Robert Mugabe afikisha miaka 91 - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Robert Mugabe afikisha miaka 91

Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe
Rais Robert Mugabe wa Zimbabwe ametimia miaka 91 leo.
Yeye sasa ni kiongozi mzee kabisa duniani, na amekuwa madarakani kwa miaka 35.
Sherehe ya siku yake ya kuzaliwa itafanywa juma lijalo.
Anatarajiwa kufanya sherehe kubwa katika uwanja wa golf huko Victoria Falls, inakisiwa sherehe yenyewe itagharimu dola milioni moja.
Rais Mugabe aanguka katika mkutano wa mataifa ya Afrika mjini Addis Ababa Ethiopia
Maelfu ya watu watahudhuria karamu hiyo, ambapo kutachinjwa ndovu, nyati, paa na simba mmoja.
Shirika la habari la taifa linasema wananchi watalipia dhifa hiyo
Zimbabwe ni moja kati ya nchi maskini duniani.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages