Kamati maskuli zahimizwa kushajiisha wananchi kukabiliana na changamoto - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Kamati maskuli zahimizwa kushajiisha wananchi kukabiliana na changamoto

Mke wa Mbunge wa Jimbo la Kitope Mama Asha Suleiman Iddi akimkabidhi Bwana Zaid Omar Nahoda Shilingi Milioni tatu{3,000,000/-} zilizotolewa na Balozi Seif kama fidia ya nyumba yake baada ya kuridhia eneo ilipo nyumba yake litumike kwa shughuli za maendeleo ya majengo ya Skuli ya Msingi Mgambo.

 Mke wa Mbunge wa Jimbo la Kitope Mama Asha Suleiman Iddi akimkabidhi Bwana Zaid Omar Nahoda Shilingi Milioni tatu{3,000,000/-}zilizotolewa na Balozi Seif kama fidia ya nyumba yake baada ya kuridhia eneo ilipo nyumba yake litumike kwa shughuli za maendeleo ya majengo ya Skuli ya Msingi Mgambo.Picha na Hassan Issa-Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar
--

Kamati za maskuli katika maeneo yenye upungufu wa madarasa Nchini zimehimizwa kuwashajiisha wananchi wa maeneo yao kujikita zaidi katika ushirikiano wa kukabiliana na changa moto hizo ili kuwapa fursa nzuri watoto wao wa kusoma kwa utulivu.
 
Mke wa Mbunge wa Jimbo la Kitope Mama Asha Suleiman Iddi alitoa himizo hilo wakati wa hafla fupi ya kukabidhi Shilingi Milioni 3,000,000/- zilizotolewa na Mbunge wa Jimbo hilo Balozi Seif Ali Iddi kwa ajili ya kulipwa fidia Bwana Zaid Omar Nahoda aliyejitolea kubomoa nyumba yake kupisha eneo hilo kutumiwa kwa maendeleo ya ujenzi wa majengo ya Skuli ya Mgambo.
 
Makabidhiano hayo yaliyoshuhudiwa pia na Uongozi wa Serikali na CCM Wilaya ya Kaskazini B, Kamati ya Skuli,Wazazi pamoja na Wananfunzi imefanyika katika Skuli ya Msingi ya Mgambo iliyomo ndani ya Jimbo la Kitope Wilaya ya Kaskazini B.
Mama Asha alisema kutokana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia yaliopo Duniani hivi sasa Wazazi wanapaswa kuwajengea mazingira yanayolingana na mabadiliko hayo watoto wao ili wasome kwa uhakika katika kukabiliana na changamoto zilizowazunguuka.
 
Aliwaasa wanafunzi wa skuli hiyo kuonyesha jitihada zao katika masomo yao wakielewa kwamba suala la elimu ni la lazima sambamba na kuwapa faraja wazazi wao.
 
Akizungumzia tatizo kubwa na ajali za bara barani kutokana na mwendo wa kasi unaofanywa na baadhi ya madereva wanaotumia bara bara iendayo kaskazini Mama Asha aliziomba Halmashauri za Wilaya za Kaskazini A na B kushirikiana pamoja katika kulitafutia ufumbuzi tatizo hilo.
 
Alisema baadhi ya madereva hao wanasahau kwamba bara bara hutumiwa na watu wote waliwemo watoto na walemavu. Hivyo ipo haja kwa taasisi zinazohusika kuzitupia macho sheria za usalama bara barani ili ziweze kuongezewa nguvu zaidi.
 
Mapema akitoa taarifa ya Skuli hiyo Mwalimu Mkuu msaidizi wa Skuli ya Mgambo Ndugu Salim Seif alisema skuli hiyo bado inaendelea kukabiliwa na changa moto kadhaa ikiwemo Ukosefu wa Maabara, walimu wa sayansi pamoja na utanuzi wa majengo ya skuli kwa lengo la kukabiliana na ufinyu wa madarasa. 
 
Wakati huo huo Mke wa Mbunge wa Jimbo hilo la Kitope Mama Asha Suleiman Iddi alikabidhi Vifaa mbali mbali kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Elimu ya Maandalizi cha Dhin Noorayn kilichopo katika Kijiji cha Fujoni.
 
Akikabidhi Vifaa hivyo vilivyotolewa na Mbunge wa Jimbo hilo Balozi Seif Ali Iddi kutimiza ahadi aliyoitoa kwa uongozi wa Kituo hicho wakati wa ziara yake Mama Asha aliwaomba wazazi kujitahidi kuchangia vituo hivyo ili kuwapa moyo walimu wanao wahudumia watoto wao.
Mama Asha alifahamisha kwa vituo vya maandalizi mara nyingi vimekuwa vikisaidia kutoa fursa kwa wazazi kusaidiwa ulezi hali inayowapa muda wa kujikita zaidi katika harakati zao za kiuchumi na maendeleo.
Mapema Mwalimu Mkuu msadizi wa Kituo hicho cha Dhin Noorayn Bibi Hawana Abdulla kwa niaba ya uongozi na walimu wa kituo hicho wameelezea faraja yao kutokana na ushirikiano wanaoupata wa uendelezaji wa kituo hicho.
Vifaa hivyo vya ujenzi ambavyo ni pamoja na Bati, misumari, mbao, miti, matofali, mchanga vimegharimu zaidi ya shilingi milioni 4.9.

Na 
Khamis Ame, 
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages