Wafanyakazi wa TBL Group watunukiwa vyeti vya ufanisi - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Wafanyakazi wa TBL Group watunukiwa vyeti vya ufanisi

 Mkurugenzi wa kampuni ya TBL Group,Roberto Jarrin akiwa katika picha na baadhi ya wafanyakazi waliotunukiwa tuzo ya you Make the Difference  katika kiwanda cha Dar es Salaam
 Mkurugenzi Mkuu wa TBL Group,Roberto Jarrin (Kushoto) akiwa na mfanyakazi wa kitengo cha ufundi wa kiwanda cha Mbeya Godwin Kambi baada ya kumtunukia cheti kwa kufanyia kazi kiwandani hao kwa kipindi cha miaka 15.Hafla  ya kuwatunuku waanyakazi vyeti ilifanyika hivi karibuni kiwandani hapo.
 Margaret Simon Mlwale ambaye ni  Katibu Muhtasi wa Mkurugenzi wa Kiwanda cha Darbrew naye amepata cheti cha kutambua mchango wake kwa kampuni,waliosimama nyuma yake kutoka kulia ni  Afisa Mwandamizi wa utawala Phinias Mashauri,Mkurugenzi Mkuu wa TBL,Roberto Jarrin na Mkurugenzi Mkuu wa DarBrew David Cason,DarBrew  iko chini ya TBL Group
 Mfanyakazi wa Arusha Anna Andrew ni miongoni mwa waliotunukiwa cheti cha kutambua mchango wake kwa kampuni .
 Mfanyakazi wa kiwanda cha Konyagi Ephreim Mwaswala akiwa ameshikilia cheti cha utambuzi wa mchano wake kwa kampuni alichotunukiwa na Mkurugenzi Mkuu wa TBL Group ,Roberto Jarrin (Kulia) katika hafla iliyofanyika kiwandani hapo hivi karibuni.Kushoto ni Meneja Mauzo wa Kiwanda cha Konyagi Joseph Chibehe
 Wafanyakazi wa TBL Group wa Mwanza wakiwa  katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa TBL Group Roberto Jarrin muda mfupi baaa ya kuwatunukia vyeti vya kutambua mchango wao wa kazi kwa kampuni .Hafla ya kukabidhi vyeti imefanyika hivi karibuni
.Mkurugenzi wa Fedha wa TBL,Deocracius Damas naye alipewa cheti cha kutambua mchango wake wa kazi kwa kampuni .

Mkurugenzi wa kampuni ya TBL Group,Roberto Jarrin,ametoa vyeti vya ufanisi (you Make the Difference) kwa wafanyakazi bora katika kipindi cha robo ya mwaka huu ikiwa ni utaratibu wa  kampuni kutoa motisha kwa wafanyakazi wake wanaofanya vizuri.

Wafanyakazi hao walichaguliwa katika viwanda vya kampuni hiyo vilivyopo Dar e salaam,Mwanza,Arusha na Mbeya,na  hafla za kuwatunukia vyeti zilifanyika hivi karibuni katika viwanda hivyo.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages