Watu wawili wamepoteza maisha na wengine takribani 50 wakifukiwa kwenye vifusi baada ya paa la jengo la maduka lililokuwa linajengwa kuporomoka eneo la Tongaat Kaskazini mwa mji wa Durban nchini Afrika Kusini.
Watu 29 wameweza kuokolewa kutoka katika jengo hilo.
Madaktari kutoka kampuni ya Netcare 911 walifika kutoa huduma ya kwanza katika eneo hilo la Tongaat.
“Shughuli hii itachukua muda mrefu. Itatuchukua muda kuwafikia wale waliokwama,” alisema msemaji wa kampuni hiyo.
Hata hivyo ni mapema mno kujua sababu ya kuporomoka kwa jengo hilo.
Chanzo: BBCSWAHILI





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)