Hapa ndipo Mwili wa Marehemu Albert Mangwea ulipopumzishwa leo Mkoani Morogoro
Baada ya siku kadhaa zilizokuwa na kila aina ya harakati, ugumu na
majonzi makubwa, Albert Mangweha aka Ngwair hatimaye leo amezikwa kwenye makaburi
ya Kihonda mkoani Morogoro ambako ni nyumbani kwao.
Kabla ya kuzikwa, wananchi wa Morogoro walipata fursa ya kuuaga mwili
wake kwenye uwanja wa Jamhuri. Umati mkubwa wa wananchi ulijitokeza
kutoa heshima zao za mwisho kwa mwili wa Ngwair aliyefariki nchini
Afrika Kusini, wiki iliyopita. Wasanii wengi kutoka Dar es Salaam nao
wamehudhuria mazishi hayo.
“Marehemu Albert Mangweha azikwa kishujaa sana ni umati usioelezeka mungu akulaze mahali pema peponi,” ameandika Izzo B kwenye Instagram.
Naye Lady Jaydee kupitia Twitter ameandika: Mpaka hapa tulipomsindikiza
panatosha. Mungu amrehemu, kazi tumeimaliza. Life goes on.”
Picha kutoka kwenye akaunti za Instagram za Millard Ayo, Mboni Masimba na Mwasiti. (140)
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)