MSONDO NGOMA MUSIC YAINGIA STUDIO NA KUTANGAZA RATIBA YA IDDI - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

MSONDO NGOMA MUSIC YAINGIA STUDIO NA KUTANGAZA RATIBA YA IDDI

SUPER D
BENDI Kongwe ya Mziki wa dansi nchini Msondo Ngoma imeingia Studio kurekodi nyimbo zake mpya zitakazokuwa katika Albam moja akizungumza na waandishi wa habari Msemaji wa Bendi Hiyo Rajabu Mhamila 'Super D' amesema kuwa bendi yake kwa sasa imeingia studio kukamilisha kurekodi nyimbo zao mpya
Alizitaja nyimbo hizo kuwa li Suluhu uliotungwa na Shabani Dede,Lipi Jema na Baba Kibebe wa Eddo Sanga,Nadhili ya mapenzi wa Juma Katundu,Kwa momba akuna Uridhi ,Machimbo nyimbo zote hizo zikikamilika zitawekwa kwenye albam moja kwa ajili ya kuwapa raha mashabiki wao wawapo majumbani

Super D aliongeza kuwa bendi hiyo kwa sasa imesimamisha maonesho yake lakini watakapoanza sikukuu ya Idi mosi watatoa burudani katika ukumbi wa DDC Kariakoo idi pili watakua TTC Chang'ombe na idi tatu watavuka bahari kuelekea visiwa vya karafuu na kufanya onesho lao Zanzibar

Bondi hiyo kwa sasa inatamba na nyimbo zake mbalimbali wameweka nia ya kukonga mashabiki wa bendi hiyo kwa kupiga nyimbo mpya na zazamani ili kila mtu apate burudani unajua bendi yetu kongwe lazima tutoe burudani za aina tofauta aliongeza Super D

Bendi hiyo iliyopata umarufu mkubwa miaka ya nyuma imewahakikishia wapenzi wake kurudi katika ubora ule ule kama ilivyokuwa awari

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages