Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Bernard K. Membe Afungua Rasmi Mkutano wa Tume ya Ushirikiano kati ya Tanzania na India - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa,Bernard K. Membe Afungua Rasmi Mkutano wa Tume ya Ushirikiano kati ya Tanzania na India

 Kaimu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Rajabu Gamaha akizungumza machache kabla ya ufunguzi rasmi wa mkutano huo. Anayeonekana pembeni ni Mhe. John Kijazi, Balozi wa Tanzania nchini India.
 Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akifungua rasmi Mkutano wa Tume ya Pamoja ya Kudumu ya Ushirikiano (Joint Permanent Commission-JPC) kati ya Tanzania na India unaofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency-Kilimanjaro kuanzia tarehe 08 hadi 09 2013. Mkutano huo unaowashirikisha Wadau kutoka sekta mbalimbali za hapa nchini na India utajadili pamoja na mambo mengine masuala ya ushirikiano katika sekta za Uchumi, Ufundi, Sayansi na Teknolojia, Elimu, Afya, Utalii, Kilimo na Nishati na Madini.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya India, Mhe. Preneet Kaur akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano huo.
Meza kuu kabla ya ufunguzi.
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bw. Omar Mjenga (kulia) akiwa na Mjumbe kutoka India wakati wa Mkutano huo.
Wadau wakisikiliza kwa makini hotuba ya Mhe. Kaur (hayupo pichani)
 Wadau wengine wakati wa ufunguzi wa mkutano huo.
 Wadau kutoka sekta mbalimbali za hapa nchini  wakimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) wakati wa uzinduzi huo.
 Wadau zaidi.
 Wadau kutoka India.
 Wajumbe wa Sekretarieti wakati wa mkutano huo.
 Mhe. Membe na Mhe. Kaur wakizungumza na Waandishi wa Habari mara baada ya ufunguzi wa mkutano wa Tume ya Ushirikiano kati ya Tanzania na India.
Mhe. Membe na Mhe. Kaur walioketi, katika picha ya pamoja na wajumbe wa mkutano huo.Picha na Reginald Philip na Olga Chitanda

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages