Mh Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu alipo zindua magari yalionunuliwa kwa ajili ya kupambana na Ujangili - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Mh Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu alipo zindua magari yalionunuliwa kwa ajili ya kupambana na Ujangili

 Mh Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu akitelemka katika moja ya gari ambalo alilizindua kwa ishara ya kuzindua magari mengine yote yatakayotumika kupambana na ujangili.
  Mh Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu  akielekea kuongea na wanahabari baada ya uzinduzi huo
 Haya ndiyo Magari ambayo yamezinduliwa Rasmi kwa ajili ya kupambana na majangili 
 Mh Waziri wa Maliasili na Utalii Lazaro Nyalandu akizungumza na wanahabari.Picha zote na Maliasili zetu Blog

HII NDIO HOTUBA YAKE KAMILI 


Ndugu Wanahabari:

Katika kutekeleza maazimio ya Bunge, na ahadi  ya serikali kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maliasili, Ardhi na Mazingira, leo nimekamilisha utaratibu wa kuzitoa silaha zilizokuwa  chini ya TRA tangu mwezi wa Novemba mwaka 2012, ili kuzikabidhi kwa wapiganaji katika Hifadhi za Taifa, Mamlaka ya Ngorongoro, na Mapori ya  Akiba kote nchini kwa lengo la kupambana na ujangili. Silaha hizi 500  aina ya AK47 ziligharimu jumla yaSh.427milioni kuzinunua, na leo Wizara  yangu inatoa Shs.212 milioni kwa ajili ya kulipia kodi na ushuru  mbalimbali ili Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA iziruhusu kutolewa.

Ndugu Wanahabari:

Kutokana na ukweli kwamba Pori ka Akiba la Selous lenye ukubwa wa kilometa za  mraba 55,000 lina ukubwa unaokaribia Hifadhi zote za Taifa chini ya  TANAPA ambazo zina ukubwa wa kilometa za mraba 57,000, na hivyo  kulifanya Pori la Akiba la Selous kuwa kubwa mno ki-menejimenti na 


kiundeshaji, na ili kuweka mazingira wezeshi ya kupambana kikamilifu 
katika vita inayoendelea dhidi ya ujangili, leo nachukua hatua 
zifuatazo:

1. Nazipandisha hadhi Kanda 8 zilizopo Pori la Akiba la Selous ili ziweze
kujitegemea kiundeshaji (Semi Autonomous status), chini ya Mkuu wa kila Kanda 

2.Naiagiza
Idara ya Wanyamapori ikamilishe mchakato wa kufungua akaunti maalumu za
benki kwa kila kanda ili kuwawezesha Wakuu wa Kanda hizi kutekeleza 
majukumu yao kwa ufanisi zaidi.

3. Mhifadhi Benson Kibonde 
ataendelea kuwa Meneja wa Pori lote la Selous kama ilivyo sasa na 
ataendelea kuwa msimamizi Mkuu wa Pori la Akiba la Selous, na atasaidiwa
na Wakuu wa Kanda wafuatao:

- Msafiri Mashiku​​- Mkuu, Kanda ya Matambwe
- Asterius Ndunguru​​- Mkuu, Kanda ya Msolwa
- Adili Y. Zella​​​- Mkuu, Kanda ya Liwale
- Bigilamungu Kagoma​- Mkuu, Kanda ya Kingupira
- William Millya​​- Mkuu, Kanda ya Kalulu
- Munhu J. Ndunguru​​- Mkuu, Kanda ya Miguruwe
- Ramadhani Mkhofoy​​- Mkuu, Kanda ya Ilonga
- Msiba Kombo​​- Mkuu, Kanda ya Likuyu-Sekamaganga.

