MATOKEO KURA ZA MAONI CCM JIMBO LA CHALINZE,RIDHIWANI KIKWETE ASHINDA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

MATOKEO KURA ZA MAONI CCM JIMBO LA CHALINZE,RIDHIWANI KIKWETE ASHINDA

Mtoto wa Rais Jakaya Kikwete,Ndugu Ridhiwani Kikwete akijipigia kura.

Leo kumefanyika Upigaji Kura za maoni kupitia chama cha CCM,jimbo la Chalinze,aidha Katika  uchaguzi  huo uliofanyika Ridhiwani Kikwete amishinda kwa kuibuka na kura 758 kati ya  kura 1321 zilizopigwa, huku mpinzani wake wa karibu  ambaye pia ni mdau mkubwa wa Soka hapa nchini,Ndugu Shaban Iman Madega ameibuka na kura 335.

Wengine  walioshiriki   katika uchaguzi huo ni pamoja na Athuman Ramadhan Maneno aliyepata kura  206 na Changwa Mohamed Mkwazu aliyeambulia  kura  12.

Katika uchaguzi huo jumla ya kura  zote  zilikuwa ni 1363 wakati  kura zilizoharibika ni 5 na Halali ni kura 1316, hivyo kwa matokeo  hayo  Kikwete  anasubiri vikao  vya juu  vya  chama  ili  kutoa baraka  kama ateuliwe   kuwa mgombea ama vinginevyo.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages