Bingwa wa Botswana katika uzito wa bantamweight Leslie Sekotswe amekuwa mtu wa hatari kiasi kwamba anamtishia maisha bondia Immanuel Naidjala a.k.a “Prince” wa namibai katika mpambano wao utakaofanyika tarehe 20 siku ya Jumatano jijini Windhoek, namoibia.
Wawili hao wanakutana katika kugombea mkanda wa IBF wa Kimataifa (IBF International Title) katika uzito wa Bantam.
Leslie ambaye alianza ngumi
wakati Immanuel akiwa bado kinda ana rekodi ya kuwapiga wapinzani wake
kwa KO katika raundi za mwanzo na ameapa kumpa kipigo kitakatifu
Naidjala wakati watakapokutana katika Casino ya Country Resort Club
jijini Windhoek, Namibia chini ya promota Nestor Tobias wa kampuni ya
Sunshine Boxing Productions iliyoko nchini Namibia.
Hii ni mara ya kwanza kwa nchi
ya Namibia kufanya mpambano wa hadhi ya IBF la kimataifa na wapenzi wa
ngumi wa Namibia wamejawa na furaha kutaka kuliona pambano hili
litakalowakutanisha mabondia wawili waliosheheni kwa kila kigenzo cha
sifa ya juu.
Huu ni mwendelezo wa IBF Afrika
wa kuleta mapambano zaidi ya 100 barani Afrika mwaka huu katika programu
yake ya Utalii wa Michezo na tarayi nchi mbalimbali zimejipanga kuandaa
mapambano kadhaa wa kadha Tanzania ikowamo!





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)