Wakati
huo huo, tumechukua hatua za kuimarisha Kikosi Dhidi ya Ujangili KDU 
nchini zinazotekelezwa katika Kanda 8 nchi nzima na kuongozwa na Wakuu 
wa Kanda wafuatao:-


1. Paskal Mrina​- Mkuu, Kanda ya Kaskazini-Arusha
2. Faustine Masalu​- Mkuu, Kanda ya Mashariki- DSM
3. John Mbwiliza​- Mkuu, Kanda ya Serengeti- Bunda
4. Benjamin Kijija​- Mkuu, Kanda ya Ziwa- Mwanza
5. Charles Msilanga​- Mkuu, Kanda ya Magharibi-Tabora
6. Keneth Sanga​- Mkuu, Kanda ya Kati- Manyoni
7. Majid Lalu​​- Mkuu, Kanda ya Nyanda za Juu Kusini-Iringa
8. Ibeid Mmari​- Mkuu, Kanda ya Kusini- Songea.

Ndugu wanahabari:

Katika
jitihada za kuimarisha ulinzi wa Tembo na mapambano dhidi ya Ujangili 
katika Pori la Akiba la Selous, tunawashukuru washirika wetu katika 
Uhifadhi, Frankfurt Zoological Society kwa kutupa Magari matano (5) aina
ya Landrover. Nachukua nafasi hii kutangaza kuwa nagawa gari moja moja 
kwa Kanda zifuatazo ndani ya Pori la Akiba la Selous: 

Kanda ya Matambwe
Kanda ya Msolwa
Kanda ya Kiwale
Kanda ya Kingupira
Kanda ya Kalulu.

Aidha,
Mfuko wa Wanyamapori umenunua Magari 14 aina ya Toyota yenye thamani ya
Shs.1.63 bilioni na nachukua nafasi hii kutangaza mgao wake kwenye 
Vituo vya Wanyamapori vifuatavyo:-

1.
Pori la Akiba Selous-Kanda ya Likuyu Sekamaganga ​-​1
2.
Pori la Akiba Rungwa​​​​​​-​2
3.
Pori la Akiba Uwanda​​​​​​-​1
4.
Pori la Akiba Lukwati-PITI​​​​​-​1
5.
Pori la Akiba Kijereshi​​​​​​-​1
6.
Pori la Akiba Rukwa-LWAFI​​​​​-​1
7.
Pori la Akiba Burigi-Biharamulo-Kimisi​​​​-​1
8.
Pori la Akiba Lukwika-Lumesule-Msanjesi​​​-​1
9.
Pori la Akiba Moyowosi-Kigosi​​​​​-​1
10.
Pori la Akiba Maswa​​​​​​-​1
11.
Pori la Akiba Mkungunero​​​​​-​1
12.
Taasisi ya Taaluma ya Wanyamapori PASIANSI​​-​1
13.
Mfuko wa Kuhifadhi Wanyamapori (TWPF)​​​-​1

Ndugu wanahabari:

Hapa Makao Makuu ya Wizara kunatokea mabadiliko yafuatayo:
1.
Namteua Bw. Nurdin Chamuya, ambaye ni mwanahabari mzoefu, kuwa Msemaji 
wa Wizara ya Malisili na Utalii, na anachukua nafasi iliyokuwa 
inashikiliwa na Bw.Chikambi Rumisha ambaye anarudi kwenye Idara yake ya 
Sera na Mipango.

Ndugu wanahabari, 
Wizara ya Maliasili na 
Utalii inachukua hatua mahsusi kujenga uwezo wa watumishi wake na 
maaskari wanyamapori kupambana na kuushinda ujangili nchini. Nawaomba 
wananchi wote wajitolee taarifa zitakazosaidia kukamatwa kwa majangili 
kabla hawajaua Tembo na wanyama wengine. Tunamwomba kila raia awe sehemu
ya mapambano dhidi ya ujangili. Tunaiomba jumuiya ya Kimataifa na 
washirika wetu wa naendeleo waungane nasi katika mapambani haya.

Tanzania Bila Ujangili Inawezekana.
Mungu ibariki Tanzania.

Asanteni

Lazaro Nyalandu, Mb.
WAZIRI

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages