UJUMBE WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA KUTOKA CHINA WAKUTANA NA WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI, DAR ES SALAAM LEO - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

UJUMBE WA VIONGOZI WA SERIKALI ZA MITAA KUTOKA CHINA WAKUTANA NA WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI, DAR ES SALAAM LEO

PIX 1Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kushoto) akimkaribisha Kiongozi wa msafara wa ujumbe kutoka Serikali za Mitaa za China, Makamu Gavana wa Jimbo la Shandong,  Xia  Geng kwenye  Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, jijini Dares Salaam. Ujumbe huo umehusisha magavana na wafanyabiashara kutoka nchini China ambapo ulikutana na Waziri Nchimbi pamoja na Watendaji Wakuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Lengo la mkutano huo ni kudumisha ushirikiano katika masuala ya biashara na uchumi na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. 
PIX 2Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kulia-meza kuu) akizungumza jambo na Kiongozi wa msafara wa ujumbe kutoka Serikali za Mitaa za China, Makamu Gavana  wa Jimbo la Shandong  Xia  Geng (kushoto-meza) kwenye  Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, jijini Dares Salaam. Wa kwanza kushoto kwa Waziri Nchimbi ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Mwamini Malemi, anayefuata ni Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP) Said Mwema na Mkuu wa Jeshi la Magereza, John Minja. Ujumbe huo umehusisha magavana na wafanyabiashara kutoka nchini China ambapo ulikutana na Waziri Nchimbi pamoja na Watendaji Wakuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Lengo la mkutano huo ni kudumisha ushirikiano katika masuala ya biashara na uchumi na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. PIX 3Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kulia) akimkabidhi zawadi Kiongozi wa msafara wa ujumbe kutoka Serikali za Mitaa za China, Makamu Gavana  wa Jimbo la Shandong  Xia  Geng kwenye  Ukumbi wa Mikutano wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, jijini Dares Salaam. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwamini Malemi. Viongozi hao walipeana zawadi ikiwa ni ishara ya kuonyesha ushirikiano kati ya China na Tanzania. Ujumbe huo umehusisha magavana na wafanyabiashara kutoka nchini China ambapo ulikutana na Waziri Nchimbi pamoja na Watendaji Wakuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Lengo la mkutano huo ni kudumisha ushirikiano katika masuala ya biashara na uchumi na Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi. Picha na Wizara ya Mambo ya Ndani.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages