BARNABA, KIDUMU KUSHEREHESHA MATEMBEZI YA HISANI 'STEP AHEAD WALK 2013 - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

BARNABA, KIDUMU KUSHEREHESHA MATEMBEZI YA HISANI 'STEP AHEAD WALK 2013

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano wa Barclays, Tunu Kavishe, akizungumza na waandishi wa habari (hawao pichani), wakati wa uzinduzi wa Matembezi ya Hisani ya Step Ahead Walk 2013 yatakayosindikizwa na Barnaba na Kidumu.
 
*********************************
'Step Ahead Walk’ ni mkakati endelevu wa Benki ya Barclays, ambao kusudi lake ni kujenga uelewa wa kusaidia mahitaji muhimu katika jamii. Matembezi hayo ya kila mwaka, yalizinduliwa mwaka 2008 hapa nchini na kusaidia kuelimisha jamii kuhusu uchangishaji fedha ili kusaidia masuala ya uzazi na afya ya watoto

KIBAO cha ‘Wanawake,’ kilichoimbwa na nyota Bongo Flava Barnabas Elias, akishirikiana na Mrundi Jean Pierre Nimbona ‘Kidumu,’ kimezinduliwa rasmi leo na kutangazwa kupamba Matembezi ya Hisani ya ‘Step Ahead Walk 2013,’ yanayoratibiwa na Benki ya Barclays Tanzania.

Akizungumza na waandishi wa habari katika uzinduzi huo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano na Mahusiano wa Barclays, Tunu Kavishe, alisema maudhui ya wimbo huo ni kuhamasisha wadau kujitokeza kwa wingi kushiriki ‘Step Ahead Walk’ ambayo lengo lake ni kuchangisha pesa kwa ajili ya kinamama na watoto wachanga.

Aliongeza kuwa, tukio hilo litafanyika Juni 8, 2013, katika hoteli ya Golden Tulip, likihusisha matembezi ya hisani ya kilomita tano, ambapo kila mtu katika jamii anakaribishwa kushiriki kwa kununua tiketi kwa silingi za Kitanzania 5,000 ambazo zinapatika katika matawi ya Benki ya Barclays kuanzia Aprili 29.

“Mwaka 2011, Benki ya Barclays na washiriki wake walifanikiwa kukusanya shilingi mil. 150 kutokana na mauzo ya tiketi na matoleo mengine kutoka kwa wafadhili, lakini mwaka huu lengo ni kuchangisha mara mbili ya kiasi hicho kutoka kwenye matoleo ya washirika muhimu na washiriki wengine katika jamii,” alisema Kavishe.

Alibainisha kuwa, kiasi kitakachochangishwa mwaka huu kitakwenda kusaidia katika masuala ya uzazi na afya ya watoto, ikiwamo Mafunzo kwa wakunga wa uzazi, matibabu ya Fistula na upasuaji kwa watoto waliozaliwa na ulemavu unaosababishwa na uzazi.

‘Step Ahead Walk’ ni mkakati endelevu wa Benki ya Barclays, ambao kusudi lake ni kujenga uelewa wa kusaidia mahitaji muhimu katika jamii. Matembezi hayo ya kila mwaka, yalizinduliwa mwaka 2008 hapa nchini na kusaidia kuelimisha jamii kuhusu uchangishaji fedha ili kusaidia masuala ya uzazi na afya ya watoto.

Kavishe alisisitiza kuwa, ‘Step Ahead Walk 2013’ itafanikiwa, kama tu itawezeshwa na kila mshiriki na jamii nzima ya Kitanzania, kwa hiyo akawataka wadau kujiunga katika matembezi hayo ili kuweza kuleta mabadiliko katika masuala ya afya ya Uzazi na Mtoto kwa ujumla hapa Tanzania. Kwa Hisani ya Habari Mseto Blog

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages