EID AL FITR 2015; SEHEMU MUHIMU ZA KUTEMBELEA NDANI YA SIKUKUU HII YA MWAKA 2015 - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

EID AL FITR 2015; SEHEMU MUHIMU ZA KUTEMBELEA NDANI YA SIKUKUU HII YA MWAKA 2015

 Waislamu wote dunia nzima wanatarajia kusheherekea siku kuu hii ya Eid Al Fitr baada ya kufunga kwa muda wa mwezi mzima katika kipindi cha mwezi mtufu. Ingawa tarehe rasmi ya sherehe huwa inategemeana na mwezi kuandama, lakini pia inatarajiwa siku kuu hii huenda ikawa ndani ya wiki ya 29 kwa kalenda ya kawaida ya mwaka, ambapo ni mwishoni mwa wiki hii.
Ni Muhimu ndani ya siku kuu hii mtu kutoa zawadi au kusaidia maskini wasiojiweza kabla ya kuelekea kwenye sala ya Eid Ul Fitr, misaada hii ni nje ya Zakhath na Sadqa ambayo huwa inatolewa katika kipidi cha mwezi mtukufu, sadaqah hizi kwa jina lingine unaweza kuziita sadaqah al fitr, hii ni kuhakikisha kuwa kila mmoja hata masikini wawe na uwezo  wa kusheherekea siku kuu ya Eid.
Hata hivyo, baadhi ya watu hupenda kusheherekea kwa namna tofauti, watu wengi duniani hutembelea sehemu za kitalii, ndani na nje ya nchi.  Kwa baadhi ya maeneo ambayo yatakuwa ni muhimu kwako kutembela katika kipindi hiki cha Eid Al Fitr, hakikisha ni maeneo mazuri kwa utalii na yasiyo na gharama kwa matumizi ya Kifamilia au mtu binafsi
JovagoTanzania, inapendelea kutoa muongozo kwa baadhi ya sehemu muhimu hapa Tanzania, sehemu hizi unaweza ukafika na kupata mahala kwa kujiwekeza na familia yako kwa kipindi kizima cha Eid, kwa kuingiza namba za siri “JOVAGOTZ15”, utakuwa na uwezo wa kupata punguzo za bei za mahotelini mpaka 53% ndani ya Jovago.com. Hotel hizi tano muhimu  zipo Katika sehemu muhimu zifuatazo;

ZANZIBAR,
 Ni sehemu ambayo watu wengi kutoka ndani na nje ya nchi hupendelea kufika, kutokana na amani ya eneo husika na vivutio vya utalii kama makumbusho ya taifa, pamoja na hifadhi za taifa. Mashariki Palace hotel ni moja kati ya hotel muhimu kufikia ambapo JovagoTanzania imeweka punguzo la 35% na Park Hyatt  itakayo kuwa na punguzo la 50%,

ARUSHA
 Mji huu una vivutio vingi vya utalii, ikiwemo hifadhi ya taifa ya Tarangire, Crater, hifadhi za milima ya Ol Doinyo Lengai, pamoja na makumbusho ya taifa. Utaweza kupata mahala pa kujiwekeza  katika hoteli ya “The New Arusha
MWANZA;
 Ni mji wa kupumzika na mahala pa utulivu wa hali ya juu,  wengine wanakuita rockcity kutokana na vivutio vya miamba mingi,  New Mwanza Hotel  ni sehemu nzuri ya kufika kwa usalama, na itakuwa na punguzo la bei mpaka  53%.
DAR ES SALAAM;
 Sehemu ya jiji ambalo wengi hupendelea kufikia iwapo kutakuwa na mipango ya kufanya utalii katika makumbusho ya taifa au starehe za siku kuu ya Eid, ni mji wenyewe sehemu nyingi za starehe na Jovago “Green Light hotel” ni sehemu pa kujiwekeza na mahala penye usalaa iwapo utafikia jijini Dar es Salaam.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages