Jifunze kuhusu Matairi ya gari lako..leo tunaangalia kuhusu ukomo wa spidi katika tairi. - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Jifunze kuhusu Matairi ya gari lako..leo tunaangalia kuhusu ukomo wa spidi katika tairi.


Imekuwa ni kawaida kwa watumiaji wengi kununua matairi ya magari yao bila kujali viwango vya matairi hayo ili mradi tu mtu kanunua. Kwenye Kununua matairi kuna vigezo vingi sana vinavyopelekea kuwa tairi kuwa sahihi katika mahitaji yako.

Mfano wa vitu hivyo ni Ukubwa wa tairi (size ya tairi), upana, na urefu wa tairi na uwezo wa mwisho wa spidi gari inapokimbia lakini wengi wamekuwa wakiangalia vitu vichache kama Upana, na Urefu tu bila kuangalia spidi inayotakiwa kukimbia katika matairi hayo kwa kingereza uitwa Tyre Speed rating ambapo matairi yote huwa yana ukomo wa spidi endapo gari inatembea.

Leo sasa tutakuangalizia jinsi ya kuweza kutambua spidi ya mwisho unayotakiwa kukimbia kutokana na matairi ya gari yako. Jinsi ya kutambua unachotakiwa kufanya ni kuangalia kwenye tairi yako kuna sehemu imeandikwa kwa mfano huu "255/65/R16 91W" Maana ya tarakimu hizo ni 255 ni upana wa tairi, 65 ni urefu wa tairi kutoka kwenye rim, R16 ni saizi ya rim na hiyo 91W ndio tairi speed rating yenyewe. Kwa mfano huo juu gari lenye tairi hilo spidi rating yake ni W ambayo unatakiwa kutembea spidi ya mwisho ni 168 Miles/hour au 270Km/hour.

Na hii ndio chati ya Speed rating ya tairi zote unachotakiwa kuangalia ni Herufi

2 comments:

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages