MPO AFRIKA YATWAA UBINGWA SAFARI POOL TEMEKE - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

MPO AFRIKA YATWAA UBINGWA SAFARI POOL TEMEKE

Baadhi ya wachezaji wa Klabu ya Mpo Afrika wakishangilia na Kikombe mara baada ya kuibuka mabingwa katika fainali za mashindano ya Safari Pool Taifa ngazi ya Mkoa,Mkoa wa Temeke iliyofanyika Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.Mpo Afrika ilishinda 13-11 dhidi ya Klabu ya Sun City.

 Katibu Mkuu wa chama cha Pool Taifa(TAPA), Amos Kafwinga akimkabidhi zawadi ya fedha taslimu shilingi 350,000/= bingwa wa mchezaji mmoja mmoja wanaume(Singles), Sulemani Cato mara baada ya kumfunga Nahodha wa timu ya Taifa Charles Venance 4-2.Dar es Salam mwishoni mwa wiki.
Mchezaji wa timu ya Klabu ya Mpo Afrika na Nahodha wa timu ya Taifa, Charles Venance akicheza wakati wa mechi ya fainali dhidi ya klabu ya Sun City wakati wa mashindano ya Safari Pool Taifa Ngazi ya Mkoa,Mkoa wa Temeke iliyofanyika mwishoni mwa wiki.

Na Mwandishi Wetu.
TIMU ya Mpo Afrika ya Mkoa wa kimichezo ya Temeke jijini Dar es Salaam imetwaa ubingwa wa mkoa baada ya kuifunga timu ya Klabu ya Sun City 13-11, katika fainali za mashindano  ya mchezo wa Safari Pool Taifa ngazi ya Mkoa yaliyomalizika mwishoni mwa wiki katika ukumbi wa Klabu ya Bushnet Mtoni Mtongani jijini Dar es Salaam. 
Mpo afrika kwa ushindi huo ilizawadiwa Kikombe, fedha taslimu shilingi 700,000/= pamoja na tiketi ya kuwakilisha Mkoa wa Temeke katika fainali za kitaifa zinazotarajiwa kufanyika mwezi ujao Mkoani Morogoro.

Nafasi ya pili ilichukuliwa na klabu ya Sun City na hivyo kuzawadiwa fedha taslimu shilingi 350,000/= na nafasi ya tatu katika mashindano hayo ilichukuliwa na Klabu ya Kurasini ambayo ilizawadiwa fedha taslimu shilingi 200,000/=  na mshindi wa nne ni klabu ya Bushnet ambao ndio walikuwa wenyeji wa mashi ndano hayo.

Upande wa mchezaji mmoja mmoja wanaume(Singles), Mchezaji waKlabu ya Bushnet, Sulemani Kato(Shetani) alifanikiwa kuchukua ubingwa kwa kumfunga Charles Venance 4-2 na kujinyakulia zawadi ya fedha taslimu shilingi 350,000/= pamoja na tiketi ya kuwakilisha Mkoa wa kimichezo wa Temeke katika fainali za kitaifa Mkoani Morogoro.

Nafasi ya pili ilichukuliwa na mchezaji Charles Venance kutoka klabu ya Mpo Afrika ambapo alizawadiwa fedha taslimu shilingi  200,000/=  na nafasi ya tatu ilichukuliwa na mchezaji, Amos Boniphace ambaye alizawadiwa 150,000/= na nafasi ya nne ni Hassan Abdubakar.
Upande wa mchezaji mmoja mmoja wanawake (Singles), Beatrice Charles alitwaa ubingwa kwa kumfunga Madina Idd 4-0 na hivyo kujinyakulia zawaadi ya fedha taslimu shilingi 250,000/= pamoja na tiketi ya kwakilisha mkoa wa Temeke katika fainali za kitaifa mkoani Morogoro.

Madina Idd ailichukua nafasi ya pili na hivyo kuzawadiwa fedha taslimu shilingi 150,000/= .Nafasi ya tatu ilichukuliwa na Manka Mushi ambaye alizawadiwa fedha taslimu shilingi 100,000/= na nafasi ya nne ni Rebeka Magaigwa ambaye alizawadiwa fedha taslimu shilingi 50,000/=.

Akizungumza na wachezaji kutoka vilabu vyote, Katibu wa chama cha Pool Taifa(TAPA), Amos Kafwinga aliwaomba klabu iliyotwaa ubingwa na ambayo itawakilisha mkoa wa Temeke katika fainali za kitaifa mkoani Morogoro kujiandaa vyema kwani ushindani ni mkubwa huko wanakoelekea na pia wazingatie nidhamu kwani bila nidhamu inaweza kuwafanya wasifanye vizuri mbele ya safari.

Mwisho aliwshuikuru TBL, kupitia bia ya Saafari Lager kwa kuendelea kufadhili mashindano hayo ambapo aliwaomba wapenzi wa pool kunywa Safari Lager ili waendelee kuwa wafadhili wakuu wa mashindano ya Pool. 

Mashindano ya Safari Pool Mkoa wa kimichezo wa Kinondoni ulishirikisha vilabu tisa ambavyo ni Mpo Afrika, Sun City, Kurasini,Bashnet,BMK,Sifa Mtoni,MTN,Amazoni na SuperStar.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages