ABDULRAHMAN KINANA AFUNGA KAMPENI KWA KISHINDO KALENGA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

ABDULRAHMAN KINANA AFUNGA KAMPENI KWA KISHINDO KALENGA

1Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimnadi mgombea Ubunge wa jimbo la Kalenga kwa tiketi ya CCM Bw. Godfrey Mgimwa wakati wa mkutano wa kufunga kampeni katika jimbo la Kalenga kwenye kijiji cha Kidamali kata ya Nzihi wilaya ya Iringa vijijini mkoani Iringa, Uchaguzi wa jimbo la Kalenga unafanyika kesho machi 16 kuziba pengo la aliyekuwa mbunge wa jimbo hilo na Waziri wa Fedha na uchumi Marehemu Dr. William Mgimwa.(PICHA NA KIKOSI KAZI CHA FULLSHANGWE-KALENGA) 2Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi katika kata ya Nzihi wakati wa mkutano wa kufunga kampeni katika jimbo la Kalenga.
4Mgombea Ubunge wa jimbo la Kalenga kwa tiketi ya CCM Bw. Godfrey Mgimwa akiwahutubia wananchi katika mkutano wa kufunga kampeni.
5Wabunge wa CCM Rita Kabati na Lediana Mng'ong'o wakimsindikiza Robi Mgimwa mke wa mgombea ubunge wa jimbo la Kalenga kupitia CCM Godfrey Mgimwa kuelekea jukwaani 6 Mgombea Ubunge wa jimbo la Kalenga kupitia CCM akimtambulisha mke wake Robi Mgimwa wakati alipohutubia maelfu ya wananchi katika mkutano wa kufunga kampeni jimbo la Kalenga. 7 Mgombea Ubunge wa jimbo la Kalenga kupitia CCM akimtambulisha mke wake Robi Mgimwa wakati alipohutubia maelfu ya wananchi katika mkutano wa kufunga kampeni jimbo la Kalenga. 8
Mke wa Godfrey Mgimwa, Mgombea Ubunge wa jimbo la Kalenga kupitia CCM Robi Mgimwa akimuombea kura mme wake katika mkutano wa kufunga kampeni kata ya Nzihi jimbo la Kalenga leo. 10Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na Katibu wa CCM mkoa wa Iringa Bw. Hassan Mtenga katikati ni Godfrey Mgimwa mgombea ubunge wa jimbo la Kalenga kupitia CCM. 11Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Tumaini na mtangazaji wa ITV Godwin Gondwe mara baada ya kumalizika kwa mkutano huo. 12Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihani msiba katika kijiji cha Kidamali kata ya Nzihi 13Salim Asas Abri kamanda wa vijana CCM mkoa wa Iringa alikuwa ni mmoja wa wananchi waliohudhuria katika mkutano huo. 14Umati wa wananchi waliofurika katika mkutano huo. 15Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara na Waziri wa Fedha na Uchumi Mwigulu Nchemba akihutubia katika mkutano huo. 16Katibu wa CCM mkoa wa Mtwara Bw. Akwilombe akihutubia katika mkutano huo 17Mkurugenzi wa Fullshangweblog Bw. John Bukuku katikati akiwa na wahadhiri wa chuo kikuu cha Tumaini kulia ni Simon Berege na Godwin Gondwe kushoto. 18Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akifuatilia hotuba ya Mbunge wa jimbo la Mwibara Kangi Lugora hayupo pichani wakati alipokuwa akihutubia mkutano huo, kushito ni Mwigulu Nchemba Naibu Katibu Mkuu Bara na Godfrey Mgimwa mgombea ubunge wa jimbo la Kalenga kupitia CCM. 20Mbunge wa Mwibara Kangi Lugora akihutubiwa wananchi katika mkutano huo. 21Mbunge wa jimbo la Ludewa aDeo Filikunjombe kiwaomba wana Kalenga kumpa kura za ndiyo Godfrey Mgimwa. 23Msanii Dokii akitumbuiza katika kutano huo uliofanyika leo kata ya Nzihi.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages