SIKILIZA LIVE KUTOKA SOKO LA HABARI KARIAKOO...! - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

SIKILIZA LIVE KUTOKA SOKO LA HABARI KARIAKOO...!

Ndugu zangu,
Leo Jumatatu, Aprili 7, Redio yako ya Kijamii ya KwanzaJamii imeandika historia kwa kuwa redio ya kwanza hapa nchini kuwaletea wasikilizaji dondoo za habari za magazetini kutokea kwenye soko lenyewe la habari, ni  pale kona ya Uhuru na Msimbazi, Kariakoo.

Ni kipindi cha kila siku kuanzia saa kumi na moja na nusu alfajiri. Mwandishi/ Mtangazaji wa KwanzaJamii atakuwa sokoni hapo na kuungana moja kwa moja na studio za Kwanzajamii radio Iringa.

Sambamba na redio, habari hizo na picha za magazeti yenyewe zitarushwa pia kwenye Mjengwablog.com. Ikumbukwe, Mjengwablog ilikuwa ni blogu ya kwanza hapa nchini kuanza kurusha kwenye blogu dondoo za magazetini.

Usikose kufuatilia na kuzipata habari zikiwa motomoto kutoka Soko la habari Kariakoo...http://www.mjengwablog.com/habari-za-kijamii/item/10489-kutoka-soko-la-habari-kariakoo.html#.U0JH6ldQ7U4

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages