Push Observer yazindua teknolojia ya kisasa ya ukusanyaji wa Taarifa ijulikanayo kwa jina la NewsRadar - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Push Observer yazindua teknolojia ya kisasa ya ukusanyaji wa Taarifa ijulikanayo kwa jina la NewsRadar

 Mshauri mkuu wa mradi wa NewsRadar, Romana Gersuni kutoka Ujerumani akielezea jinsi teknolojia hiyo mpya na ya kisasa ya ukusanyaji taarifa mbalimbali ya Push Observer inavyofanyakazi zake.
 mkuu wa mikakati wa kampuni ya Six Telecoms ambayo ni kampuni mama ya Push Observer, Rashid Shamte akielezea faida ambazo watazipata kampuni mbalimbali nchini, husasani za kibiashara kwa kujiunga na huduma ya NewsRadar waliyoianzisha nchii.
Mkurugenzi Mtendaji wa  Kampuni ya Push Mobile Fred Manento akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na ufanisi wa mradi wa NewsRadar ambao utawawezesha wafanyabiashara kupata taarifa mbalimbali kwa kutumia mradi huo mpya na wa kisasa nchini
 Afisa Mawasiliano wa kampuni ya Push Observer, Tunu Makamula akiteta jambo na wadau wa kampuni hiyo waliohudhuria semina elekezi na uzinduzi rasmi wa mradi wa NewsRadar ambao utawawezesha wafanyabiashara kupata taarifa mbalimbali kwa kutumia mradi huo mpya na wa kisasa nchini.

Sekta zote Nchini sasa zinaweza kupata taarifa mbali mbali zilizorushwa kwene vyombo vya habari kupitia teknolojia mpya ya usambazaji taarifa  ijulikanayo kwa jina la NewsRadar ya kampuni ya Push Observer.

Push Observer Limited ni kampuni ya Tanzania inayomiliki vyombo vya
kiinteligencia na teknolojia ya sanaa ya kufuatilia, kukamata na kuchuja vyombo vya habari - magazeti, matangazo (radio & televisheni),  Internet na uchambuzi, ripoti ya ushindani kwa ajili ya biashara,  serikali na wateja wengineo wa mashirika yasiyo ya kiserikali.

Hivi sasa, Push Observer wanachunguza vituo vya redio 90+, vituo vya
televisheni 15+, magazeti (magazeti, majarida, magazeti na majarida) 70+
na machapisho online ikiwa ni pamoja na blogs na mitandao maudhui.
Observer ni kampuni ya kiTanzania inayoongoza kidigitali, kwa viwango
vya kimataifa na ushirikiano wa kimataifa katika data na uanachama na
vyombo kama FIBEP, Nudge, Vision Critical, na Harvard Innovation Labs.

Kwa mujibu wa Mkuu wa Mikakati wa Six Telecoms, Kampuni mama ya Push
Observer, Rashid Shamte alisema kuwa kupitia teknologia hii ya  usambazaji ya kisasa, wateja wao wataweza kupata habari taarifa muhimu  na mpya masaa ishirini na nne ya wiki. Aliongeza kuwa,tumezindua  teknolojia hii kwa wateja wetu kutokana na teknologia ya uchunguzi wa  vyombo vya habari kubadilika sana miaka ya karibuni”.

“Huduma hii ya kusambaza taarifa imekuwa ya kisasa, rahisi na ya ubora wa hali  ya juu kutokana na uwekezaji wetu katika teknolojia hii. Wana vifaa vya  kisasa ambavyo vinaweza kupata taarifa kupitia televisheni, magazeti,
mitandao ya kijamii na redio kwa muda muafaka, vifaa hivyo vinauwezo wa
kupata taarifa had 350,000 kutoka vyombo mbali mbali. Kwa kutambua
mahitaji ya wateja wetu kupata habari na taarifa za muhimu tumeamua
kuzindua huduma hii na ili kuwahakikishia wateja wetu upatikanaji wa
taarifa muhimu na taarifa zinginezo za kwene vyombo vya habari kwa muda
muafaka” alisema Mkurugenzi Mtendaji wa Push Observer, Tom Kyalo.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages