Beer Sector Taxation  Workshop uliofanyika leo katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam, wakifuatilia mada mbalimbali zilizokuwa zikitolewa kwenye semina hiyo
 Mkurugenzi Mkuu wa Heineken Tanzania, Michael Mbungu, akifafanua jambo wakati wa mkutano wa  Alcoholic Drinks and  Beer Sector Taxation Workshop ,uliofanyika jana katika Ukumbi wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam. Wengine kutoka kushoto ni  Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya bia ya Serengeti Breweries Tanzania (SBL) Kalpesh Mehta ,   , Christopher  Mgifi kutoka Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji   na Mkurugenzi  Mkuu wa TBL Group ,Roberto Jarrin  
Baadhi ya wadau wakuu walioshiriki katika semina hiyo wakiwa katika picha ya pamoja

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages