"MWANAMKE MWEYE KOVU JEUSI" hadithi ya kusisimua - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

"MWANAMKE MWEYE KOVU JEUSI" hadithi ya kusisimua

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgtvFtrfvJlaX2sWoZND3-53Qunvibrc9YLce-RILrpfqIY0D_wEvS0CnGrvavCGKQqiBWaReq11NXIFiLAfN7xlK59PI2lrypjiwGRfjfiIlyxqJfA06QFZ4hTu7ygksKgczrOllXjbQka/s1600/SAM_1393.JPG
AMANI KIZUGUTO
MTUNZI
0717-376735 
Nakumbuka vizuri ilikuwa siku ya jumapili ambayo kama ilivyoada kwangu huwa sikosi kwenda kanisani hasa misa ya kwanza kwani huwa napenda sana kusali misa ya kwanza ili baadaye niweze kuendelea na mambo yangu mengine,siku hiyo niliamka asubuhi na mapema kutoka pale nyumbani kwangu mnazi mmoja karibia na ofisi za chama cha mapinduzi za mkoa wa Dar-es-salaam na kuelekea kanisani pale saint.alban posta taratibu kwa miguu kwani gari yangu ilikuwa imeharibika wiki ya pili sasa na isitoshe pale nyumbani kwangu mpaka pale posta hapakuwa mbali sana kiasi cha kama dakika 20 tu hasa kwa kijana kama mimi ambaye damu ilikuwa bado inachemka.niliingia pale kanisani nikiwa sijachelewa sana misa ilikuwa imeanza kama dakika 7 hivi nakumbuka sana somo la siku hiyo alilolitoa padri Kiaka lilikuwa linahusu umuhimu wa kuombea siku yako ya kufa kwani haina siku wala saa.


Misa ilipoisha mida ya saa 3 asubuhi niliona nijivute mpaka mitaa ya upanga pale nyuma ya diamond jubilee mwendo wa pole pole nikamuone  rafiki yangu Martin ambaye pia alikuwa ni mfanyakazi mwenzangu. Sikutaka hata kumtaarifu kwenye simu kwani simu yangu haikuwa na pesa pia nilijua kwa kuwa tuliahidiana jana kwamba kesho nikitoka kanisani nitaenda kwake basi haina shaka nitamkuta tu kwani pia Martin huwa sio mzururaji sana hasa mida ya asubuhi kama haendi kazini.Wakati naingia ndani kwa rafiki yangu kipenzi  Martin nakumbuka ilikuwa ni mida ya saa 4 asubuhi mlangoni nilipishana na mdada wa makamo mweusi kiasi ambaye nakumbuka vizuri alikuwa amevalia dela la rangi ya kijani kibichi likiwa linamichirizi ya rangi ya zambarau na kwa ndani alikuwa amevaa suruali ya jeans ya rangi  nyeusi huku kichwani akiwa amejifunga mtandio mweusi kufunika nywele zake nilimsalimia aliitikia haraka haraka huku akikwepesha sura yake na huku akionyesha ni mtu aliyekuwa na shauku ya kuondoka lile eneo haraka sana, mimi hata sikumjali nilijua atakuwa ni mmoja kati ya wasichana ambao alikuwa na uhusiano nao bwana Martin kwa kuwa rafiki yangu Martin alikuwa ni mtu aliyependa sana wasichana,nilifika mpaka pale alipokuwa amepanga Martin ilikuwa ni nyumba ya uwani akiwa amepanga chumba na sebule huku nyumba ya mbele kukiwa hakuna mtu hata mmoja aliyekuwa amepanga kwa maelezo yake ile nyumba ya mbele kulikuwa na mpangaji lakini amehama na sasa mwenye nyumba alikuwa yupo akiifanyia marekebisho tayari kwa kuingia mpangaji mwingine. Ile nimefika tu mlangoni nikakuta mlango upo wazi kitu ambacho kikawaida sio busara kuingia nyumba ya mtu bila kugonga basi nikajivuta pale mlangoni na kuanza kuugonga ule mlango hallow Martin hallow  niligonga kama dakika tano bila kupata jibu lolote kutoka mule ndani ilinibidi nishangae kidogo kwa maana hata kama angekuwa msalani ni lazima angesikia ile sauti yangu na kwa nini akae kimya sikuamini kama alikuwa amelala wakati nimepishana na Yule dada anatoka chumbani kwake muda si mrefu,ikanibidi niingie tu ndani kama hayupo atanikuta mule mule nikimsubili, mungu wangu sikuamini nilipoingia pale sebuleni kwake nilikutana na michirizi ya damu kutoka pale sebuleni kuelekea chumbani kwake mh ikanibidi nipitilize haraka moja kwa moja kule chumbani kwake ile kuingia tu nikakutana na mwili wa Martin akinikodelea macho huku ukiwa umekakamaa huku pia ukiwa  umegandana na damu na alama kubwa ya kisu kwenye shingo yake,nilimkimbila pale alipokuwa amelazwa na kumuangalia mungu wangu alikuwa tayari ameshakufa,nilifikiria pale haraka haraka ni kipi nifanye nikaanza kuitafuta simu yake mule ndani mpaka nikaipata nikawapigia simu polisi na kuwaeleza lile tukio sikutaka nijihusishe moja kwa moja na lile tukio ndio maana niliamua kutumia simu yake pia simu yangu nilikuwa bado sijaweka vocha kisha nikaanza kutoka nje kabla sijatoka nje ya chumba chake macho yangu yakatua kwenye meza ndogo iliyokuwa mule chumbani kwake mara nikakutana na karatasi imeandikwa kwa Wino Mwekundu 
“NILIYEMUUWA NI MIMI MWANAMKE MWENYE KOVU JEUSI” shiti moyo ulijikuta unasisimuka na kuanza kudunda dunda kwani lile jina si mara ya kwanza kwangu kukutana nalo hasa kwenye kazi zangu,mungu wangu huyu mwanamke amemuuwa tena na Martin? Martini amemfanyaje tena huyu mwanamke hatari kama amemuuwa na Martin basi na mimi siku zangu haziko mbali hapana inabidi nimzibiti kwa kila hali nilijikuta nimekaa naangalia ile karatasi aliyoandika huku nikiutazama na mwili wake pale chini kwa muda wa dakika kadhaa mpaka machozi yakaanza kunitiririka kwa mbali,nilishitushwa na kelele zilizotoka nje nikahisi polisi watakuwa tayari wameshafika pale basi nikaona haina haja ya kuondoka tena nikachukuwa  shuka pale na kuanza kuufunika ule mwili hallow inspector vipi tayari umeshafika? Habari umeipataje? Ilikuwa ni sauti ya bwana Gerald mmoja wa ma afisa upelelezi pale makao makuu, ndio mimi niliyewapigia simu nilimjibu kwa mkato huku nikimsaidia kutoa vifaa vya kuchukulia finger print pamoja na camera digital ya kipelelezi kupiga picha mule chumbani kwa ajili ya kupata nyayo zake na alama zingine za Yule muuwaji,mkuu wangu wa kazi pia inspector Thomas na yeye pia alikuwa ni mmoja ya watu waliokuwa wamefika pale kwa ajili ya kushuhudia lile tukio wakati kina inspector Gerald wakiendelea kukusanya baadhi ya kumbukumbu mule ndani bosi wangu aliniita nje alipiga simu hospitali ya taifa ya muhimbili kuwajulisha kuhusu lile tukio kisha akaanza kuniuliza maswali kadhaa kuhusu lile tukio aliniuliza kwanza nilijuaje kama Martin amekutwa na lile tukio nikamjibu mimi mwenyewe imetokea tu kama bahati kwani tulikuwa tumepanga kukutana naye siku ya leo nikitoka kanisani ili tuelekee bagamoyo kusherekea siku ya mchumba wake ya kuzaliwa,ndio na mbona hili tukio tumejulishwa kupitia simu yake aliendelea kunihoji, ni mimi ndiyo nilitumia simu yake kuwajulisha kwani simu yangu haina pesa kabisa, je huyo muuwaji unamjua au unaweza kuwa unamhisi nani? Ni MWANAMKE MWENYE KOVU JEUSI bosi wangu alijikuta anashituka ohh wewe umejuaje? Aliniuliza kwa shauku kubwa ya kutaka kujua nimefahamu vipi aliyefanya lile tukio ni mwanamke mwenye kovu jeusi nikamwambia kuwa kama kawaida yake ameacha note juu ya meza mule chumbani mwa Martin ameandika kwa wino mwekundu, basi bosi wangu alinituma nikamletee ile karatasi aliyoiacha huyo mwanamke mwenye kovu jeusi,basi nilienda na kutoka nayo pale nje na kumpa aiangalie, aliiangalia kwa muda wa kama dakika 2 hivi halafu akaludisha macho kwangu na mimi muda ule nilikuwa pia nimemetolea macho basi tukajikuta tumetoleana wote macho,hivi hakuna anayemjua huyu muuwaji? Kwa maana sasahivi amezidisha haya mauaji alianzisha tena mazungumzo,
simjui ila uwezo wa kumpata upo kwa nini asipatikane kwa maana tukimchekea tutajikuta na sisi wote anatuondoa wakati nazunguma haya tayari gari ya kubebea wagonjwa kutoka muhimbili hospitali ilikuwa tayari imeshafika pale nyumbani kwa marehemu Martin tayari kwa kuchukua ule mwili kuupeleka hospitali ili ufanyiwe pia uchunguzi mwingine wa kitabibu .Wale manesi walishuka kutoka ndani ya ya ile gari ya kubebea wagonjwa na kuingia mule ndani tayari kwa kuuchukuwa ule mwili kwa ajili ya kuupeleka hospitali.
                             *************************************
Baada ya mwili kuondolewa pale nyumba ambayo  Martin alikuwa amepanga kwenda hosptali kwa ajili ya uchunguzi zaidi bosi wetu inspekta Thomas alituita wafanyakazi wote pamoja na askari kanzu ambao tulikuwa pale kwenye lile tukio,ndio nimewaita hapa tuzungumze kidogo nazani mmeona tukio lililotokea leo,hii hi fedheha sana kwa jeshi la polisi, huyu mwanamke haiwezekani tumshindwe kiasi hiki mwanzo alikuwa anawauwa watu wengine lakini sasahivi ameingia mpaka kwenye jeshi letu lapolisi, hapa maswali ya kujiuliza haraka haraka ni kwamba huyu mwanamke amejuaje kama Martin ndio alikuwa anajukumu la kufuatilia hili faili lake? Inamaana kuna watu ndani ya ofisi yetu watakuwa wanampa siri huyu mwanamke bosi alianza kuzungumza huku akionyesha kwenye sura yake wazi kwamba kile kitendo kilikuwa kimemuumiza sana.
Basi taratibu mkuu haya tutaenda kuyazungumza ofisini mkuu maana hapa tulipo hatuwezi kujua inawezekana akawa bado yupo au ameweka hata vinasa sauti maana inaonekana huyu mtu ni hatari sana ,ilikuwa ni sauti ya Jamira mmoja wa askari shupavu sana tuliokuwa nao pale kituo cha kati kwenye jeshi letu la polisi, ilionekana bosi aliafiki ule ushauri aliopewa na Jamira kwani baada ya hapo alituambia ya kwamba tunaweza kwenda huku akimwabia Gerald ahakikishe baadaye wanakutana ofisini kwake.
                                     *******************************
Habari ya kifo cha kutatanisha cha Martin kila mmoja pale ofisini kilimhudhunisha sana kwani Martin alikuwa mmoja ya vijana wachapakazi sana pale ofisini hadi siku umauti yanamkuta nakumbuka yeye ndio alikuwa mtu anayefuatilia faili la huyu mtu aliyekuwa akijiita MWANAMKE MWENYE KOVU JEUSI sasa tena na yeye kuuliwa na mtu aliyejitambulisha kwa jina hilo kila mtu alishituka sana.
Basi baada ya uchunguzi wa kitabibu hospitali ya taifa Muhimbili kukamilika ilibidi zianze taratibu za kusafirisha mwili wa marehemu. Tuliusafirisha mwili wake mpaka wilayani Bunda ambapo ndipo palikuwa nyumbani kwa wazazi wake. Na mimi ni mmoja ya watu tuliochaguliwa na bosi wangu kusindikiza maiti ya marehemu nadhani hili lilitokana na ukaribu wangu baina ya mimi na Martin. mazishi yake yalifanyika huko kwao kwenye kijiji kilichojulikana kwa jina la Kasunguti,kwa mimi ilikuwa ni mara yangu ya kwanza kufika mkoa wa Mara toka nizaliwe mara nyingi safari zangu nyingi nilikuwa naishia mkoa wa Mwanza tu. Nakumbuka siku ile tulipoingia nyumbani kwa wazazi wake tulikuta umati wa watu wengi sana, wazazi wake walikuwa hawaamini kama mtoto wao amefariki mpaka pale walipoliona jeneza likishuka kutoka kwenye gari iliyokuwa imebeba ile maiti ya Martin. Mama yake alikuwa akilia huku akilalamika ya kwamba Martini ndio alikuwa mtoto tegemewa kwani alikuwa anawasomesha wadogo zake watatu sasa sijui watafanyaje. Sikuamini siku ile kama ilikuwa ndio siku ya mwisho kuuona mwili wa rafiki yangu kipenzi Martin.
                               ******************************
Ilikuwa imepita wiki moja baada ya kurudi kutoka Bunda kumzika Maritin nakumbuka siku hiyo nilikuwa nipo ofisini nikijaribu kupitia faili moja lililokuwa linamhusu jambazi mmoja ambaye mpaka siku ile ilikuwa bado sijamjua ni nani ila nilikuwa nimeshafanikiwa kupata baadhi ya nyaraka muhimu kuhusu huyo mtuhumiwa mara ofisini kwangu akaingia Gerald, tuliongea mambo mbalimbali kisha akaniambia ya kwamba lile faili la mwanamke mwenye kovu jeusi alikuwa amekabidhiwa yeye  na ameambiwa ndani ya wiki tatu ahakikishe tayari mtuhumiwa ameshajulikana na kukamatwa, nilimwambia ajitahidi na awe makini sana kwani huyo mtu anaonekana hatari sana,akasema hakuna shida kwani yeye kama iliyo ada siku zote huwa yupo makini. Alijaribu kuniomba ushauri pakuanzia kumfuatilia Yule mtuhumiwa nilimshauri aanzie kwanza kupitia lile faili alilokabiziwa ili ajue ni wapi Martin aliishia nadhani mpaka hapo atakuwa na nafasi nzuri ya kujua wapi pa kuanzia, tulizungmza nae sana mambo yetu mengine nakumbuka sana siku hiyo mpaka muda wa kutoka kazini saa 9 arasili.
                        *******************************************
Basi kama iliyo ada ya majukumu ya kikazi Gerald alianza kuifuatilia ile kesi ya Mwanamke mwenye kovu jeusi maana aliambiwa ndani ya wiki tatu awe tayari ameshajua kila kitu kuhusu huyo muuaji wa kutisha ikiwezekana pia awe tayari ameshatia ndani ya mikono ya sheria, alianza kwanza kwenda kufanya mahojiano na mwanadada mmoja  ambaye alikuta jina na mahali alipokuwa anaishi pamoja na sehemu aliyokuwa akifanyia kazi kwenye faili aliloliacha marehemu Martin huyo dada alikuwa anafanya kazi benki ya taifa ya biashara makao makuu pale alijulikana kwa jina la Zainabu Athuman akiwa mmoja wa maafisa mikopo pale makao makuu. Basi siku hiyo asubuhi na mapema Gerald alidamkia pale benki kwani alihofia kwamba akichelewa Yule dada anaweza asimkute kwani mara nyingi huwa anazunguka sehemu mbalimbali hasa kwenye maofisi kutoa elimu kuhusu mambo ya mikopo. Ofisi ilipofunguliwa tu  Gerald alikuwa mmoja wa watu wa kwanza kuingia mule ndani ya jingo la benki moja kwa moja mpaka mpaka mapokezi,”samahani naweza kuonana na Zainabu Athuman?” ilikuwa ni sauti ya Gerald akimuuliza mmoja wa wahudumu pale meza ya mapokezi,samahani  una ahadi naye? Mdada mmoja wa pale mapokezi alimuuliza, hapana sina ahadi naye ila ninashida naye. Ya kiofisi au ya binafsi? Ya kiofisi, ilibidi Gerald adanganye kidogo ili apate nafasi tu ya kuonana naye,kuepuka usumbufu ambao huwa hauna maana uliojaa katika ofisi nyingi hapa Tanzani ok sawa nenda gorofa ya kwanza mkono wa  kulia utakuta ofisi imeandikwa ofisi ya afisa mikopo ndio hapo hapo,Gerald alishukuru na kupanda ngazi kuelekea kuonana na Zainabu.

 alipofika pale mlangoni, alikuta mlango ukiwa wazi na kwa ndani alimuona Zainabu akipanga mafaili yake vizuri juu ya meza mule ofisini, Gerald akamuuliza,samahani naweza kuingia? Ndio hakuna shida wewe pita Zainabu alimjibu Gerald huku akikaa kwenye kiti chake na kuanza kukizungusha pale kwenye kiti kushoto kulia, Gerald aliingia na kukaa kwenye kiti cha wageni kisha na kumtazama Zainabu hivi kama dakika 2 mpaka Zainabu akamshitua kaka vipi nakusikiliza wewe maana nataka kuondoka hapa, alimwambia Gerald huku akimshusha chini juu chini juu,
Basi Gerald alianza kujitambulisha, kisha akatoa na kitambulisho chake halafu akamueleza nia ya yeye kuwa pale ofisini muda ule,Zainabu alionekana kuishiwa nguvu kisha akaanza kumwelezea Gerald ya kwamba mbona tayari alishakuja mwenzako na nilimueleza kila kitu lakini? Ndio hilo nalijua lakini mimi imekuja ili kupata uhakika zaidi kuhusu hili jambo,Gerald alizungumza kwa umakini huku akimkazia macho kuongeza msisitizo, hivyo basi na maswali kidogo naomba nikuulize ili nipate majibu ya kuridhisha kutoka kwako. Unamfahamu vipi huyu mwanamke anayejiita eti anakovu jeusi? Kiukweli simfahamu huyu mwanamke ila nachojua ni kwamba alikuwa na uhusiano na mdogo wangu mpendwa Rashid,hapo hapo Gerald alimkatisha, huyo Rashid yupo wapi? Alishafariki, maskini Zainabu aliendelea kuongea huku akionekana kama ni mtu aliyekumbuka mbali sana. Unaweza ukaendelea, Gerald alimwambia, ndio huyu mdada simfahamu vizuri ila naweza kusema kuwa alikuwa na uhusiano na mdogo wangu ambaye baadaye alikuja kufa kifo cha kutatanisha kule bahari beach,mimi huyu mwanamke nimewahi kumuona mara mbili na hata hapa pia nikimuona namkumbuka ilaaah ilaah ilaah alianza kusita kuendelea kuongea Zainabu, ila nini? Wewe usiogope sema yote sawa maana hapo utakuwa umelisaidia sana jeshi la polisi.unajua Napata tabu sana kwani huyu mwanamke ni wa ajabu sana kwanza aliacha ujumbe wa karatasi kwenye mfuko wa marehemu mdogo wangu Rashidi pia na hata hapa ofisini wiki mbili baada ya kifo cha mdogo wangu alikuja na kusema ya kwamba nikithubutu kumtaja jina lake basi kabla yeye hajakamtwa mimi nitakuwa sipo duniani na pia kwa yoyote nitakayemtajia jina lake akijua pia lazima atamuondoa duniani, ndio maana nakuwa na  hofu ya kumzungumzia kwani pia mdogo wangu Maimuna alikaidi huo ujumbe hapa napozungumza wiki ya pili sasa tumetoka kwenye msiba wake hivyo mimi siwezi kuzungumza zaidi ya hapo samahani sana alimalizia Zainabu huku machozi yakimtiririka ..
Gerald alibakia asijue la kufanya kwani wakati anaendelea kumbembeleza Zainabu amwambie kuhusu Yule mwanamke aliyejiita mwenye kovu jeusi alisikia mlango wa ofisi ya Zainabu ukigongwa kuashiria kuna mtu alikuwa anahitaji kuingia.
Basi pale pale Gerald alimuaga na kuondoka huku akimuahidi ya kwamba ataludi tena siku nyingine,Zainabu hakumjibu kitu zaidi ya kujifuta machozi na kujiandaa kuzungumza na Yule mgeni aliyekuwa pale mlangoni. Gerald alitoka mule kwa kasi ya ajabu huku yule mtu aliyekuwa anahitaji kuingia mule ofisini akimshangaa mpaka nje kisha akaelekea kwenye sehemu ya maegesho ya magari tayari kwa ajili ya kuchukua gari lake kuondoka basi Gerald akufungua gari lake na kuingia wakati anataka kukaa kwenye siti akahisi kama amekalia kitu kigumu kilicho chini ya kava la siti ya kiti cha gari ikabidi ainuke ili aangalie ni kitu gani hicho kwani gari ni ya kwake na ndio aliyokuja nayo pale basi ikambidi ainue lile kava la siti ya gari alikuta kuna bahasha ya kazi ikabidi ashangae ni nani aliyeiweka pale akaichukua na kuiangalia kujua inahusu nini, kuifungua akakuta kuna barua imeandikwa kwenye karatasi ngumu yenye rangi nyekundu maandishi yakiwa ya rangi nyeusi, maandishi yenyewe yalikuwa yanasema ifuatavyo
Ndugu Gerald najua ni wewe ndio uliyepewa jukumu la kunifuatilia mimi ila nakuomba utambue ya kwamba mimi ni mtu hatari na hilo utaamini ukifika nyumbani kwako ni mimi “MWANAMKE MWENYE KOVU JEUSI”
Gerald aliisoma ile karatasi zaidi ya mara 5 huku akiangalia kila upande kuona kama atamuona Yule mwanamke  hakufanikiwa alizidi kuchanganyikiwa pale huku akijiuliza huyu mwanamke amejuaje kama mimi leo asubuhi nitakuwepo hapa? Nani amemwambia wakati hakuna hata mtu mmoja aliyemwambia kuwa leo ataenda pale, pili Yule mwanamke aliweza vipi kupitisha ile bahasha mpaka pale chini ya lile kava la siti ya gari lake,wakati alifunga na ufunguo,alijikuta akishangaa mpaka akaja kushituliwa na mlinzi wa lile eneo la kuegeshea magari, “kaka samahani mbona gari umeliweka vibaya wengine wanashindwa kuegesha magari yao”.ilikuwa ni sauti ya Yule dada aliyekuwa anakusanya ushuru wa kuegesha magari,ilimbidi  Gerald aombe radhi kisha akaondoa gari lake kuelekea ofisi kwake aliendesha gari huku kichwani akiwa na mawazo, amakweli huyu mwanamke ni hatari kwa staili hii inanibidi niongeze umakini.
                                ******************************
Wakati Gerald yupo ofisini akiendela na kazi mara akipigiwa simu na jirani yake ya kwamba anahitajika mapema sana yumbani kwake kwani kunatatizo ilemetokea,kusikia hivyo Gerald alichanganyikiwa kwani alihisi Yule mwanamke mwenye kovu jeusi atakuwa ameshafika kwake na kufanya jambo lisilo jema,
Naomba unisindikize kwangu samahani sana,Gerald alimuomba Siwah amsindikize nyumbani kwake, Siwah alishangaa sana kwani kwa muda ule iliwapasa kuwa kazini, samahani bwana nisindikize kuna dharura nimepigiwa simu hivyo sina budi kuwahi nyumbani alizidi kusisitiza huku akichukua simu yake na kujaribu kumpigia mpenzi wake Furaha ambaye walikuwa wakiishi wote japo walikuwa hawajafunga ndoa, alipiga simu zaidi ya mara tatu iliita bila kupokelewa,Gerald alijihisi kuchanganyikiwa, Siwah tafadhari twende nyumbani kwangu nahisi si salama, aliomshika mkono Siwah na kumvuta nje waelekee kwenye gari tayari kwa ajili ya safari ya kuelekea kwake. Wakati wapo ndani ya gari wakielekea nyumbani kwa Gerald ndipo alipoanza kumuelzea kisa kizima alichokutana nacho siku ile asubuhi toka alipoenda kazini kwa dada Zainabu maongezi yao yote yalivyokuwa na mwisho alimueleza jinsi ile bahasha aliyoikuta china ya siti ya gari lake.Siwah alishangaa sana kusikia yale maneno “sikia ndugu yangu huyu mwanamke ni hatari sana hata Martini alikuwa analeta masihara nayeye umeona yaliyomkuta?” inabidi umakini uongezeke mara dufu katika kufuatilia hili swala kwani bosi amekupa siku ngapi? Alimalizia Siwah kwa kumuuliza Gerald huku wakiwa wamekaribia kabisa nyumbani kwake. Amenipa wiki tatu na sasa ni siku ya 4 hata sijapata pa kuanzia wewe acha tu kama ni kazi basi hii imetia fola. 
Walifika nyumbani kwa Gerald na kukuta watu wakiwa wamejaa sana ukizingatia ile nyumba walikuwa wamepanga watu kawa  wa 5 hivi, majirani pia wa nyumba za jirani pia walikuwa wamekusanyika pale uwani kwenye ile nyumba. Waliposhuka kwenye gari wale watu walimtazama kwa sura ya hudhuni sana Gerald kisha jirani yake mmoja akamuambia afadhali umekuja jirani hali ya hapa nyumbani ni mbaya sana,Gerald aliona wanachokiongea hata hakieleweki moja kwa moja akaelekea upande wa pili ambapo ndipo alipokuwa amepanga yeye, “sasa unaenda wapi bwana mbona unakuwa kama sio mwelewa hebu subili kwanza hapa tuwasikilize tujue tatizo nini” ilikuwa sauti ya Siwah huku akimshika shati Gerald asiondoke. Ilimbidi ahairishe kuondoka pale  kwa kufuata ushauri wa rafiki yake na kusimama kuwasikiliza  kujua tatizo ni nini, samahani sana jirani hapa nyumbani hali sio nzuri mida ya saa 5 hivi alikuja mdada mmoja akiwa amejifunika vitenge akiwa na gari aina ya Toyota surf, alipofika hapo getini alipiga honi sana akatoka shemeji kwenda kufungua ile kufika tu na kufungua lile geti, mbona wajiuma uma wewe nambie sema usiogope kama wamemuuwa au vipi Gerald alidakia haraka haraka akongea kwa sauti iliyojaaa wasiwasi na shauku ya kutaka kujua ni nini kimetokea, hapana siwezi kusema moja kwa moja wamemuuwa ila baada ya kufungua tu geti Yule dada alishuka akiwa ameshikilia bunduki na kumuelekezea walekee ndani kwako ndipo pale tulipokupigia simu, inamaana bado wapo ndani? Alidakiwa Siwah kumuuliza swali Yule jirani aliyekuwa akihadithia pale, hapana waliingia ndani baada kama ya dakika 5 alitoka naye na kumpakia kwenye gari huku wakiwa wamebeba baadhi ya makaratasi,shiiti  ngoja kwanza hebu twende ndani Gerald alimwambia Siwah hukua akitoa pisto yake ndogo na kutangulia, mbona una haraka sana Gerald hata hawajamaliza kutuelezea wewe umeshaanza kukimbilia ndani haya hebu endeleeni kunielezea mim,i Siwah aliwaambia wale majirani.
Gerald kuingia ndani alikuta vitu vimefumuliwa fumiliwa na kuchambuliwa sana huku kwenye kabati za chumbani kwake zikiwa zimepekuliwa na baadhi ya karatasi zikiwa zimepekuliwa na zingine zikionyesha wazi zimechukuliwa kuangalia pembeni mwa kitanda akaziona simu za mpenzi wake zikiwa kwenye kabati dogo la vipidozi  mule chumbani, akakuta kuna missed call nyingi na za kwake zikiwepo pia, basi Gerald akachukua zile simu na kuziweka kwenye mfuko wake wa suruali wakati anataka kutoka kuelekea sebuleni kuangalia juu ya mlango ule wa kuingia chumbani kwake akakutana na maandishi yaliyoandikiwa kwa marker pen nyekundu MWANAMKE MWENYE KOVU JEUSI LEO AMEKUTEMBELEA CHUMBANI KWAKO..
                                             *******************************
Gerald baada ya kuona yale maandishi yalimchanganya sana pale pale alijihisi kuchanganyikiwa ikawa mara  atoke aelekee sebuleni mara aludi chumbani mara aingie chooni, haiwezekani huu ni usanii wa hali ya juu huyu mtu amejuaje kama mimi naishi hapa, mtoto wa watu pia ameondoka naye mimi nitawajibu vipi ndugu zake hapana  huu ni usanii nafanyiwa wakati anaendelea kuzunguka mle ndani peke yake huku akiongea mara Siwah akingia mule ndani akiwa ameshika kiatu kimoja cha kike mkononi,kaka huyo mwanamke hatari amedondosha kiatu kimoja hiki hapa kinaweza kutusaidia katika upelelezo wetu,mbona hueleweki Siwah alimuuliza Gerald baada ya kumuona amekaa kwenye kochi sebuleni kwake huku akizungumza peke yakena kurusha rusha ngumi na mikono hovyo,Siwah alimsongele kwenye kochi Gerald na kuanza kuzungumza naye kwa upole sana, Gerald alimulezea kila kitu huku akimumbia aende chumbani kwake juu ya mlango akasome kilichoandikwa, wakati wanaendelea kuzungumza mara simu ya mpenzi wake ikaita mfukoni Gerald aliitoa na kuipokea tu mara akasikia sauti nzuri ya kike, samahani sana mimi naitwa Candra,Gerald alimjibu upande wa pili samani mwenye simu hayupo, ndio hilo nalijua mwenye simu nipi naye kwangu hapa mimi naye zungumza naitwa Candra au ukipenda niite wanamke wenye kovu jeusi nipo kwenye haraki za kulifuta hili kovu langu jeusi unanisikia lakini? Alizungumza Yule mwanamke ambaye kwa sauti yake ilikuwa ni ngumu sana kuamini kwamba ni yeye ndio aliyekuwa akifanya vile vituko, ndio nakusikia Gerald alijibu kwa upole ndio sasa hebu sikiliza kwanza hii sauti alimwambia huku akimsogezea sauti ambayo ilikuwa ikitoka kwenye kama redio Fulani hivi, Gerald alisika sauti yamaongezi baina yake yeye na bosi wake siki alipokuwa akikabidhiwa lile faili, kisha akasikia na sauti ya maongezi baina yake yeye na Zainabu siku ile asubuhi alipoenda ofisini kwake kwa ajili ya kumhoji, 
mwisho Gerald alichoka kabisa aliposikia sauti ya mazungumo yake  yeye na wale majirani wake pale nje na maongezi yake yeye na Siwah ambayo yalikuwa hayana hata dakika 10 mule ndani,Gerald alijikuta akichoka kabisa pale juu ya lile kochi.unanisika kwa makini sasa nakuomba ujitoe kufuatilia hili jambo nakupa siku tatu kama unataka mpenzi wako aendee kuwa hai ilimalizia ile sauti na kukata simu,Gerald akaichuka simu ili aangalie ile namba ainpigie kwa simu yake ajalibu kuzungumza na mpenzi wake ajue kaka yu hai kuangalia kwenye received call hakuiona namba,aliitafuta ile namba wapi hakuiona hata kidogo,Siwaha siwah hii kali huyu mwanke kila jambo nalofanya analijua sasa ndio nini mbona hii kazi inazidi kuwa ngumu hivi? Gerald alimhadithia kila kitu alichokisika kwenye ile simu.kaka inabidi siku yakesho asubuhi uombe kikao na bosi wetu umueleze kila kitu bwana maana haiwezekani huyu mtu atuzidi maarifa kiasi hiki hapana hapana hiyo haikubaliki hizo ni dharau sana

 
                                   ****************************
Baada ya kikao kilichokuwa takribani dakika 50 kati ya mkuu wa upelelezi mkoa wa Dar-es-salaam na ma afisa wapelelezi waandamizi kuhusu jinsi ya kumdhibiti Yule mwanamke mwenye  kovu jeusi kama yeye alivyopenda kujiita, mkuu wa upelelezi aliwaongeza watu wawili washirikiane na Gerald akatika kumtafuta Yule mwanamke mwenye kovu jeusi kati ya watu waliongezwa Siwah pia likuwa ni mmoja wapo na dada mmoja aliyejulikana kwa jina la inspekta Amina, baada tu ya kikao kuisha  wote walitawanyika kila mmoja akieleka mahali pa kuanza  kumtafuta Yule mwanamke,
Mimi niliondoka moja kwa moja mpaka makao makuu ya mamalaka ya mawasiliano huku Gerald akielekea kule benki ya taifa ya biashara kwenda kumuhoji tena dada Zainabu wakati Amina akibaki pale pale ofisini akijalibu kupitia lile faili la Yule dada. Nilipofikia pale ofisi za mamalaka ya mawasiliano nilijitambulisha na kuingia moja kwa moja mpaka kwenye ofisi ya injinia upande wa mawasiliano ya simu nilifika pale huku nikiwa na simu ya Furaha mpenzi wa Gerald aliyetekwa,ambayo aliitumia jana kumpigia Gerald, nilipofika mule ndani nilimkata kaka mmoja ambaye alionekana ni mtu asiye na utani hata kidogo wala asiyependa masihara, haya kaka nambie unashida gani? Na nani amekuruhusu kuja mpaka huku ofisini kwangu? Kwa maana shida zote za wateja na malalamiko yanasikilizwa japo chini? Jamaa aliongea kwa sauti iliyojaa kejeli na dharau sana,
Samahani sana kaka kwa kukuingilia kwenye ofisi yako huku ukiwa na kazi nyingi za kufanya, ahaa acha maneno mengi bwana eleza shida yako nijue kama inanihusu ama vipi? Yule  jamaa alinikatisha, sawa kuna nambo moja imenipigia simu jana usiku sasa nilikwa nahitaji msaada jinsi ya kumtambua huyo mtu mwenye iyo namba na anapatikana wapi,nilianza kumeleza Yule injinia. Sasa hiyo shida ndio ya kuileta hapa? Mbona watanzania mnakuwa sio waelewa kabisa? Kwani amekutukana? Na sisi hapa sheria zinasema ya kwama haturuhusiwi kutoa taarifa yoyote ile bila barua ya polisi na pia hizo taarifa inabidi waje kuzichua polisi wenyewe sio mtu binafsi sijui unanipata kaka? Jamaa alinieleza huku akiwa bize na kompyuta iliyokuwa juu ya meza yake pale ofisini.
Sikutaka kuendelea kuzungumza naye sana nilitoa kitambulisho changu na kukambidhi akitazame alikipokea akakitazama kama sekunde 25 kisha mwenye akawa mpole, samahani sana afisa, hamna shida nilinjibu, samahani sana unajua humu huwa kuna watu wengine wanakuja bila sababu za maana mtu ameona meseji kwenye simu ya mpenzi wake basi huyo anakuja hapa au anaenda kwenye kampuni za simu ajue ni nani yupo wapi  samahani sana kiongozi, Yule injinia alizidi kujitetea huku akiacha kuchezea kompyuta yake na kukaa kunisikiliza kwa makini. Ndio kaka hebu tuzungumze sasa kaka hebu nambie tatizo nini? Kaka jifunze kuheshimu wa tu sio vizuri hivyo inamaana kama mimi nisingekuwa afisa wa polisi ungeendela na majibu yako utumbo? Hata shida yangu usingeisikiliza si ndio? Hapana kaka samahani sana watu ni wasumbufu sana kaka kama nilivyokuambia niwie radhi kaka sikutaka kuendelea kujibishana nae Niliitoa ile simu ya furha na kumuonyesha kuwa siku ya jana kuna simu iliingia lakini baada ya kumaliza tu kuongea nayo haijabaki kwenye call list, aliichukua ile simu nay eye kuikagua hakuiona pia, kisha akainambia nimtajie namba ya simu ya furaha, nilimtajia aliingiza kwenye computer yake na kuangalia, pia hakuona ile simu kwenye data base zao, kaka nimeshagundua kitu kwani aliyewapigia simu amezungumza nini? Sikutaka kumueleza kila kitu ila nilimuambia tu ya kwamba huyo mtu aliyepiga simu ni mtuhumiwa na tunamtafuta, hapo hapo alidakia ah sawa nimeshamgundua…!!
Nilidakia hapo hapo, umeshamjua huyu mwanamke anayetusumbua? Bora hii zoezi liishe maana tumeshachoka sasa, nilijikuta namtamkia huku akinitazama machoni na pia akinisikiliza maneno niliyokuwa namuambia,hapana simaanishi namjua huyo mtu namanisha nishamgundua huyu mtu njia aliyotumia kupiga mpaka namba yake isionekane, nilijikuta nachoka kabisa kwa maaana nilijua zoezi linaweza kuwa limefika mwisho kumbe wapi, haya hebu nambie endelea nilijikuta nazungumza kivivu na kwa nafsi ya kukata tama, huyu mtu atakuwa amekaa sana Columbia na brazili aliendelea kuniambia, huko ndio huu kchezo upo pia atakuwa na utaaalamu sana na compyuta hapa hata tufanyaje namba yake hatuwezi kuipata kirahisi maana alichokifanya hapa ni kuingilia kwenye syteam ya wave transformation katika satellite yetu kuna code atakuwa ametumia kufanya hivyo.niliishiwa nguvu kabisa, sasa tutaipataje kuipata nilimuuliza, hapo ndipo kazi ilipo kuipata iyo namba ni kipindi tu pale itakapokuwa inazungumza ndipo hapa itasoma lakini baada ya hapo huwa inafutika hii huwa inatumiwa sana na wauza madawa ya kulevya Brazil na Columbia kwa lengo la kuwezesha shughuri zao pia huwa inatumiwa na watekaji wa watu huko chile ambapo kuna magenge ya wahuni huwateka watoto wa matajiri na kuwapigia simu wazazi wao watoe pesa lasiivyo watawauwa watotot wao hivyo huwa wanatumia hii system ili kuepuka kukamatwa,
Jamaa alizidi kuleta hadithi na maneno mengi mpaka akajikuta ametoka nje ya mada, kaka nakuelewa sasa unajua nini lengo hapa ni moja tu jinsi ya kumkamata huyu mwalifu sasa tunafanyaje? Tatizo ni kwamba naweza kutegesha hapa ikiita nijue lakini akibadili laini tu hapa inakuwa kazi nyingine sipati kitu ila nakuahidi hili jambo nitalifanyia kazi kwa nguvu zote naomba unipe siku tatu samahani sana tuwasiliane ijumaa aliniambia Yule injinia basi tuliagania huku tukibadilishana naye namba za simu.
Nilitoka kwenye zile ofisi za mamlaka ya mawasiliano na kuingia kwenye gari yangu ndogo tayari kulekea ofisini ili kujua pia wenzangu ni kipi wamekipata maana tuliahidiana ya kwamba  saa 6 wote watatu mimi Gerald na Amina tuwe ofisini tufanye kakikao kadogo kujua ni kipi cha kufanya, niliendesha gari yangu taratibu huku nikwa nazungumza na simu nakumbuka nilipofika pale magomeni kulikuwa na foleni kubwa sana kwani msafara wa rais wetu ulikuwa unapita basi nilipungumzamwendo na kuendelea kuzungumza na simu huku nikiwa nimeshusha kioo cha gari yangu kwani air condition yangu ilikuwa imeharibika mara ikaja pikipiki aina ya baja kwa nyuma kwenye ile foleni ya magari ikiendeshwa na mtu mmoja ambaye alikuwa amevalia helment ya blue kichwani akiwa amevalia utazani ni mtu aliyekuwa anaenda safari ya mbali sana kwani kwenye mikono na miguu alikuwa amevaa plastiki za kuzuia michubuko ile pikipiki ilikuja mpaka usawa wa gari yangu kisha Yule mwendesha pikipiki akanitazama kwa sura ya tabasamu hapo ndipo nilipogundua ya kwamba ni mwanamke akanisalimia kaka habari, nilimuitikia kwa kichwa kwani nilikuwa nazungumza na simu bado, mara akatupia bahasha mule ndani kwenye gari yangu halafu huyo akaondoka kwa mwendo wa kasi nilishituka nikajikuta nawepa pembeni simu yangu na kuiangalia ile bahasha huku nikimtazama na Yule mwanamke kwenye kioo cha gari yangu kwa mbele akiondoka bila hata kusimama pale kwenye mataa kiasi kwamba mpaka akasababisha ajali maeneo yale kati ya daladala nagari moja lililokuwa limebeba maji ya kunywa ya uhai ambalo lilionekana lilikuwa ni gari la kusambaza maji sehemu mbalimbali hapa mjini.
Niliitazama ile bahasha kwa wasiwasi sana kwa juu ilikuwa imeandikwa jina langu halisi, huyu mtu amelijuaje jina langu halisi? Hii ni hatari potelea mbali nikaichukua ile bahasha na kuichana kujua mule ndani kuna nini, nilkuta kuna ujumbe uliokuwa umeandikwa kwa rangi nyekundu uliokuwa ukisomeka
                         Dear Siwah Erique
 mimi naitwa Mwanamke mwenye kovu jeusi kwa leo nilikuwa nakusalimia tu na kukuambia ya kwamba karibu sana kwenye himaya yangu nitaludi tena kukusalimia vizuri baaadaye kazi njema.
Nilipousoma ule ujumbe nilishangaa sana kisha nikajikuta nacheka mwenyewe,amakweli mimi ni mjinga yani nashindwa kumkamata mtuhumiwa mbele yangu kweli kazi ipo mwaka huu sawa na aje tu mimi hata simuogopi hata kidogo. Upande wetu uliruhusiwa na trafiki nikaondoa gari yangu taratibu kuelekea stesheni ambapo ndipo ofisi zete zilipokuwa.
Niliwakuwa wenzangu wameshafikia wakinisubili mimi, tuliingia kwenye ofisi ya Amina kwa ajili ya kufanya kakikao kadogo cha watu watatu, alianza Gerald kuzungumza ya kwamba hakumkuta Zainabu kazini siku ile kwa taarifa aliyoikuta ni kwamba alikuwa mgonjwa, alipoomba namba yake ya simu alimpigia ambapo alipokea mdada mmoja aliyejitambulisha kama mdogo wake ambaye alisema ya kwamba Zainabu jana aliludi toka kazini akiwa hajisikii vizuri wakampeleka hospitali ambapo yupo hoi wodi ya wagonjwa mahututi alizidi kuleza Gerald ya kwamba allipofika pale muhimbili na kujitambulisha aliambiwa ya kwamba kuwa Yule mwanamke jana imeonekana alipigwa na kamera ya mionzi ambayo ndio imekausha damu yake na pale alipo uhakika wa kupona ni mdogo sana.
Basi baada ya kueleza hayo na mimi nilieleza ya kwangu toka pale ofisi za mamlaka ya mawasiliano mpaka kule barabarani nilipotupiwa ile bahasha na Yule mwanamke mwenye gari yangu  kisha tukaanza kujadili jinsi ya kupambana na Yule mwanamke, Amina alitueleza ya kwamba Yule mwanamke tu ndio atakuwa amempiga hiyo mionzi Zainabu, hivyo basi inabidi tuongeze umakini, tulijadiliana na kufikia mahitimishoa ya kwamaba  ni lazima kesho asubuhi tuanza kumsaka, kaka hili zoezi ni gumu ten asana tututa,tafutia wapi? Hata pa kuanzia hatupajuai kila anayegusa anga zake anaondoka duniani hapa nilipo mimi sina hata raha kwa maana sijui hata mtoto wa watu Furaha anaendeleaje.Gerald alilaamika tulikubaliana tukaanze kumsaka mitaaa ya mbezi beach ambapo ilisemekana kuwa alikuwa akiishi na mdogo wake Zainabu kabla hajafa, tulielewane tukajaribu kwa siki nzima ya kesho kwenda kufanya upelelezi upande wa kule.
 Wakati tumemaliza kujadiliana mara simu ya Gerald ikaita kuangalia alishangaa kuona namba yake simu ndio ilikuw ikimpigia, jamani nashangaa hapa simi inaita namba inayoonekana kwenye screen ni namba ya ngu what is this? Mimi hata kuipokea naiogopa alisema huku akiiweka wenye  meza pale ofisini mara Siwah akaichukua na kuipokea  haraka haraka enhe nani  mwenzangu? Ni mimi mwanamke mwenye kovu jeusi sauti iliongea upande wa pili huku ukiacha isikike sauti Siwah aliiweka simu loudspeaker ili wasikie wote, walishangaaa sana kusikia yale mazungumzo yao ambayo yalikuwa hayana hata dakika 2 yakizungumzwa kupitia ile simu yakiwa yemerekodiwa mwisho wa yale maongezi Yule dada alisema ya kwamba nilikuambia ujitoe kufuatilia hili jambo lakini inaonekana wewe sio mwelewa si ndio? Sasa nakusubili kwako ile sauti ya kike ilizungumza kisha ikakata simu. Gerald alijihisi kuogopa sana pale pale wakaanza kujadili hivi huyu mwanamke inakujae haya mazungumzo yetu tunayazungumza hapa hapa na anayapata hapa hapa? Kwa staili hii hatufanyi lolote sasa nilijikuta nazungumza kwa ukali kidogo, usikasilike hapa ni kujua haya maongezi anayapataje?
hebu tusachi kwanza humu ndani Amina alizungumza huku akianza  kuangalia kila mahali kuona kama kuna kinasa sauti chochote…!
                                 ****************************
Amina aliangalia kila mahali bila kuona kinasa sauti chochote huku mimi na Gerald tukiwa tu najaribu kujadili kuhusu hatima ya Yule mwanamke mwenye kovu jeus,i basi wakaafikiana ya kwamba kwa usalama zaidi wa Gerald ni bora siku hiyo asiende kulala kwake kwa maana siku zote mambo aliyoyazungumza Yule mwanamke yalikuwa yanatokea, waliagana nakuelekea nyumbani kwa Siwah kwa ajili ya kulala.
                              **************************
Kesho yake asubuhi na mapema baada ya kuwasili ofisini  mimi Gerald na Amina tulipewa askari kanzu watano wa ziada kwa ajili ya kuelekea maeneo ya mbezi beach kujaribu kumtafuta mwanamke mwenye kovu jeusi, tuliaacha wote gari zetu pale kwenye maegesho ya magari ya kazini na kuchukua gari zingine kabisa za kazini lakini zenye namba za kiraia ambazo huwa tunazitumia kwenye shughuri zetu mbali mbali maalumu ambazo hatukupenda kujulikana, tulichukua gari tatu moja nikiwa nayo mimi na dereva nyingine Amina na nyingine Gerald akiwa na askari kanzu mmoja, bai tulienda moja kwa moja kufika mbele tukagawana majukumu, mimi nitakuwa napita kwenye ma ofisi mbali mbali,Gerald kwenye nyumba za wageni na nahotel huku Amina tukimpa kazi ya kupeleleza ufukweni
,nilipita kwenye viwanda na ofisi mbalimbali nikijitambulisha kisha na kuomba list ya wafanyakazi na picha zao ambapo nilikuwa najaribu kuangalia baadhi ya wafanyakazi na kuwahoji kidogo na wengine kuwaahidi ya kwamba nitawatafuta wakati natoka kwenye kiwanda cha kutengeneza dawa za mswaki na mafuta ya  mwili mara nikasikia ile simu ya Furaha mchumba wa Gerald ikiita kwani mpaka kipindi hicho ilikuwa bado nonayo mimi toka juzi tulipotoka nyumbani kwa Gerald kuangalia kumbe ilikuwa ni meeji imeingia ikisomeka ya kwamba niliwaambia mjitoe kujihusisha na kunifuatilia mimi sasa subilini majibu baada ya masaa kadhaa,kuangalia kama kawaida namba ya aliyetuma haikuonekana nikajua tu atakuwa Yule dada mwanaharamu tunayemtafuta, nilitafakari nikaona nikiwajulisha wenzangu nitawaondoa kwenye morali ya kufanya kazi, nikaona si mbaya nitawajulisha baadaye tukikutana,wakati nikiendelea kutafakari mara simu yangu ya mkononi ikaaita kuangalia kumbe alikuwa ni Yule injia wa pale mamalaka ya mawasiliano, “Ndio injinia nakusikiliza, sasa kakaleo asubuhi niliitegesha hiyo namba hivyo nimefanikiwa kuipata namba ya simu ya huyo mtu anayewasumbua na pia inaonyesha muda huu anapatikana mitaa ya bahari beach inspekta, alimalizia kuniambia yule injinia wa mamlaka ya mawasiliano. Sawa kaka basi naomba unitumi hiyo namba yake  ili tuanze kumtafuta kwa maana tupo mitaa ya karibia na hapo unaposema alipo sasahivi, nilimjulisha Yule injiniaalinielewa na baada ya kama dakika 2 alinitumia data zote ile namba ya simu jina lililotumika kuisajili ile laini na umbali ambapo ilionekana Yule mwanamke yupo kutokea kwenye mnara wa simu, nilimjibu kwa kumshukuru kisha nikawapigia simu Gerald na Amina kuwaambia ya kwamba tukutane karibia na hayo maeneo si chini ya nusu saa kwa ajili ya kuhakikisha tunamtia nguvuni Yule mwanamke, basi tulijongea pale lile eneo ambalo lilikuwa kando kabisa mwa bahari ya hindi, mimi nikiwa wa kwanza kufika, tulipofika lile eneo niliwambia vijana wangu niliokuwa nimeongozana nao kuwa makini kwani tupo kwenye eneo hatari sana,tulikaa pembeni kidogo kwenye mwamba Fulani uliokuwa pale ukingoni mwa bahari tukiwa tukiwasubiri kina Gerald pamoja na Amina, mara nao walifika lile eneo bila kukawia kila mmoja akitokea upande wake,alipofika lile eneo Amina aliliangalia kisha akaniambia kwa sauti ya majonzi, “maeneo hay ndipo tulipoikuta maiti ya marehemu Yule mdogo wake na Yule dada anayefanya kazi benki” kisha akaendelea nahisi huyu mtu atakuwa yupo haya haya maeneo,mwili ulinisisimka sana kusikia vile kwani kumbe nilikuwa kwenye eneo hatari ambapo muda wowote umauti unaweza kutukuta, haya hakuna muda wa kupoteza hapa cha msingi tuanze kumsaka haya maeneo kwa maana nimeambiwa ya kwamba yupo maeneo haya haya, nilianza kuwaambia ili tuanze kuwajibika huku kila mmoja wetu nikimwambia achukue tahadhari, tulipnaga mikakati pale na kungalia asili ya lile eneo kiukweli kulikuwa na watu kwa mbali ndani ya bahari wakiendele na shughuli zao za uvuvi hasa mida ile nazani walikuwa wakikagua tu zana zao za uvuvi kwa ajili ya maandalizi ya uvuvi siku ile usiku, lile eneo lilikuwa tulivu sana kwani kwa muda wa takribani kumi tulizokaa pale tukipanga mipango yetu mbalimbali hapakuonekana mtu wa aina yoyote kupita lile eneo, kweli haya yatakuwa ni maficho yake lakini katika mazingira haya mbona kuna wavuvi tu? Sioni nyumba wala mwatairi ya magari, wala sasa anaishi vipi? Gerald alijikuta akutuambia pale, au inawezekana huyo injinia wa mamlaka ya mawasiliano nchini amenunuliwa au ni huyo mwanamke pia amefanya utundu wake kwenye simu ili kutupoteza jama maana hili eneo huyo mtu ataishi wapi? Aliendelea kusisitiza Gerald, ndio inawezekana huyu mwanamke itakuwa alianza kushituka au alihisi kuwa tumekaribia kumpata ndio akafanya hivi, haiwezekani hili eneo halina mtu bwana Amina pia alendelea kusisitiza.
Ilinibidi niwashushe munkari kidogo ili tuweze kuelewana, sawa jamani yote yanawezekana hapa cha msingi ni tufanye yafuatayo tutawanyike kutokea hapa kuelekea sehemu mbali mbali kama yupo maeneo haya tutampata sawa na kama hayupo basi tuendelee na zoezi letu
Tulitawanyika pande zote huku tukiambina kwa yoyote atakayohisi au kumuona basi atujulishe mapema sana iwezekanavyo, tuliendelea na lile zoezi la kumtafuta mara kwa umbali kama wa mita 70 nilimuona mwanamke akiwa chini amelala kwenye mchanga ule wa kando kando ya bahari huku akiwa kama ni mtu asiyekuwa na nguvu akiomba msaada alionekana kama ni mtu ambaye kuna jambo baya lilikuwa limemkuta ,basi pale pale nilimuamrisha mmoja wa wale askari kanzu niliokuwa nimefuatana nao awajulishea kina Gerald na Amina wote wafanye kuja upande ule tuliokuwepo huku sisi tukizidi kumsogelea lakini kwa tahadhari kubwa sana kwani tulijua fika atakuwa ni mwanamke mwenye kovu jeusi ameamua kutumia ile mbinu baada ya kuona tayari tumeshagundua makazi yake, nilimuambia Yule askari kanzu atoe maelekezo waje upande  ule ila wafanye kama vile kuzunguka kwani wote tukielekea upande mmoja anaweza kutuzidi ujanja kwani wote tulikuwa hatujui alikuwa na silaha gani pale..!!
Tuliendelea kumsogelea Yule dada kwa tahadhari kubwa sana huku kila mmoja wetu akiwa ameweka silaha yake tayari kwa lolote litakalotokea,tulizidi kumsogelea Yule dada moaka zikabakia kama mita kumi hivi huku tukiwa tumemzunguka, pande zote dada Yule alionekana wazi akiwa hana nguvu hata kidogo kwani likuwa akijaribu kujivuta lakini alishindwa, Gerald ambaye alikuwa upande wa kulia tukiwa tunaangaliana mara nikasikia Gerald akitamka kwa nguvu, my god mpenzi wangu Furaha jamani muacheni mpenzi wangu alizidi kusema kwa sauti ya juu Gerald, basi tuliacha kumuelekezea silaha Yule dada wote kisha tukamskimbilia kwa kasi Yule dada.
Tulipofika tulimkuta hali yake ikiwa si nzuri kwani alikuwa anaonekana ni mtu aliyechoka sana huku akiwa kama vile amekimbia mateso Fulani,ohh mpenzi wangu jamani kumbe alikueleta huku alizungumza Gerald huku machozi yakiwa yakimtiririka,bila kupoteza muda nilinyayua simua yangu ya mkononi na kuwapigia simu hospital ya taifa ya mwanayamala ili waje na gari la kubebea wagonjwa waje kumchukua kwani hali yake ilikuwa ni mbaya sana,Gerald alikuwa akijaribu kumsemesha lakina Furaha hakuwa hata na nguvu ya kuzungumza alikuwa akijaribu kuonyesha kwa ishara na macho pande wa kaskazini ambapo sisi wote tulipojaribu kupaangalia hatukuona kitu.tuliamua kufanya maamuzi ya haraka haraka kwa kuwa tuliona pale muda unaenda na kwa foleni ya jijini ingewezekana akatufia mikononi wakati tukiwa na usafiri hivyo tuliamua kusogea na gari tuliyokuwa naye ili tukutane nao barabarani
                                     *********************************
Tulimfikisha hospitali ya mwananyamala huku hali yake ikiwa bado si nzuri wauguzi na madakatari walimpeleka wodini na kumutundika na dripu za kumuongezea nguvu kwani ilionekana fika alikuwa hajapata cjakula kwa zile siku mbili alizokuwa kwa Yule mateka,sisi tulitoka nje na kukaa kusubili ripoti ya madaktari watuambie alikuwa anaendeleaje tulikaa pale kwa muda wa takiribani saa 2 ndipo muuguzi akatoka nje na kutuambia kwa muda ule tungeweza kuingia ndani na kwenda kumsalimia tuliingia kwa ukweli tulimkuta akiendelea vizuri sana japo aliweza kuzunguma maneno mawili ma tatu japo kwa shida shida sana tuliwashukuru ma daktari na kuwataka sisi tuende huku tukiahidi kuludi kesho yake kwa ajili ya kumchukua mahojiano kuhusiana na mwanamke mwenye kovu jeusi..!! mimi na Amina pamoja na wale askari kanzu wengine tuliondoka huku tukimuacha Gerald akiwasubili ndugu zake na Furaha waje wamuone kisha na yeye aende kujipumzisha.
                                        *****************************
Niliamka asubuhi na mapema kama kawaida yangu baada ya kufanya mazoezi ya viungo asubuhi kwa kufuatiliza kipindi cha mazoezi cha kituo cha hbari cha terevisheni cha ITV nilienda kujoga na kujiandaa kwa ajili ya kuelekea kazini, nilifika ofisini asubuhi na mapema baada ya kusaini kitabu cha mahudhurio nilielekea moja kwa moja ofisini kwangu nilishika faili la ile kesi ya huyu mwanamke aliyejiita mwenye kovu jeusi na kuanza kulipitia hatu kwa hatua huku nikijaribu kunote baadhi ya vitu amabvyo nilihisi ya kwamba vitakuwa vya muhimu kwa siku hiyo kabla sijaelekea hospitali kwenda kumuona Furaha.niliendelea kufanya ule uchambuzi kwa kama dakika 20 hivi ndipo alipoingia Amina ofisini kwangu kunijulia hali na kuniambia ya kwamba kama nipo tayari basi tutoke wote tuelekee hosptali ya mwananyamala kwenda kumjulia hali mgonjwa ikiwezekana na tufanye nae mahojiano kidogo kisha sisi tuendelee na majukumu mengine,nilimuelewa Amina tulitoka wote ambapo tulielekea mwanayamala hospital tukiwa na usafiri wangu binafsi ambapo tulipitia kwenye mgahawa mmoja mitaa ya kinondoni kwa ajili ya kupata kifungua kimywa kwanza kisha ndio tuendelee na safari yetu. Wakati tupo pale tunakunywa chai kwa pembeni yetu alikuwepo dada mmoja ambaye alikuwa kama mtu aliyekuwa hajiamini kabisa huku akiwa yupo makini akifuatilia maongezi yetu, ila sisi ahtukumjali mpaka pale tulipokuja kutoka nje kuendelea na safari ndipo ujumbe wa meseji ulipoingia kwenye simu yangu ya mkononi kwanza sikutaka kuusoma kwani ni vibaya kuendesha gari huku ukiwa unasoma meseji au unazungumza na simu. Tulifika hospitali ambapo tulimkuta Gerald akiwa tayari ameshafikaakiwa nje ya wodi  huku akiwa na na dada yake na Furaha sura ya Gerald ilionekana ikiwa ni yenye tabasamu bashasha, karibuni sana jamani alizungumza dada yake na Furaha kwa rafudhi ya kihehe ambaye baadaye nilikuja kugundua ya kwamba alikuwa akiitwa Witness,tuliingia wodini ambapo tilikuta daktari na nesi wakijaribu kuangalia maendeleo ya afya yake “samahani daktari tunaweza kumchukuwa mahojiano kidogo?nilimuuliza daktari baada ya kuona tayari wameshamaliza kumungalia maendeleo ya afya yake, ndio ila mpaka kwa sasa hali bado haijamludi sawa hivyo basi inabidi mumulize taratibu hasa itakuwa vizuri kama huyu mpenzi( wake huku akimshika shati Gerald na kumvuta mbele yetu) yeye ndio kama akifanya hiyo kazi alizungumza Daktari, basi Gerald alikaa kwenye kitanda na kumvuta mpenzi wake Furaha na kumlalia kwenye mapaja kisha akaanza kumuuliza maswali madogo madogo huku akimnywesha uji ili azidi kupata nguvu. Furaha alijaribu kutuelezea japo kwa shida sana kwamba Yule dada hakuwahi kumuona kabla ila kwa sasa akimuona atamkumbuka alijaribu kutueleza ya kwamba anamakao yake kwenye yumba moja iliyopo kando mwa bahari mitaa ya mbezi beach.wakati mazungumzo yanaendelea ghafra aliingia nesi akiwa amevalia sare ya nguo za kinesi na kutuomba tumpishe kidogo kuna dawa anataka kumpa mgonjwa Yule nesi alionekana akiwa na wasiwasi Fulani hivi, basi bila ya hiyana tulimpisha wote tukatoka nje alichomoa sindano na kumchoma Furaha kisha akaondoka zake baada ya kama dakika 5 hivi na sisi ndipo tulipoludi wodini ile kufika tu, tukakuta hali ya Furaha imebadilika tena asaivi imekuwa mbaya zaida hata ya jana tulivyomleta pale hospitali  palepale Witness akatoka nje haraka na kwenda kumuita nesi kwenye chumba chao nesi alikuja na kustaajabu, vipi tena hapa imekuaje? Alianza kusema jamani jamani mpenzi wangu mmemfanyaje yani mmemchoma sindano baada ya dakika tano tu amekuwa zezeta? Alizungumza Gerald kwa machungu machozi yakimtiririka hapana sio sisi alianza kuruka nesi mbona sisi tulishapita mida na dakitari yalianza pale mabishano kati ya Witness, Gerald na Yule nesi,mimi niliona ya kwamba tukiendeleza yale mabishano wakati hali ya mgonjwa inazidi kuwa mbaya sio vizuri basi pale pale nikatoa simu ili niwapigie muhimbili wajiandae kumpokea mgonjwa mahututi ikiwa kama order kutoka kituo cha polisi, wakati naitoa ile simu ndipo nikakumbua ya kwamba kuna msejeji iliingia kipindi tumetoka kunywa chai pale kinondoni halafu sikuisoma kipindi tunakunywa chai kwanza nlitaka kuiacha lakini nikaona sio mbaya ngoja niisome mungu wangu sikuamini ule ujumbe niliousoma kwenye ile simu yangu….!!!
Ujumbe ulikuwa umekuja kwa namba isiyofahamika ukisema ya kwamba “najua mnaenda kumchukua mahojiano Furaha ila haitawezekana mwanamke mwenye kovu jeusi” mwili ulinisisimuka kwani nilijua ya kwamba basi atakuwa ni yeye aliyejifanya nesi pale hospitali na kumchoma sindano ile Furaha ili kupoteza ushahidi,mungu wangu tatizo la kutokumjua sura huyu mtu ndio kunasababisha haya yote haiwezekani mtuhumiwa anatukimbia hapa hapa, nilijikuta nasema kwa sauti ya chini chini huku nikisubili kuzungumza na simu upande wa pili,baada ya kumaliza kuwataarifu hospitali ya muhimbili furaha aliingizwa kwenye gari ya wagonjwa tayari kwa ajili ya kupelekwa muhimbili,  huku mimi Amina na Geral tukitoka nje kwa ajili ya kushauriana kipi hasa cha kufanya ambapo Gerald alikuwa kama amechanganyikiwa vile kutokana na lile tukio,ilibidi niwaeleze kila kitu kuhusu ule ujumbe nilioupata kutoka kwenye namba isiyojulikana, hivyo basi niliwaomba tusilaumiane bali tuwe makini na tumuombe tu mwenyezi mungu Furaha afifariki kwani yeye ndio atakayeweza kutusaidia ile kazi ya kumkamata Yule mtuhumiwa hatari anayefanya mauaji ya hovyo kila siku pale jijini.
Tulimaliza kupanga baadhi ya mikakati kisha na sisi tukajipakia kwenye gari kwenda hospitali ya taifa ya muhimbili kwenda kuona ni kipi kilikuwa kinaendelea kule. Ki ukweli tulikuta hali ya mgonjwa ikizidi kuwa mbaya tena mbaya sana kwani japo kuwa alikuwa amelazwa kwenye wodi ya wagonjwa mahututi lakini pia walituamba hata mapigo yake ya moyo yalikuwa yakiende taratibu sana kwa mwendo wa kusua sua sana hivyo tumuombe sana mwenyezi mungu kauli ile ilizidi kumchangaya Gerald na sisi pia kwani pale ndio ilikuwa mahali ambapo tuliona panafaa kupata habari zote tulizokuwa tunazihitaji basi tuliona hakuna jinsi zaidi ya kumuomba mwenyezi mungu tu amsaidie lakini wakati bado tunaendelea kushauriana mara akatoka Witness ambaye alikuwa ni dada wa Furaha alitoka nje akija pale tulipokuwa tumekaa huku akilia sana pale pale indicator ikanigonga kichwani ya kwamba Furaha atakuwa tayari ameshatutoka, basi Gerald baada ya kusikia hivyo alianza kulia sana pale pale ilibidi tufanye zoezi la kumuondoa Gerald na Witness pale hospitali.
                              *************************************
Baada ya kumaliza msiba wa mpenzi wake na Gerald nakumbuka vizuri sana Gerald alipewa likizo ya mwezi ofisi hivyo basi zoezi la kuendelea kumsaka Yule mwanaharamu aliyejiita mwanamke mwenye mkono wa bandia lilibakia mikononi mwangu na Amina huku mkuu wetu kazini akizidi kulalamika kabisa kwa nini tunashindwa kumtia kizuizini wakati kuna wahalifu wengi zaidi yak wake ambao tuliweza kuwazibidi tena kirahisi tu sana, nilimhakikishia mkuu wetu wa kazi atupe muda zaidi kwani Yule dada alionekana ni mjanja sana hivyo tusipokuwa makini anaweza kutumaliza wote hadi yeye, mkuu japo alikuwa ni muelewa ila alikuwa ni mtu mwenye papara sana alitaka kila jambo limalizike kwa muda aliotaka bila hata kuangalia uzito wa jambo lenyewe na aina ya watu au mtu tuliyekuwa tukikabiliana naye. Basi tulimaliza maongezi na mkuu wetu huku tukitoka ofisini mimi nilimwambia Amina ya kwamba naelekea nyumbani kwa Gerald maana aliniomba siku ile nimsindike makaburini kwenda kuangalia kaburi la mpenzi wake, basi tulikubaliana vizuri yeye Amina huku nikiwa nimemuagiza aelekee kule maeneo ya mbezi beach karibia na tulipomkuta marehemu Furaha akajaribu kama kufanya uchunguzi kwa njia yoyote ile kwani angeweza kuambulia lolote, kwa sababu ni mtu wa pili sasa anakutwa mitaa ya kule kwani hata mdogo wake na Zainabu Yule mdada aliyekuwa akifanya kazi benki ya biashara mwili mwa maehemu mdogo wake ulikutwa maeneo yaleyale,basi tulikubaliana akaniahidi nisijali ataenda na atahakikisha anakuwa makini sana, alichukua baadhi ya camera za cctv akaziweka kwenye begi lake baadhi ya vinasa sauti pamoja na nyaraka zingine ndogondogo kwa ajili ya kwenda nazo kulepamoja na bastola moja ili ikiwezekana zile kamera akazifunge mahali ziwe zinachukuwa matukio yote ya mahali pale, pia alichukua kile kiatu ambacho tulikihisi ni cha Yule mwanaharamu ambacho tulikikuta kule nyumbani kwa Gerald siku ile ambapo alikidondosha pindi alipoenda kumteka marehemu Furaha. Baada ya hapo tuliondoka wote kwa pamoja nikimpa lifti na kwenda kumucha mwenge kisha mimi nikaelekea zangu nyumbani kwa bwana Gerald kwenda kumchukua ili tuelekee makaburi ya kinondoni kwenda kutembelea  kaburi la mpenzi wake furaha ambaye kutokana na maelezo ya madaktari tuliamni ya kwamba atakuwa amekufa kwa kuchomwa sindano ya sumu ili kuficha ushaidi na Yule mwanamke aliyejiita eti anakovu jeusi. Bai nilifika nyumbani kwa rafiki yangu Gerald nikamkuta akiwa tayari ameshajiandaa akiwa amevalia t-shirt nyeupe yenye picha ya marehemu Furaha mbele ya kifua,suruali nyeupe huku pia akiwa amejifunga kitambaa cha rangi yeupe mkononi sikujua alikuwa akimaanisha nini.
Tuliondoka taratibu kutokanna nafoleni ya jijini mpaka mida ya yaa 5 asubuhi tukawa tumeshafika tayari makaburini, basi tulipofika kwanza tulitafuta mahali tukapaki gari kisha tukaelekea kwenye kaburi lile ambapo baada ya kufika Geral alisali juu ya lile kaburi kisha akawa kama vile anafanya usafi na kupanga mashada juu ya lile kaburi, wakati anaendelea nilisikia sauti ya mlinzi wa pale makaburini akiniita kwa mbali huku akionyesha ishara ya kwamba gari langu nilikuwa nimelipaki vibaya kuna mtu ambaye tulikuta gari yake imepaki pale aina ya escudo rangi ya kijani alidai alikuwa anataka kulitoa gari lake basi sikuwa na jinsi zaidi ya kumwambia Gerald anisubili naludi baada ya kama dakika 5  nilifika na kulitoa gari kisha nikampisha Yule mtu ambaye alikuwa anatoka mule na gari lake wakati naludi kwa mbali nilimuona Gerald akiwa amepiga magoti akisali huku akiwa amepiga magoti na mwanamke mkmoja jirani yake nahisi alikuwa hajamuona kwanza sasa nilianza kujiuliza Yule atakuwa ni nani? Maana tulienda watu wawili tu na Gerald hakunambia kama alikuwa amemuambia mtu yoyote wakutane pale,baada ya Gerald kufngua macho alishituka sana kisha nikawasikia kwa mbali kama wakiwa wanazozana na Yule mwanamke basi na mimi nikaongeza mwendo kuwahi lile eneo kwa maana niliona kama vile mazozano yamezidi na sio vizuri kwa mtu kama yeye kwani ule ulikuwa muda mzuri sana kwake kutuliza akili  Yule mwanamke aliponiona nakuja kwa kasi kwanza alishituka kisha akachoma kama kifaa Fulani chenye insha nyembamba kwa mbele akamlushia nacho Geral mkononi kisha huyo akakimbia zake kwa kuluka ukuta upande wapili nilifika na kumkuta Gerald akiwa tayari amesha kichomoa kile kifaa lakini mkono wake ukiwa kama unavimba vile nilimuuliza Yule ni nani na kwa nini imekuwa vile?
Alinijibu ya kwamba Yule mwanamke ni Yule mwanaharamu ambaye ndio tulikuwa tukimtafuta na pale anadai alikuwa ananisubili kwa hamu sana na siku yangu ilikuwa imefika huku akisisitizaya kwamba kama tukitaka kuwa salama basi tuachane na ule mpango wetu wa kumfuatilia..!! nafsi ilishangaa sana palepale nilijikuta nakosa mpaka raha inamaana nani kamuambia sisi muda ule tungekuwa pale?na amejiamini vipi mpaka kutufuata mpaka pale? Je kwanini alimfuata Gerald pindi mimi nilipoenda kuondoa gari kwenye parking ili aipite? Nilianza kuhisi sasa ya kwamba Yule mwanamke hakuwa peke yake walikuwa wengi waliokuwa wanafanya ule michezo huku wakishirikiana pia nilijiuliza Na kile alichomchoma nacho Gerald mkononi ni nini? Kwa maana mkono ulikuwa kivimba tu..!! japo alikuwa ameshakichomoa je angekuwa bado ingekuwa aje…?

 
                             *******************************************
Nilimuambia Gerald tuondoke haraka kwani mahali pale palikuwa sio salama tena hatukujua Yule mdada alikuwa amejipangaje kama aliweza kuja hadi pale makaburini na kuweza kutufanyia ule ushenzi basi tusingeweza kujua alikuwa amejiandaje basi tulielekea kwenye gari nakuondoka zetu huku tukipitia hospitali ya regency kwenda kunda kuangalia ule mkono Gerald alikuwa amechomwa na nini? Basi tulipofika hospitali daktari alitueleza ya kwamba kile kitu kilichomchoma Gerald kilikuwa na sumu kali sana kwanza Yule daktari wa kihindi alianza kutuangalia kwa wasiwasi sana huku akishindwa hata kutuelezea akidai ya kwamba kwa kuwa tayari wameshampa dawa basi inatosha, baada ya kumsisitizia ndipo akajaribu kutafafanulia kuhusu ile sumu ya kwamba ile ni sumu hatari sana na inapatikana nchi ya vietnamu ambayo unapichomwa nayo usipokichomoa hicho kitu ulichochomwa nacho ndani ya dakika kama kumi basi uwezekano wa kuendelea kuishi unakuwa haupo kabisa,Yule daktari alisema yeye sio mzoefu sana ila anachokijua ni kwamba ile sumu huwa wanaitumia huko nchini Vietnam kwenye mapigano yao ya jadi ambapo watu huwa wanaiweka kwenye silaha zao za jadi. Tulijikuta mimi na Gerald tukistaajabu sana na kisha kuangaliana bila ya kujua ni vipi imekua vile na ile sumu imeingiaje nchini.
Basi tulimshukuru sana daktari kwa matibabu yake kisha tukaondoka zetu ambapo tulipitia fast food kupata chakula cha mchana kisha nikamludisha Gerald mpaka nyumbani kwake na mimi nikaelekea nyumbani kwangu sikutaka hata kuludi kazini tena kwani nilihisi ya kwamba muda ulikuwa umeisha na isitoshe ni bora niwahi nyumbani nikapumzike nifanye usafi kwani ni mara chache sana huwa Napata muda wa kufanya usafi ukizingatia nilikuwa naishi mwenyewe.
                                     *************************************
Nilifika nyumbani kwangu nakumbuka ilikuwa kama mida ya saa kumi na moja jioni, baada ya kufika nikaona nitoe nguo nifanye usafi, ila wakati hata sijatoa nguo nje mara ukaingia ujumbe wa simu kutoka kwa Amina ukunitaka tukutane mwenge yeye akiwa anatokea mbezi beach,kuna jambo la muhimu sana nilinyanyua simu na kumpigia Amina lakini simu ilikatwa nilijaribu tena vile vile ikakatwa mara ikaingia meseji tena samahani jpo mazingira mabaya boss wewe fanya hivyo, basi sikuwa na jinsi zaidi kuvaa nguo za jioni kisha kupanda gari yangu na kwenda mwenge kuwahi kuonana na Amina, nilitumia kama muda wa saa moja na nusu mpaka kufika lile eneo nilipaki gari yangu pale mbele kidogo mwa benki ya efatha kisha nikachukua simu yangu na kumpigia Amina ambaye baada ya kupokea aliniambia ya kwamba mbona yeye hakuniambia lolote na wala hajatuma meseji yoyote isitoshe yeye alikuwa bado yupo kule mbezi beach akiendelea na uchunguzi, nilikata ile simu kisha nikashangaa hii imekaaje? Inamaana kuna mtu alitumia simu ya Amina kuwasiliana na mimi au meseji zilijituma zenyewe nilifungua simu yangu upande wa meseji kisha na kuangalia kama zile meseji  kweli zilikuwa zimetumwa na Amina au nilikosea nilikuta ni kweli zilikuwa zinaonyesha zimetoka kwa Amina, basi sikuwa na jinsi akili ilinicheza haraka haraka nikajua tu atakuwa Yule mwanaharamu anatuchezea akili tu hakuna jingine pale pale niligeuza gari kwa kasi ya ajabu na kuanza safari ya kuludi nyumbani kwangu.
Nilipofika nyumbani kwangu hali niliyoikuta haikuwa ya kawaida nilikuta tofauti sana, nilikuta vitu vimechambuliwa hovyo hovyo huku ikionyesha dhahiri mule ndani palikuwa pamepekuliwa sana nilipoingia ndani chumbani kwangu pia baadhi ya nyaraka zangu sikuzikuta hazikuepo, lakini kilichonishangaza ni jinsi milango yangu nilivyoikuta kwani niliikuta kama nilivyokuwa nimeiacha,akili ilinicheza nikajua tu Yule mwanaharamu atakuwa amepita kwangu,mungu wangu yani inamaana mpaka sasa sisi watu wa usalama tunaanza kuishi kwa woga kisa mhalifu? Hii si sawa haina maana ya kuwa wanausalama sasa haiwezekani huyu dada maisha yangu na mimi ayaweke hatarini? Na kwa nini hasemi anachokitaka? Na pia huyu mtu anajiamini nini? Na anaweza vipi kutuchezea akili kiasi hiki? Na kwanini kila mtu anayejua anajua siri kuhusu yeye au kumfuatilia lazima amuondoe duniani? Hii haiwezekani hata kidogo, kwanza kajuaje kama naishi hapa? Nahisi kuna mtu atakuwa anampa baadhi ya data pale ofisini kama ikiendelea hivi itabidi mimi nijitoe tu katika kufuatilia hii kesi kwa maana sijawahi kukutana na kesi ngumu kama hii.
Huyu mtu hana huruma hata kidogo kamuuwa kikatili mchumba wa Gerald mchana wa leo tena kataka kumuuwa Gerald? Sasa kama uwezo wake ni huu sizani kama atashindwa kumfuata Gerald hata nyumbani kwake kumtoa na kumtoa  uhai, nilijikuta natafakari mwenyewe huku nimekaa juu ya kitanda changu huku nikitazama jinsi chumba changu kilivyokuwa kimenyambulika,kwa kusachiwa, nilijikuta machozi yakianza kunitiririka taratibu pale juu ya kitanda kila nilipojaribu kuoanisha matukio kuhusu Yule mwanaharamu, haiwezekani yani afisa upelelezi kabisa wa jeshi la polisi naishi kwa wasiwasi hivi hii haina maana kabisa nilijikuta najisemea kila muda maneno yale mpaka usingizi ukanipitia pale pale juu ya kitanda.
Nilikuja kushituka mida ya saa 8 usiku baada ya kuhisi kama kulikuwa na watu wakipita pita nje ya kile chumba changu,nilijiweka sawa juu ya kitanda kisha nikashika bastola yangu kwa ajili ya jambo lolote kama lingeweza kutokea, niliinuka na kuanza kuangalia kila upande kama kuna usalama au vipi, nilizunguka mpaka sebuleni kisha nikachungulia na dirishani nikajihakikishia palikuwa salama ndipo nilipogundua tu ya kwamba kilichokuwa kinanitesa ni woga.hivi huyu mwanamke inakuwa anatuzidi maarifa?atakuwa mwanamke mmoja kweli? Au watakuwa ni kundi la watu maana siamini kama mwanmake mmoja anaweza kuwa na ujasiri wa hivi..!hii itakuwa ni ngumu sana sasa hapa najitoa mhanga ngoja nilivagae hiliswala kwa muda wa wiki 2 likinishinda namwambia mkuu kwamba basi nimenyoosha mikono. Maana kwa sasa anamuwinda tena Gerald sasa sijui anahisi marehemu Furaha kuna vitu alimwambia Gerald? Yani hii ni mbaya na aibu kwa jeshi letu yani watoto wa mjini wapelelezi wazima tunazidiwa mbinu kweli hii ni mbaya sana.
                                  *************************************
Asubuhi kama kawaida yangu niliamka na kufanya mazoezi ya viungo vya mwili kisha nikajiandaa kwa ajili ya kuelekea ofisini kwenda kulipoti kisha kundelea na majukumu mengine.nilipofika ofisini nakumbuka vizuri sana siku ile nilimkuta Amina akiwa tayari ameshafika tuliingia ofisini kwangu kisha akaanza kunihadithia kuhusu jana yake alivyokuwa kule mbezi alipoenda kumfuatilia huyu mwanaharamu,kaka yangu zile kamera nilizifunga kisha mimi nikaenda kukaa mahala kwa mbali kidogo ambapo kulikuwa na mama lishe huku nikiwa nalaptop yangu nikifuatilia kila kitu kilichokuwa kikiendelea pale, alisimama kuzungumza Amina huku akivuta pumzi kwa juu.huku mimi nikimtazama usoni kwa umakini na macho yangu yaliyokuwa yamekata tama.ndio nakusikiliza nilimwambia,huku nikimuona akitoa laptop yake na kuanza kunionyesha baadhi ya matukio, nilimuona mwanamke aliyekuwa amevalia suruali ya blue poolneck la rangi ya kaki miwani mieusi akitokea mhali pasipojulikana maana palikuwa kama kuna mfuniko Fulani hivi mahali pale nahisi alikuwa kama ametoka kwenye pango Fulani hivi kisha akaenda moja kwa moja mpaka kwenye zile kamera na kuzichukua zote,shiit huyu mwanamke alijuaje kama umefunga kamera hayo maeneo? Inamaana huyu mwanamke anaakili kuliko sisi nilimwambia aludishe ludishe nyuma pale alipokuwa akitoka na kuigandisha sura yake ambapo tuliipiga picha afadhali huyu mwanamke hapa ndipo yatakuwa makazi yake. Mitaa hii nilianza kumwambia Amina ila kinachonishangaza ni jinsi kila jambo tunalopanga anakuwa analijua hapo ndipo panapo nitatiza na kisha nikamuhadithia jinsi jana mimi na Gerald yaliyotukuta kule makaburini na jioni alivyonichezea akili kisha akaingia nyumbani kwangu na kufanya ukaguzi na kuondoka na baadhi ya nyaraka basi tulimaliza mazungumzo pale na Amina kwa kuahidiana ya kwamba inabidi tujipange tukafanye uvamizi tukiwa na askari kwa kutosha lie eneo, tuliagana na Amina huku akiwa anatoka nje ya ofisi yangu huku akiniachia laptop yake ili niendelee kumuangalia kwa umakini Yule mwanamke katika zile crip mara nikasikia simu ya mezani pale ofisini kwangu ikiita nikanyayua waya kupokea ile simu upande wa pili kulikuwa na sauti ya kike ambapo ilianza kuzungumza bila kupumzika kwa maneno makali.
                                                        ********************************
Nilitulia tulii nikimsikiliza Yule mwanamke ambaye alikuwa akitoa vitisho sana hasa kuhusu kumfuatilia kwangu akijitambulisha kwamba yeye ndio mwanamke mwenye kovu jeusi, na ya kwamba kila kitu alikuwa anakijua, tunachokifanya kwani mtandao wake ulikuwa ni mkubwa sana, alizungumza kwa vitisho sana, nilitulia kimya nikimsikiliza kwa makini mpaka alipomaliza kuongea, ndipo nilipomuuliza sawa dada umemaliza? Hakunijibu zaidi ya kukata simu tu, nilijaribu kuangalia tena namba ya simu aliyonipigia kwenye simu yangu lakini sikuikuta hata nikajua itakuwa kama kawaida yake huyu mwanamke atakuwa ametumia private namba ili tusiweze kumtambua kwani namba yake ilikuwa hata haisomi kwenye mitandao ya simu, basi niliendele kuiangalia ile picha yake pale kwenye laptop huku nikiigandisha ili kuiangalia kwa umakini zaidi, nilipojilizia na ile picha nilimpigia simu Amina aje ofisini kwangu huku akiwa na nyaraka mbalimbali zote zilizohusu Yule mwanamke baada ya dakika 5 Amina aliingia huku akiwa amebeba nyaraka zote wakati anaingia mule ofisini kwangu mara Amina alijikwaa yale mafaili na vitu vingine vyote alivyokuwa amebeba vikadondoka chini,mungu wangu nusura ajipigize kidevu kwenye meza iliyokuwa pale ofisini kwangu bahati nzuri aliwahi kuweka mkono pale mezani, nilimpa pole huku nikisimama na kwenda kumsaidia kuokota yale mafaili na vitu vingine ambavyo alikuwa amevibeba na kuja navyo mule ofisini kwangu wakati nakusanya vitu pale chini nikakiona kiatu cha kike kile ambacho tulikichukua nyumbani kwa Gerald siku marehemu Furaha alipoenda kutekwa nyara na Yule mwanamke haramu kama mimi nilivyopenda kumuita ambacho tulisadiki kitakuwa ni kiatu cha Yule mwanaharamu, nilipokiinua kile kiatu pale chini mara kwenye kisigino nikaona kama kumetikisika hivi halafu kukawa kama kuna vitu vinacheza cheza kwa ndani nilipokibinua na kukitoa kile kisigino mungu wangu mule ndani ya kile kiatu niliona kuna vifaa Fulani hivi vya mawasiliano, japo mimi sikuwa mtaaramu sana wa mambo ya erectronics ila niliweza kuona kuna kama kipaza sauti kidogo hivi, huku kikiwa kimeambatanishwa na vitu vingine vikiwa vimewekwa kwa ustadi mkubwa mule kwenye kile kisigino cha kile kiatu,nilijikuta naacha hata kuendelea kukusanya vitu vingine na kuludi kwenye kiti changu huku Amina akinitazama sana akiwa hajui ni kipi kilikuwa kinaendelea,nilimuonyesha vile vinasa sauti alishangaa sana pia na yeye, kumbe ndio maana kila siku tunakuwa tunalaumiana ya kwamba  huyu mwanamke siri zetu anakuwa anazipata wapi kumbe hiki kiatu ndio tukiwa tunazungumza yeye anazipata habari zote moja kwa moja mungu wangu, alizungumza Amina kwa sauti ya upole ila iliyojaa udadisi sana huku akitazama kile kiatu na kuitoa ile microphone na kuwa kama anaichezea chezea vile  mipango yake sasa mwisho wake umefika, nilimtazama kisha nikamuambia sikia hicho kiatu kitoe kwanza nje ndipo tuanze mazungumzo kwani hadi hapa tunapozungumza maongezi anayasikia huyu mwendawazimu, Amina alitii kile nilichomuambia akakitoa kile kiatu nje kisha akaludi mule ofisini kwangu tukaendelea na maongezi.
Kwetu tuliona ni hatua kubwa sana kwani mpaka pale tulikuwa tumefanikiwa kupata mkanda wa video uliokuwa na picha ya Yule mwanamke japo haonekani vizuri sana, lakini pia tulikuwa tumefanikiwa kugundua kifaa alichokuwa akikitumia kunasa mazungumzo yetu ambayo kuna kipindi mpaka sisi wenyewe ilikuwa inatuchanganya mpaka tukawa tunahisi wenyewe tunasalitiana, tulipanga usiku ule ule kwenda kuweka kambi mitaa ile huku tukiwa na kikosi cha kutosha kuhakikisha Yule mtuhumiwa tunamtia kifungoni siku ile kwani karibia mambo yote muhimu tulikuwa tumefanikiwa kupata basi nilitoka pale ofisini kwangu huku nikiwa nimemuacha Amina mule ndani na kwenda ofisi ya mkuu wetu wa kazi kwa ajili ya kumuambia maazimio tuliyokuwa tumefikia ili ikiwezekana aweze kutupatia vitendea kazi vya kutosha pamoja na wasaidizi wa kwena nao kwenye operesheni ya usiku ,mkuu wetu alituelewa akadai pia na yeye atashiriki katika ile operesheni siku ile akiwa kama msimamizi mkuu pia akasema tusiende wengi twende watu wa nne tu, tunatosha kumdhibiti, sikuwa na la kumpinga, nilijua pia ya kwamba mkuu na yeye alitaka akashiriki kwa minajili ya kujijengea umaarufu hasa kama tukifanikiwa kumkamata kwani kazi yote itaonekana kama aliifanya yeye ili aweze kujenga sifa nzuri ikibidi apandishwe hata cheo kwani mabosi wengi wa upelelezi huwa hapo hivyo wanapenda sana wao kupata sifa za mwishoni mwishoni, basi tulikubaliana pale na inspekta Thomas ambaye ndio alikuwa mkuu wetu wa kazi kwamba itabidi mida ya saa kumi tuanze safari ya kuelekea huko,basi tulitawayika kila mmoja akiendelea na shughuri zake.
                                             ****************************************
Mida ya saa 9 tulianza kujiandaa kwa ajili ya ile oparesheni tunayoenda kuifanya, tulichukua bastola kila mtu yake huku tukiwa na risasi za ziada za kutosha kwa kila mmoja kisha tukachukua kamera, zile picha tulizozipata kutoka kwenye ile kamera, intelligence auto mobile call, kisha kila mmoja wetu akavaa na kifaa cha kuzuia risasi kifuani, halafu mkuu wetu wa kazi pamoja na Amina walivaa miwani ambazo zilikuwa zina uwezo wa kuvuta picha umbali wa mita mia mbili. Baada kujihakikisha tupo tayari tulichukua moja ya gari zilizopo pale kituoni ambayo ilikuwa na namba za kiraia ili isiwe rahisi kugundulika. Tulianza safari yetu taratibu huku tukiwa tunapiga story tu zingine dereva akiwa ni mmoja wa wafanyakazi wenzetu pale ofisini aliyejulikana kwa jina la Salimu, ni moja kati ya vijana ambao mkuu wetu aliwapenda sana kuwatumia katika shughuri ambazo nay eye alikuwa anahusika tulienda taratibu sana kama vile tukiwa hatuna haraka yoyote huku mkuu wetu akisema ya kwamba sipati picha jinsi vichwa vya habari kesho au keshokutwa vitakavyokuwa vinapamba na hili tukio, sijui wataandikaje MUUWAJI AKAMATWA,MUUWAJI AULIWA, POLISI WAFANIKIWA KUMZIBITI MUUWAJI HATARI, mimi nilikaa kimya tu na kumungalia maana nilijua wazi shughuli iliyopo mbele yetu si ndogo kutokana na jinsi Yule mwanamke alivyokuwa  mjanja na mwepesi wa kucheza na akili zetu pia nilihofia ya kwamba huwenda alikuwa na habari kuwa tulikuwa tunaenda hivyo lazima atakuwa amejipanga kwa mawili iwe kukabiliana na sisi au kukimbia, basi tulifika mpaka kwenye hilo eneo na kupaki gari yetu mbali kidogo ili isiwe rahisi kufanikiwa kuonekana kisha tukashuka na kupanga ni jinsi gani tutelekea lile eneo mkuu wetu wa kazi akasema eti mimi na Amina ndio tutangulie halafu wenyewe watakuja kwa nyuma huku wakiwa kama wanafanya kujenga duara Fulani,nilijua tu Yule mkuu alitaka kama ni jambo baya litukute sisi halafu yeye aepuke sikuwa na jinsi zaidi ya kutangulia kwani kwa sheria zetu za kazi huwezi kumbishia mkuu wako wa kazi kwa kila atakalolisema, basi tulitangulia  mimi na Amina huku mimi ndio nikiwa kwa mbele zaidi, wakati tunzazidi kukalibia lile eneo mara kwa mbali nikaona mwanamke akiwa amevalia suruali ya kaki na juu t-shirt ya rangi ya kijivu akitokea upande wa pili na kuelekea sehemu ambapo palikuwa kama kuna mwamba Fulani, Yule dada alikuwa makini sana huku akiangalia upande huu mara ule, alipofika pale  akabinua kama jiwe Fulani kisha akazama ndani,atakuwa ndio yeye leo mwisho wake umefika sijui anatoka wapi nilimwambia Amina huku nikikimbia kwa kasi sana mpaka pale, ambapo nilikuta lile jiwe likiwa limefunikwa sikupoteza muda pale pale akili ikanituma haraka haraka nikamjulisha mkuu wa kazi kupitia zile intelligence mobile phones nilizokuwa nimevaa kwamba Yule mwanamke tumeshamuona alipoingia hivyo basi aongeze kasi waje kwa maana anaweza kutuzidia, sikutaka hata kusikia jibu lake pale pale nilifungua lile jiwe huku Amina akiwa ameshafika lile eneo, nilihangaika kwa muda wa kama dakika 2 hivi ndipo nilipofanikiwa kulitoa lile jiwe sikuamini nilichokiona mule ndani kwani kulikuwa na ngazi zilizokuwa zinateremka kuelekea chini huku kukiwa na mwanga hafifu, niligeuka nyuma kumuangalia Amina vipi upo fiti nilimuuliza akanijibu kwa kuonyesha ishara ya dole gumba kwamba yupo sawa, niliangalia kwa mbali nikamuona mkuu wetu akiwa na Salimu nao wakija lile eneo pale pale nilimuonyesha ishara ya tuzame chini Amina, kisha mimi nikaanza kushuka zile ngazi.
                                 ******************************************
Nilishuka huku nikiwa na tahadhari kubwa sana kwani sikujua Yule adui yetu alikuwa yupo mahala gani na pia alikuwa na silaha gani na isitoshe sikuwa na pafahamu vizuri mule pangoni,basi kila hatua niliyozidi kupiga na mwanga ndivyo ulizidi kuongezeka nilipiga hatua kushuka chini huku kwa nyuma nikimuona Amina akiwa ananifuata kwa ukaribu kabisa, pia nilisikia na vishindo vya kina inspekta Thomas na Yule Salim na wao ndio walikuwa wamefika na kuanza kushuka zile ngazi wakitufuata, nilishuka zile ngazi mpaka chini kabisa aithee lilikuwa ni handaki kubwa sana lile kwani kumaliza tu zile ngazi nilitumia zaidi ya dakika tano nilipofika chini kabisa sikuamini kwani nilijihisi kama vile nilikuwa nipo sebuleni kwa mtu palikuwa mahali pa pana kabisa pale huku kukiwa na baadhi ya vitu palikuwa pamechimbwa vizuri kiasi kwamba sikuweza kudhania kama nilikuwa pangoni, palikuwa na vitu muhimu ambavyo huwa vinakuwepo sebuleni kama makochi, television meza na kadhalika yani kwa ufupi ilikuwa ni sebule iliyokuwa imekamilika,sikutaka kuendelea kushangaa pale sebuleni kwani nilijua linaweza kuwa kosa na Yule adui akatukuta pale na kututeketeza wote kwani tulikuwa tupo kwenye himaya yake hivyo hatukujua alikuwa yupo upande gani.
Nilimsubili Amina na yeye akafika pale kisha na mkuu wetu akafika tukaangalia kisha tukapeana ishara tutawanyike kwenye ile nyumba iliyokuwa chini ya ardhi tulitawanyika sisi watatu huku mkuu wetu wa kazi yeye akiwa amebakia pale  sebuleni, basi mimi nilielekea upande wa kushoto ambapo nilikutana na kama chumba Fulani hivi nilipoingia nilikutana na geti la chuma ila likiwa wazi ambapo ilinibidi niingie kwa uangalifu sana, baada ya kuchungulia ndipo nilipogundua ya kwamba mule ndipo palikuwa selo ya Yule mwanamke kwani kulikuwa na majeraha ya damu damu sana mule huku kukiwa na vifaa vya kutesea watu kama shoti za umeme na vingine, nilizidi kushangaa ila sikutaka kupoteza muda tena nikachumpa upande wa pili nikajikuta nimetokea mahali ambapo nilihisi ndipo palikuwa chumbani  kwake kwa maana palikuwa pazuri ajabu huku kukiwa na mapambo na vifaa vya kisasa kabisa kama computer, air condition na vingine, nilijiuliza mule chini umeme Yule mwanamke aliupata wapi? Kwa maana palikuwa kama mchana, nilijaribu kupaangalia pia nikajihakikisha hapakuwa na mtu nikatoka haraka nikashika korido nyingine nikakuta mahali ni kama pa wazi Fulani hivi huku pakiwa na njia kubwa iliyokuwa ikielekea mahali ambapo palikuwa na mwanga zaidi nilizidi kuufuata ule mwanga mwisho nilijikuta nimetokea sehemu ambapo palikuwa na maji maji yaliyokuwa yamejenga kama mkondo Fulani hivi ukiwa umeingia kwenye kama mwamba Fulani pembezoni mwa bahari, wakati natoka ili niweze kupakagua vizuri nikaona boat moja ndogo ikitoka pale na kuelekea baharini umbali wa kama mita mia mbili toka nilipokuwa nimesimama, mungu wangu atakuwa ndio yeye huyu ametukimbia, nilijikuta nasema kwa sauti ya juu huku nikilaani, kugeuka kwa nyuma nikamuona Salimu na Amina nao kumbe walikuwa wameshafika pale, ndipo Salim alipoanza kutuambia ya kwamba yeye ndio alikuwa akimfukuzia alimuona mara ya kwanza kwa mbele kwenye kona moja akitokomea huku akiwa amebeba mkoba Fulani hivi na begi ambapo begi lilimzidi uzito hivyo basi aliliacha chini alimkimbiza  kwa kuhusi kwamba atamkuta, hatukuwa na jinsi tena ikatubidi tuanze kuludi sebuleni tumsikilize mkuu wetu atasemaje, tuliludi huku tukiwa tumelipitia lile begi alilokuwa amelidondosha na kisha kuludi pale sebuleni, kwa kweli wote tulishangaa jinsi ile nyumba ya chini ya mwanga iliyokuwa kwani kama mtu ungebebwa na kuwekwa tu pale katu usingehisi chochote kama upo kwenye nyumba iliyopo chini ya ardhi. Tuliludi pale sebuleni ambapo tulimkuta mkuu wetu yeye akiwa amekaa hana hata wasiwasi, tulimueleza ya kwamba tayari tumeshamkosa, akasema sawa sasa inabidi tufanye upekuzi mule ndani ili kujua kama kuna vitu vyoyote ili tuweze kuondoka navyo tulisimama na kuanza kuelekea chumbani kwake kwanza wakati tunakaribia kuingia mule chumbani mara umeme ukakatika ghafla, mungu wangu Amina alijihisi woga akanishika mkono na kuning’ang’ania
mule ndani palikuwa giza sana kiasi kwamba hatukuweza hata kuonana sisi kwa sisi na hatukuwa na mwelekeo wowote ule tena ilitubidi tusimamekwa dakika kadhaa ili tuweze kulizoea kwanza giza kisha ndipo tujue la kufanya, akili ikanicheza haraka haraka nikatoa simu yangu mfukoni ambayo ilikuwa na tochi kwa mbele nikaiwasha ile tochi ili angalau tuweze kufanikiwa kutoka mule ndani, ilibidi tuailishe kwanza zoezi la kuendelea kusachi mule ndani tukaona njia sahihi ni kutoka nje kwanza kwani hatukujua Yule mtu alikuwa amezima vipi ule umeme na isitoshe pia ingewezekana akawa ametegehsa hata mabomu mwisho wake tukajikuta wote tunalipuka mule  tulianza kutoka nje kwa tahadhari kubwa sana, tuliporudi mpaka pale sebuleni mara tukasikia sauti ya mtu akizungumza huku ikiwa na kama mwangwi Fulani hivi, mmeanzisha mapambano sasa sioni hata mmoja wenu ambaye atakaepona sasa, tuligeuka ili kungalia wapi sauti ilikuwa inatokea mara simu yangu ilipigwa na kitu ikadondoka chini, sikuaimi kile kitendo kwani kama ilikuwa risasi yenyewe ilitoka bila kelele yoyote na mlengaji akionekana akiwa na shabaha sana,paligeuka tena mule ndani kuwa giza huku wote tukiwa tumekumbatiana kwa hofu, nilianza kusikia sauti ya mkuu wetu wa kazi kwa chini chini akiboboja, nilimfunga mdomo asije kuharibu kila kitu, Yule mwanamke alizidi kuzungumza huku sauti yake ikiwa kama vile inajirudua rudia “haya kama nyie wanaume kweli tokeni basi tuone leo mwisho wenu umefika” nilizidi kuchanganyikiwa kiukweli toka nizaliwe sikuwahi kukutana na wakati mgumu kama siku ile, ilibidi tuwe wapole tu pale kwanza
 nilishangaa huyu mwanamkwe si ameondoka na boat sasa ilekuaje tena awepo mule mule ndani kipindi kile?na kwa nini alihindwa kutuuwa kama kweli alikuwa anatuona Au huyu mwanamke ni jini nini? Halafu tutachukuaje hatua wakati yeye hatujui amejificha upande gani kwani yeye tu ndio nilihisi alikuwa anatuona wakati sisi hatukujua alikuwa sehemu gani. Tulikaa pale kwa muda wa zaidi ya saa tano huku tukiwa hatuna jinsi ya kufanya kwa kuhofia usalama wetu,mpaka baadaye sana sikumbuki ilikuwa ni saa ngapi ila nahisi ilikuwa ni usiku sana ndipo simu ya mkuu wetu ilipoita na kuitoa mfukoni tena bila woga na kuanza kuzungumza nahisi ilikuwa ni simu ya mke wake kutokana na mazungumzo waliokuwa wakizungumza huku akiwa analalamika mbona alikuwa kimya sana siku nzima bila ya kumpa taarifa yoyote , baada ya kumaliza kuzungumza na ile simu mkuu wetu aliwasha tochi ya simu yake bila woga  alimulika chini pale tulipokuwa tumesimama kwa kuhofia kumulika pengine  kwa kuhisi Yule mwanaharamu angeweza hata kutupa adhabu yoyote ile au kutuuwa pia kwa maana Yule mwanamke ki ukweli alikuwa katiri sana,kwa pale chini alipomulika niliweza kuiona simu yangu nikainama na kuichukua wakati naichukua ndipo kwa pembeni yake niliweza kukiona kama kichuma Fulani chembamba kilichoipiga ile simu mpaka ikaanguka, mimi nilijua ni risasi kumbe ilikuwa tofauti  niliwasha simu yangu na kumulika juu kwa woga woga ndipo nilipoona kumbe kule juu kulikuwa na vyuma vingi sana hivyo basi kile kipisi kitakuwa kilikuwa kimeanguka tu  pia niliweza kuona vi spika vidogo vikiwa vimewekwa kwenye kona juu kabisa ambavyo ndivyo nilivyokuja kugundua alikuwa anatumia kutolea ile sauti
nilipata moyo wa ujasiri ghafla tena kwani nilijua sasa sio risasi kama nilivyokuwa nimedhania mwanzo, niliwambia wenzangu kwa sauti ya kuwanong’oneza ya kwamba inatubidi tutoke mule bila kuhofia chochote liwalo na liwe,kwani Yule mwanmke alikuwa natuchezea akili tu kwa kutumia teknolojia hata hakuwepo tulikubalina wote kwa pamoja kisha tukaanza kutafuta njia yakutokea kwa kutumia tochi ya simu yangu na ya mkuu tulifika mpaka pale sebuleni kisha tukaziona zile ngazi za kupanda kutoka, pale mwanga hafifu wa nje tulianza kuuona kwani muda ule ilikuwa ni usiku sana hivyo isingewezekana kuwa na mwanga sana.
                              **********************************
Tulifanikiwa kutoka nje ilikuwa yapata kama mida ya saa sita hivi usiku pale nje kando kando mwa bahari palikuwa pametulia sana hakukuwa na pirika pirika zaidi ya kuona kwa mbali boti za wavuvi zikieleka kando kando mwa bahari baada ya kumaliza shughuli za uvuvi, tulijiangalia kama wote tulikuwa tupo salama, tulijihakikisha wote tupo salama huku Salim akiwa amefanikiwa kutoka na lile begi liliokuwa na vitu mbalimbali vya mwanamke mwenye kovu jeusi,tulielekea hadi mahala tulipokuwa tumepaki usafiri wetu tuliokuwa tumekuja nao,tulilikuta gari likiwa vile vile kama tulivyokuwa tumeliacha.
                                         ****************************
Nilifika kwangu pakiwa pamepambazuka kabisa mida ya saa kumi na moja hivi, basi kwa kuwa nilikuwa nimechoka  na huku usingizi ukiwa umenishika sana niliingia ndani moja kwa moja chumbani na kulala,bila hata ya kubadili nguo nilizokuwa nimezivaa.
Nilikuja kushituka mida ya saa nne asubuhi baada ya simu yangu kuita ambapo baada ya kuangalia nilikuta kuna missed call zaidi ya tano, niliangalia simu ilikuwa inatoka kwa Gerald, nilimpigia ambapo aliniambia Yule mwanamke mwenye kovu jeusi jana usiku alimpigia simu na kumuambia ajiandae kwani zamu yake ilikuwa imefika kisha baada ya yeye nitafuata mimi, nilicheka kidogo kisha nikamuambia “sikiliza ndugu yangu huyu mwanamke anatapatapa tu hana lolote kwani mpaka sasa tumeshafanikiwa kuzibiti uwezo wake wa kupata taarifa zetu kitu ambacho ni kikubwa na kizuri zaidi halafu pia tumefanikiwa kuyagundua makazi yake ya ajabu yaliyo kwenye pango” nilizidi kumuhadithia jinsi usiku wa jana yake ilivyokuwa na kila kitu mpaka tulivyofanikiwa kutoka ndipo Gerald nay eye pia akanambia ya kwamba basi Yule mwanamke atakuwa ni hatari sana kayajuaje yale makazi kwani kwa upeo wake na kumbukumbu yake ndogo ni kwamba ile ilikuwa ni moja ya sehemu ambazo zilikuwa makazi ya waarabu enzi za ukoloni ambapo wakoloni walitumia kama sehemu za kujificha na ikiwezekana kutoroka pindi mambo yalivyokuwa hovyo, kisha Gerald akanambia ya kwamba mbona hata michoro ya mahala pale yapo mule ofisini na pale panajulikana kama pameshafungwa na Yule mwanamke pale sijui alipajuaje.tuliongea mengi huku akiniambia ya kwamba mkono wake ulikuwa ukiendelea vizuri nilimwambia ni vizuri basin a kama nikipata muda kesho jioni yake nitaenda kumsalimia.
Nilijiinua pale kitandani kisha kuelekea jikoni kwa ajili ya kupasha maziwa kidogo ninywe kisha niendelee na majukumu mengine kabla ya kujiandaa ili nielekee kazini maana tulipanga tukutane mida ya saa tisa,
Wakati naingia jikoni chini ya mlango wangu niliona kuna vitu vilikuwa vimetegeshwa huku vikiwa vimefunikwa na karpet niliviangalia ndipo nilipokuja kugundua kuwa vilikuwa ni vinasa sauti nilivichomoa pale nikaviweka sebuleni kwa minajri ya kwamba nitavipitia niende navyo ofisini kwani nilijua ya kwamba vilikuwa tu vimewekwa na Yule mwanamke mwenye kovu jeusi na swali langu kubwa lilikuwa ni wapi Yule mwanamke alikuwa anavitoa vile vifaa kwani vingine kwa jinsi vilivyokuwa advanced vingine teknolojia yake hata hapa nchini ilikuwa haijafika kweli mtu tuliyekuwa tunapambana naye hakuwa mtu wa mchezo hata kidogo.
                                   *********************************
Tulikuwa kwenye ofisi ya mkuu wetu inspekta Thomas tukiwa wanne mimi inspekta Thomas Amina na Salim, mkuu wetu inspekta Thomas alipandisha juu lile begi tulilolitoa janausiku  kule kwenye ile nyumba ya maficho ya Yule mwanaharamu alianza kulifungualile begi na kutoa vitu vilivyomo mule ndani, alitoa pesa  ambazo zilikuwa kwa juu juu tu pale ndani ya begi ambazo zilikuwa ni pesa za kimarekani zaidi ya dola elfu mbili kisha kwa chini kulikuwa na sura za bandia zaidi ya kumi na mbili huku tatu zikiwa ni za kike kisha kulikuwa na kopo Fulani ambali baada ya kulisomoa tuligundua kulikuwa na sumu hatari sana, nahisi ndiyo aliyotumia kumchoma nayo Gerald kule makaburini,pia kulikuwa na note book moja ambayo mkuu aliitoa alipojaribu kuiwasha kulikuwa na password, humu kuna siri kubwa sana inaonekana haiwezekani ifungwa na password ambazo zipo moja kwa moja kwenye system, alilalama bosi, huku akimsogezea Salimu ajalibu kuifungua, pia tulikuta palikuwa na passport sita mbili zikiwa za Tanzania huku zikiwa na sura tofauti, na majina tofatu, moja ikiwa ya Kenya, moja ya Africa kusini, moja ikimuonyesha kama ni raia wa visiwa vya shelisheli humu ya mwisho ikimuonmyesha kama ni raia wa brazil,mh mh mh aithe huyu mwanamke ni hatari yani hivi vitu vyote jamani lakini mwisho wake umeshafika,alizungumz Amina huku mwili ukiwa unamsisimka, chini kabisa ya lile begi kulikuwa na faili ambalo ndani yake kulikuwa na makaratasi mengi mengi sana, nililichukua na kuanza kuchambua zile karatasi nilikuta mkataba wa Yule mwanamke wa nyumba ya kupanga nchini Victoria sherisheri, ambapo palionekana ndio palikuwa ni makazi yake, hapo nilivuta picha na kukumbuka usiku ule aliotukimbia pale na ile boat nahisi ndio alikuwa anaelekea huko, pia nilikuta mkataba mwingine ukimuonyesha kama mpangaji kwenye nyumba moja iliyokuwepo mikocheni,pia kulikuwa na karatsi ambazo zilionyesha akiwa na akounti katika benki ya taifa ya biashara, baada ya kuona karatasi hii pia nikavuta picha za Yule mkaa marehemu ambaye dada yake ni mfanyakazi wa benki ya biashara pale makuu Zainabu,tena nilishituka sana kwani mara ya mwisho taarifa nilizozipata ni kwamba Yule dada alikuwa hoi hospitali ya taifa muhimbili akiumwa sana, mungu wangu nikitoka hapa leo itabidi nijaribu kwenda kumuona huyu dada sio vizuri nahisi pia atakuwa na siri nzito sana kuhusu huyu mwanamke,nilijikuta najisema mwenyewe huku tukiendekea kuchambua vitu mbalimbali ndani ya lilebegi,
kwenye  zipu ya pembeni ya lile begi Salim alikuta kuna simu aina ya nokia3350 ambapo baada ya kuiwasha ndipo alipogundua ya kwamba hakukuwa na laini ile wenye ile sumu kulikuwa na meseji mbalimbali zingine zikioneka  zimetoka nje ya nchi na kilichotushangaza zaidi na kutuchanganya kuna baadhi ya meseji tulizikuta mule zilionyesha kwamba Yule mwanamke alikuwa kama anapewa maeleko tu ya kufanya kwa malipo huku mtu aliyekuwa akimuelekeza ikionekana kama alikuwa ni mtu mmoja mkubwa serikalini kwani alimuambia asiwe na tatizo lolote likitokea yeye atamsaidia, wote tulishangaa, mkuu wetu alichukua simu yake na kujaribu kuipiga ile namba ya simu lakini haikuita aliambiwa namba aliyopiga haikuwepo, tuliona jambo la msingi ni kuikaihifadhi kisha tutaenda tume ya mawasiliano kwenda kuulizia wataweza kutusaidia zaidi,tulichambua sana mule na kuhakikisha kila kilichokuwepo tumekiona ilipofika mida ya saa kumi na moja mkuu wetu alisema twende tukale kisha mapema kisha tukiludi tumalizie ile kazi kwani yeye alikuwa na njaa sana mimi nilimjulisha ya kwamba nilikuwa nimeshiba kwani nilikuwa nimetoka kula si muda kabala sijaja kazini lakini mkuu wetu akasema si shida twende nitakunywa hata kinywaji chochote kwani sio vizuri nikibakia peke yangu mule ndani, katika kazi kuna muda wa kupumzika alinambia, basi sikuwa na kipingamizi zaidi kwa maana ningeonekana kama vile nimekataa ofa yake basi tulitoka kuelekea kwenye mgahawa ambao haukuwa mbali sana  pale ofisini huku vile vitu tukiwa tumeviacha mule ofisini kwa mkuu wetu.
                                           *************************************
Tuliporudi kutoka kula ilitushangaza sana baada ya kukuta ofisi ya mkuu wetu ikiwa wazi wakati tuliacha pakiwa pamefungwa,baada ya kuingia mule ofisini mule mungu wangu hatukuamini baada ya kukuta vile vitu vyote vikiwa havipo…..!!!
                                                *****************
Bosi wetu alihamaki kukuta mule ofisini kwake palikuwa peupe ilihali mlango tuliacha akiwa ameufunga, huku mlango ukiwa umeludishiwa vile vile, tulihamaki sana kutokana na ile hali
“Sasa huu utakuwa ni utoto sasa na haya ni zaidi ya matusi” alisema bosi kuhu akiwa amejaa ghazabu sana ilibidi tuanze kumshusha zile ghazabu ili tuanza kufuatilia ili kujua ni kipi kilichojiri, baada ya mkuu wetu kuwa mpole nilitoka nje na kumuita dada aliyekuwa pale kaunta ili kumchuma maelezo atuambie ni kipi kilichojiri,alikuja huku akionyesha wazi hakuna alilokuwa analifahamu, baada ya kuingia mule ndani mkuu alianza kumuuliza ya kwamba ni nani aliyeingia mule ndani, kwa kipindi kile kifupi ambacho sisi tulinda kula? Alionekana kama ni mtu aliyekwa akijaribu kuvuta kumbukumbu kisha akatuambia ya kwamba alipita pale mapokezi mdada ambaye alikuwa amevalia sare za kiaskari, na sura yake sio ngeni sana machoni pake, lakini hakumbuki ni nani kwa maana muda ule kulikuwa na askari wengi sana waliokuwa wamekuja kutoka depo, na muda ule walikuwa tayari wameshatawayika kwenda kwenye ma lindo sehemu mbalimbali baada ya kumaliza gwaride la saa 12 pale ofisini, tulimsikiliza kwa makini kisha mkuu wetu akampigia simu mkuu msaidizi wa kituo huku akimuomba amletee majina ya watu wote waliohudhuria paredi la saa 12 alikuwa na shida nayo sana,basi Yule OCS hakusita alikuja nayo mle ofisini kuhu akionyesha ya kwamba ndio alikuwa akiondoka kazini, aliniuliza kama kuna tatizo lolote,mkuu wetu alimjibu ndio kuna vitu vimepotea mule ofisini kwake katika muda mchache ambao tulikuwa tumetoka kwenda kula sasa kutokana na taarifa za askari aliyepo mapokezi anadai ya kwamba kuna mwanamke ndio alikuja humu kati ya wale waliokuwa kwenye paredi lile la jioni.
Basi walikubaliana ya kwamba itabidi kesho asubuhi na mapema watakapoludi kurepoti kabla ya kwenda kwenye makazi yao basi lifanyike paredi la ugunduzi ambalo latafanywa ka kusaidiwa na Yule mwanamke wa pale mapokezi, tulitawanyika pale huku mkuu wangu akinisisitizia mimi kesho niwahi mapema sana kwa sababu toka pale mnazi mmoja nilipokuwa nimepanga mpaka stesheni hapakuwa mbali sana hivyo itanibidi niwahi ili kufanya lile zoezi. Sikuwa na kipingamizi katika lile tulikubaliana nao kisha kila mmoja wetu akitawanyika
                               **********************************
Nilifika kwangu usiku ule mida ya saa mbili usiku baada ya kuoga nilivaa nguo mahususi kwa ajili ya kulalia kisha nikwa nimekaa naangalia taarifa ya habari, mara simu yangu ikaita alikuwa ni Amina akinijulisha ya kwamba alikua anaomba kama inawezekana nimsaidie kumpeleka kwake sinza mori kwani alikuwa na vitu vingi halafu alikuwa amekaa zaidi ya saa toka nilipomuacha pale stendeni ya vidaladala stesheni bila ya gari yoyote kuja, niliona si mbaya kwani Amina alikuwa ni mmoja ya wadada niliokuwa nao karibu sana pale kazini yeye pamoja na Jamila ambaye Jamila ni mdada niliyekuwa nampenda sana toka nilipomjua kwani alikuwa ni mkimya sana huku akiwa ni mtu asiyekuwa na makuu sema kwa kipindi kila Jamila alikuwa ameenda nchini marekani kwenye course ya social intelligence kwa takiribani miezi mitatu, muda mwingine nilikuwa namkumbuka sana Jamila kwani achilia mbali na kumpenda ila alikuwa ni mchapakazi na huku akili yake ikiwa nyepesi sana katika kuchambua mambo.
Nilimkuta pale stesheni Amina na kumchukua na gari yangu ili kumuwahisha kwakeambapo alikuwa akiishi peke yake kwa maana nay eye pia aliniambia atajitahidi kesho kuwahi hata kwa kutumia taxi wani alikuwa hajafanikiwa kununua gari, ili tuje tusaidiane katika lile paredi la utambuzi, basi tulienda taratibu kutakana na foleni huku tukipiga story mbali mbali tulifika kwake ilikuwa ni mida ya saa 4 hivi usiku basi wakati tumepaki gari nje tuliona taa za ndani kwake zikiwa zimeweka,Amina alishituka na kuniambia ya kwamba yeye pindi alipoondoka alicha taa amezizima, wakati tunajishauri mara kwa ndani kupitia dirishani tuliweza kumuona mtu kwa mbali ambaye baada ya kuona gari imesimama nay eye alichokifanya ni kuzima taa mule ndani hivyo basi tukakosa ujanja wa kuingia ndani kwa maana tusingeweza kuingia ndani wakati mtu Yule amezima taa na hatukujua ni nani na alikuwa na silaha gani.
Tulishauriana pale huku tukiwa hatuna la kufanya hatukutaka kuita watu kwanza tulijua tu atakuwa ni mwanamke mwenye kovu jeusi atakuwa ameingia kutegesha vinasa sauti vyake au kufanya upekuzi kama ilivyokuwa ada yake. Lakini kitu kilichotushangaza ni jinsi alivyoweza kucheza na muda kwani mara zote kila alipoenda sisi hatukuwepo sasa tulijiuliza kwa siku ile alijuje kama Amina atachelewa kazini. Tulijadiliana pale kwa zaidi ya  saa zima kwani yle mtu alikuwa kama akitufanya watoto akiwasha simu na kuzima mara ya chumbani mara ya jikoni mara ya sebuleni ili mradi tu kutuchanganya kisha nikamwambia Amina liwalo na liwe  nikamuomba bastola yake kisha nikachungua fungua na kuanza kuingia mule ndani, nilifungua mlango na kuwasha taa pale sebuleni sikuweza kumuona mtu, palikuwa pametulia tulii, nilijaribu kutazama tena kwenye korido sikuweza kumuona mtu, nilielekea jikoni wakati natokea tu nikaona mlango wa kule jikoni uliokuwa ukitoka nje pia ukifunguliwa na mtu akitoka kwa kasi ya ajabu akikimbia kulekea barabarani basin a mimi sikutaka kupoteza muda nilitoka nje ambapo aliniona nikija kwa kasi kumbe alikuwa makuja na piki piki akawa ameipaki nyuma ya ile nyumba aliponiona nakuija kwa kasi alishindwa hata kuipanda ile pikipiki na kuanza kukimbia kwa miguu akielekea barabarani, sikutaka kumuacha nilianza na mimi kumkimbiza huku nikimjulisha Amina kwa sauti sina hakuka kama alinisikia nilimkimbiza alishika barabara akawa kama anaelekea sinza parestina alikuwa na mbio za ajabu zijawahi kuona, nilizidi kumfuata kwa kasi ya ajabu huku bastola ikiwa tayari tayari mkononi na kwa muda mule barabara ilikuwa imeshakuwa nyeupe kwani watu wengi walikuwa maeshalala ilikuwasaa sita hivi inaelekea saa saba usiku, basi Yule mtu alipofika sinza makaburini alisimama kidogo na kuningalia kama nilikuwa bado namfuata aliponiona nilikuwa bado namfuata akakimbilia ndani ya makaburi, namimi sikutaka kujifikiria nilipofika pale na mimi nikaingia mule makaburini, sikuweza kumuona tena mule kila upande nilipoangalia hakuonekana, basi nikasimama mule makaburini kwa muda wa kama sekunde tano huku mapigo ya moyo yakianza kuongezeka nikasogea mbele kama hatua nane hivi palikuwa na kaburi kubwa ambalo lilikuwa limejengwa kifahari sana na likiwa limeinuka juu ambalo lilikuwa chini ya mti mkubwa wa mkuyu, nilimuangalia kama alikwa labda amejificha pale mbele ya lile kaburi lakini sikumuona, nilijikuta nakata tamaa na kuona potelea mbali haikuwa siku yake kumkamata basi nikageuka ili niludi kwa Amina niende zangu nikalale,mungu wangu kila nilipojaribu kupiga hatua nilihisi kama kuna kitu kinanivuta kwa nyuma,nilisimama nikajua kama ni Yule mtu basi atazungumza kitu au atafanya jambo lolote,nilisubili kwa muda wa zaidi ya dakika 5 bila kusikia wala kuhisi lolote nikajaribu kupiga hatua tena niondoke lakini wapi nilijikuta navutwa tena. Mwili ulianza kusisimka kwa maana sehemu yenyewe niliyokuwa ni makaburini palikuwa panatisha na ni usiku nilianza kujisemesha pale ili kama ni Yule mtu basi anijibu lakini wapi palikuwa kimya sana,huku upepo tu ukivuma kwa mbali,nilijaribu tena kupiga hatua kusogea mbele lakini wapi bado nilivutwa hapo hapo nikajua mwisho wangu umefika tayari…..!!
                          *******************************
Nilijitahidi kukauka pale kwa takribani robo saa bila kufanya lolote ili niweze kuona kipi kingefuata lakini hali ilizidi kuwa tofauti kwani muda ulivyokuwa unaenda ndivyo na mimi woga ulivyozidi kuniingia, “sasa si unidfanye lolote wewe uliyenishika jamani mbona wanifanyia hivyo” nilijikuta nazungumza kwa sauti iliyojaa utetemeshi sana, kila nilivyojaribu kuongea kwa nyuma nilihisi kama sauti ya viumbe wa ajabu amabo walikuwa wanazungumza ,mungu wangu haya yatakuwa mashetani sasa yamenishika sio bure, nilijikuta najisema mwenyewe moyoni, haiwezekani akawa mtu haya yatakuwa ni mashetani tu ni hivi nimekuja hapa makaburini mida hii ni saa saba inanenda saa 8 mungu wangu au itakuwa ni mizimu tu ya mtu mmoja wapo hapa makaburini, sasa sijui nitafanyaje mimi hapa?
mara kwa mbali sana niliweza kuona watu wakiingia mule makaburini mvulana mmoja na msichana wakiwa wanakuja mitaa ile niliokuwa mimi nilijua tu atakuwa jamaa ameopoa mwanamke anayejiuza mitaa ile kwani ile ni moja ya sehemu ambapo huwa kuna wasichana wengi wanaofanya biashara ya kuuza mili yao,pale pale nikajua itakuwa ni pona yangu labda ile mizimu iliyokuwa imenishikiria nyuma itaniachia,nikaanza kunyoosha mkono juu ili wanione, mungu wangu baada ya kuniona walikimbia sana huku wakipiga kelele basi namimi nilizidi kushituka huku mapigo yangu ya moyo yakizidi kwenda mbio, ooh watakuwa wameyaona haya mamizimu yaliyonishika huku nyuma, mungu wangu leo nimepatikana sio bure, au huyu mwanamke mwenye kovu jeusi atakuwa ni mzimu nini? Kwanini alikimbilia humu? Na kwa nini namtafuta haonekani jamani,
ilinibidi nisimame pale potelea mbali litakalokuja kutokea na litokee pia huku muda ukizidi kwenda kila nilipotaka kugeuka nyuma moyo ulikuwa unasita kwa kufohia sura yangu kukuta uso kwa uso na mizimu, kwani kwa mila za kwetu mtu ukiona sura za mizimu huo ni mkosi kubwa sana katika maisha. Nilikaa pale huku usingizi ukiwa unaninyemelea sana muda mwingine nilikuwa najihisi kusinzia mara nashituka na kuendelea kusimama sawa.
Ilipofika mida ya saa 9 hivi nilijaribu kugeuka nyuma kwa minajili ya kwamba litakalokuwa na liwe niligeuza shingo yangu pole pole sana kuangalia kule nyume kulipokuwa na lile li mti la mbuyu likubwa bahati nzuri sikuweza kuona kitu chochote, nikageuka mbele na kutaka kuondoka sasa lakini wapi bado nilijikuta nikiwa navutwa pale pale machozi yalianza kunitoka taratibu na kujua mwisho wangu ulikuwa umefika tayari maana ile mizimu itakuwa imekasirika kwa mimi kugekuka nyuma na kuangalia sura zao, niliendelea pale kusimama nakumbuka sikuwahi kusimama kwa kiasi kile zaidi ya miaka mitano toka nilipotoka kambini, kwa siku ile kwangu ilikuwa ni azabu tosha huku nikijiapiza kabisa ya kwamba kama nikiweza kunusurika pale itanibidi niombe kujitoa katika kufuatilia ile kesi kwani majaribu niliyokuwa nakutana nayo na jinsi utata uliokuwa ikijitokeza kila siku ulikuwa unanchanganya sana.
Nilisimama pale mpaka mida ya saa kumi na moja na robo hivi bila kukosea ndipo moyo wa jasiri ulipoanza kuniludia tena baada ya kuona tayari pameanza kukucha na jua kutokeza ikanibidi nigeuke nyuma tena ili kuiangalia ile mizimu ikiwezekana niiombe msamaha kwani muda waliokuwa wameniweka pale ilikuwa ni adhabu tosha sana upande wangu basi niligeuka  taratibu tena nyuma,sikuweza hata kufanikiwa kuona jambo lolote wala mtu yoyte kula ntuma zaidi ya ndege tu waliokuwa wapo juu ya ule mti wa mbuyu huku wakiwa wanalia lia kuashiria ya kwamba palikuwa pamekucha sasa,nilishusha pumzi chini kisha na mapigo yangu ya moyo yakaanza kuludi sawa,kwa maana wakati nageuka tena mapigo yalikuwa yanenda kasi sana.
Basi baada ya kujihakikishia pale hapakuwa na kitu chochote wala sura ya mzimuwala umbo kwa mara ya pili tena  nikajaribu kutaka kuondoka tena lakini bado nikajihisi navutwa,kuangalia ndipo nilipokuja kugundua ya kwamba kumbe kuna kipande cha nondo kilichokuwa kimetokeza kwa pembeni baada ya kaburi kujengewa kumbe ndicho kilikuwa kimechoma kwenye ile suruali yangu ya kulalia kwa chini na kusababisha nijihisi kama vile nimeshikwa navutwa.nilijichoma pale huku nikijilaumu kwa woga wangu wote umenifanya nilale makaburini bila ya sababu za msingi.
Niltoka pale makaburini haraka haraka ilikuwa yapata kama mida ya saa kumi na moja hivi nikaelekea moja kwa moja mpaka nyumabani kwa Amina ambapo nilikuta akiwa na wasiwasi sana hhuku akinieleza muda wote ule alikuwa hana amani moyoni kwani ilimbidi ampigie mpaka mkuu wetu simu kumjulisha kuhusu lile tukio, sikutaka kukaa sana kwani nilikuwa na usingizi sana kutokana na kulala makaburini kwa kujitakia, kisha nilimuhadithia tukio zima kwa nini ilitokea mpaka mimi nikalakla mule makaburini, alinionea huruma sana huku akiniomba nimsamehe kwani bila ya yeye kumsindikiza kwake haya yote yasingetokea.
Nilimuambia hakuna shida kwani ile ilikuwa ni kama ajali kazini kisha nikamsisitizia tuondoke naye muda ule ili mimi niende kwangu nikalale yeye aelekee kazini kwa ajili ya kwenda kufanya lile zoezi la utambuzi kwani jana amri ilitolewa watu wasitawanyike mpaka lilezoezi liwe limekamilika. Hivyo basi nilimsisitiza akalifanye lile zoezi kwa uangalifa sana akishirikiana na Yule dada ambaye alikuwa mapokezi pia pale pale tilimpigia simu mkuu wetu na kamanda wa mkoa wa kipolisi wa kinondoni kumuelezea hali halisi hivyo kama kuna hatua walikuwa wamepanga kuzichua basi waziache mara moja.
                                   **********************************
Nakumbuka siku ile nililala fofofo sana kwa ajili ya kulala makaburini bila ya kujitakia,ilikuwa kuamshwa saa kumi na simu ya Gerald iliyokuwa imeita zaidi ya nusu saa sasa niliipokea huku nikiongea kwa uchovu uchovu sana, aliniuliza wapi nilipokuwa nilimjibu nipo nyumbani kwangu ndipo kuna kitu kama alikuwa anataka kunielezea kuwa nitafute gazeti jioni ya leo haraka sana.nilishituka nikajua itakuwa wamefanikiwa kumzibiti Yule mwanamke mwenye kovu jeusi Au ameuliwa wakati akili sasa inatoka kwenye usingizi ili niweze kumuuliza vizuri kwani kulikuwa kuna habari gani zaidi hadi anipigie simu na kuongea kwa msisitizo vile mara simu yangu ikakata chaji na mtaani        umeme ulikuwa umekatika….!!!
                  *********************************
Nililaumu sana juu ya ule ukiritimba uliokuwa ukifanywa na shirika letu la umeme kwani  kwa mtu kama mimi kukata vile umeme walikuwa wananiathiri sana sababu nilikuwa na vifaa vingi sana ambavyo vilikuwa vikihitaji umeme,mungu wangu sasa hapa nafanyaje? Nilijiuliza nikaona hakuna jinsi zaidi ya kutoka nje na kwenda kuangalia hilo gazeti lilikuwa na habari gani kwani sikuwa na uhakika umeme ungerudi muda gani. Basi nilienda bafuni kwanza kuoga kisha nikavaa track suti zangu ambazo nilikuwa napendelea kuzivaa sana mida ya jioni kisha nikatoka zangu nje huku mkononi nikiwa nimeshika shilingi elfu moja kwa ajili ya kununulia hilo gazeti nilitoka nje na kushika barabara mpaka pale mahakama ya mwanzo ya mnazi mmoja ambapo ndipo palikuwa na vibanda vya kuuzia magazeti nilifika na kuanza kuangalia vichwa vya habari pale vya magazeti huku muuza magazeti akinitazama kwa umakini sana huku akitazama na gazeti alilokuwa amelishika kama vile akifananisha kitu hivi
Sikuamini baada ya kuliona lile gazeti ambalo Gerald aliniambia kama nimeliona macho yalinitoka  sana baada ya kuona kichwa cha habari “AFISA WA POLISI AMEFUMWA MAKABURINI AKIWANGA USIKU WA MANANE” huku juu ya lile gazeti kukiwa na picha zangu tatu zimepigwa nikiwa natoka makaburini, muyo wangu ulinyong’onyea ghafla nikajihisi mnyonge sana nililichomoa lile gazeti na kumpa Yule muuza magazeti pesa yake kisha mimi nikaanza kuludi zangu kwangu, nililikunja lile gazeti mkononi kwa kuwa nilipanga nitaenda kulisomea nyumbani.
                                ********************************
Niliwaza sana kuhusu ile habari kuwa pale juu ya lile gazeti kwanza nilihisi iliwekwa kwa dhumuni la kunichafua kwani habari yenyewe ilikuwa inadai ya kwamba nilienda kuwanga eti ili nifanikiwe kumtoa bosi wangu ili  mimi niweze kushika ile nafasi huku wakiwa wamepamba na maneno mengi tu ya uongo roho iliniuma sana kwani nilikuwa kwenye wakati mgumu sana  kwanza tayari walikuwa wameshaanza kunifitinisha na mkuu wangu wa kazi halafu pia ingeweza kusababisha nikatolewakatika kitengo cha upelelezi kwani sasa kila mahala ningepita watu wangekuwa wananijua hivyo basi ingeniwia vigumu san katika utendaji wangu wa kazi,nilifikiria lile gazeti la udaku ambalolilikuwa linatoka kila siku jioni walijuaje kama mimi nilikuwa makaburini mpaka wakanivizia na kunipiga zile picha, niliona tofauti na mazingira ya kazi yangu kuwa ngumu lakini pia jamii sijui itanichukuliaje katika lile jambo, hadi kunakipindi nikaanza kujilaumu kwa nini nilikubali kumsindikiza Amina usiku ule kwake kwani haya yote yasingetokea nilijipa moyo konde kwani nilijua mimi ni mwanaume jambo lile nikilitilia akilini sana lingeweza kuniathiri hata nishindwe kufanya mambo mengine niliamua vyovyote itakavyokuwa nitapambana na lolote litakalojitokeza.
Siku inayofuata sikuweza kwenda kazini kwani niliona ni bora kupumzika kwanza ili kuepuka maneno na pole ambazo ningekutana nazo kutokana na ilie tukio huku siku nzima nikishinda kwa dada yangu maeneo yak awe.
Kesho yake niliamka asubuhi na mapema sana ili kuwahi kazini kujua ni kipi kilichojiri kwani siku ile nzima simu yangu haikuwa na chaji hivyo sikuweza kupata majibu kutoka kwa Amina kuhusu lile zoezi la utambuzi kama lilikuwa limefanikiwa, nilitaka nikapate majibu kisha nielekee kwenye ofisi za lile gazeti ili kujua ilikuwaje mpaka wakaniandika vile.  Wakati naingia ofisini pale wakati napanda ngazi nilishangaa sana baada ya kuona kila mfanyakazi akinitolea macho huku wakijaribu kama kunikwepa hivi roho iliniuma sana baada ya kukutana na dada mmoja pale kazini na kumsalimia kwa kumpa mkono akakataa kupokea mkono wangu na wakati naondoka nikasikia akizungumza ya kwamba nilikuwa na dawa hivyo basi kwa atakayeshikana mkono na mimi dawa aliyopewa na mganga eti itamuingia.
Roho iliniuma sana kwa lile tukio nilifika mapokezi ambapo nilisaini kisha kuelekea ofisini kwangu ambapo Yule dada wa mapokezi pia alikuwa akinitazama kwa wasiwasi. Nilianza kufanya shughuli mbali mbali mule ofisini kwangu baada ya kama nusu saa simu ya mezani ya mule ofisini iliita ambapo niliambiwa nilikuwa nahitajika katika ofisi ya kamanda mkuu wa mkoa ambaye yeye ndio alikuwa mkuu wetu kwa mkoa mzima wa Dar-es-salaam upande wa polisi usalama barabarani na upelelezi, moyo ulishituka kwani haikuwa kawaida yake kukutana na watu ambao tulikuwa chini ya upelelzi kwani mambo yote alikuwa akitoa maagizo kwa mkuu wetu wa upelelezi wa mkoa inspketa Thomas, nilijiinua pale kitini na kutoka na kisha kuanza kupanda ngazi kuelekea floo ya mwisho ambapo  ndipo zilikuwepo ofisi zake niliingia mbapo nilimkuta kama mtu aliyekuwa akinisubiri kwa hamu sana, alianza kuneleza kwa sauti iliyojaa jazba sana kwamba mimi ni mshirikina sana toka zamani nawachezea wenzangu pale ofisini kwamba kila jambo lina mwanzo na mwisho “ si unaona sasa mpaka magazeti yamekuona” enhe hii ni fedheha sana katika jeshi letu hatuwezi kuvumilia hii hali, aliendelea kuzungumza bila kituo wala kunipa nafasi ya mimi kumjibu, hii haiwezekani hapa umeenda kinyume na tofauti zetu za kazi haiwezekani kabisa aliendelea kusisitiza,huku akiniambia kwa aibu zangu kutokana na lile tukio ndio maana hata jana sikuweza kwenda kazini, nilikaa kimya ambapo alizungumza mengi sana  kwamba mimi navujisha pia siri kwa mwanamke mwenye kovu jeusi ndio maana inakuwa ngumu sana kumkamata “usibishe kuna barua pepe zenu mlizokuwa mkitumia kuwasiliana nae na simu zenu tumezipata usizani huyo mwanamke wako mnamfuatilia nyie tu mpo vikosi vingi sana”  kisha akaniambia ya kwamba kuanzia muda ule nimeshushwa cheo changu cha afisa upelelezi msaidizi wa mkoa kwa muda usoijulikana nilijaribu kumuelezea hali halisi jinsi ilivyokuwa kule makaburini ya kwamba hata kama wanataka kuamini basi wamuulize Amina lakini hakuonekana hata kunisikiliza, sikia bwana Siwah hili ni agizo kutoka kwa kamishina wa polisi idara wa upelelezi makao makuu mimi hapa nilipo natimiza amri ya mkuu wangu tu, alisisitizia huku akinipa na barua na kuonyesha kama ni mtu aliyekuwa akitaka kutoka mule ofisini.
Sikutaka kubishana naye sana kwani nilijua tu ningeweza kupandisha hasira zangu tu, nilitoka mule ofisini huku roho yangu ikiwa inaniuma sana baada ya kusikia eti mimi nauhusiano na mwanamke mwenye kovu jeusi yani juhudi zote nilizozionyesha leo imekuwa vile? Sikuwa na jinsi niliona wameamua kutumia tu sababu zisizo na msingi ilimradi tu wanitoe kafara. Basi nilitoka pale ofisini na kuelekea mitaa ya gerezani ambapo ndipo zilipokuwa ofisi zalile gazeti la la jioni leo ambalo ndilo lilikuwa limeichapa ile habari iliyokuwa inanihusu mimi,nilifika pale mapokezi ambapo nilikutana na dada mmoja wa pale mapokezi nilimuomba kuonana na mhariri wa lile gazeti, Yule dada alianza kunijibu majibu ambayo sikuridhika nayo mara mhariri hajaja, oh hawezi kuonana na wewe kwa muda huu wa asubuhi aliongea mengi nikaona yote hayana maana kisha nikatoa kitambulisho change nikakiweka pale juu ya meza, alikiangalisha huku pia akinitazama na mimi usoni kisha akasema “oh kumbe ndio wewe”  nilihisi alikuwa tayari ameshajua tu kilichonipeleka pale ni kuhusiana na ile habari ya juzi kwenye gazeti lao basi alimpigia simu Yule mhariri kisha akanijulisha ya kwamba naweza kwenda huku akisimama na kunielekeza mahali ambapo ofisi yake ilipokuwa ndani ya lile jingo.
Niliingia mule kwenye ile ofisi na kumkuta Yule mhariri ambaye alikuwa kijana wa makamo tu kama mimi, tulisalimiana kisha nikamwambia ya kwamba nilikuwa nahitaji maelezo ilikuwaje mpaka wakaniweka kwenye habari mbele kwenye gazeti lao bila hata ya mimi kuniuluza, alionekana kujaa wasiwasi na woga hasa baada ya kuona mimi nilikuwa serious huku nikiwa sicheki ili kuonyesha msisitizo
Alianza kuniambia ya kwamba zile habari pamoja na picha wao walitumiwa na mwandishi mmoja kwa njia ya barua pepe aliyejitambulisha kwa jina la “ mwanamke mwenye kovu jeusi”.
Niliguna  kisha nikamwambia aendelee kunipasha, aliendelea kuniambia ya kwamba Yule mwandishi wa habari aliwatumia ile habari huku akiwa ameambatanisha na namba yake ya simu basi wao walichokifanya ni kumpigia simu na kumuuliza ili kupata uhakika zaidi ambapo aliwambia ni kweli kabisa, nilimkatisha kisha nikamuuliza “ je ile ilikuwa ni mara ya ngapi kwa yule mwanamke kuwapatia habari”
Aliniambia ya kwamba ilikuwa ni mara ya kwanza nay a kuwa Yule dada ni mwandishi wa habari za uchunguzi ndivyo yeye alivyodai ndio maana hata jina lake hakutaka lifahamike. Nilisononeka sana baada ya kusikia vile nilijua Yule mwanamke amefanikiwa kunivuruga kabisa kuanzia kwenye jamii hadi kazini kwangu.enhe unaweza labda kuniambia huyo mwanamke mmeshawahi kufanya nae kazi labda na pia yupo vipi mounekano wake? Halafu anakaa wapi? Nilijikuta namuuliza maswali mfululizo bila hata ya kusubili nijibiwe, Yule mhariri alijiua fika jilikuwa nimepaniki kwani alianza kunishusha hasira zangu kwa maneno yaliyojaa samahani na utetezi mwingi ili nisimchukulie hatua yoyote , tulijaribu kupiga ile namba aliyokuwa nayo ya Yule mwanamke lakini haikupatikana, baada ya kumaliza kupiga ile simu nilimwambia Yule mhariri awe makini na kazi yake kama miiko ya kazi yao imewashinda basi aachane na hiyo kazi akatafute kazi nyingine. Niliondoka pale ofisini huku hasira zikiwa zimenijaa sana kifuani kwani mpaka pale Yule mwanamke alikuwa amefanikiwa vizuri sana kunipotezea mwelekeo alionekana Yule mwanamke alikuwa ni mtu mjanja sana huku akiwa ni mtu mwenye mbinu mbalimbali ili aweze kufanikisha malengo yake.
Kule kusimamishwa kazi kwa muda usiojulikana kusema kweli kulinichanganya sana nilijaribu kuwasiliana na Amina na Gerald ili wanieleze ni kipi kilikuwa kinaendelea, lakini wote walionekana kama vile walikuwa wakinikwepa, nilijihisi mnyonge sana kwa kutengwa kwa sababu zisizo na maana nilijua watakuwa wameamliwa vile na mkuu wetu wa kazi eti kwa lengo labda siri zisivuje kwani walidai mimi nilikuwa na uhusiano na Yule mwanamke mwenye kovu jeusi. Nilikaa wiki nzima nyumbani bila hata ya kwenda popote nikisubilia labda nitaitwa kazini lakini ilikuwa tofauti mwisho nikaamua ni bora niende nyumbani Tanga nikapumzike na kusalimia wazazi kwani kuendelea kukaa Dar es salaam nilikuwa nazidi ku kuweka matatani maisha yangu bila ya sababu za maana.
Basi siku iliyofuata nilianza safari ya kuelekea nyumbani kwetu Tanga ambapo nilipanga niende nikapumzike angalau kwa muda wa wiki nzima kupumzisha akili huku nikiwa nasubili hatima yangu kazini nilondoka mida ya saa 6 hivi kwani Tanga sio mbali sana tena kwa mimi ambaye nilikuwa natumia usafiri wangu binafsi isingeweza kuchukua zaidi ya saa 4 kufika Tanga mjini maeneo ya chumbageni ambapo ndipo wazazi wangu walipokuwa wakiishi niliwachukulia wazazi wangu zawadi ndogo ndogo kwa maana ingekuwa ni aibu kwenda nyumbani nikiwa sina hata zawadi ya kuwapelekea wazee kwani ilikuwa imepita zaida ya miezi ita bila ya mimi kwenda  Tanga kwani mara ya mwisho nakumbuka ilikuwa kwenye msiba wa mtoto wa mama yangu mdog ambapo napo nilienda lakini sikukaa sana kwani ofisini nilipewa likizo ya siku mbili hivyo basi nilienda kuzika na kuludi tu. Nilianza safari yangu taratibu sana kwani nilijua hiki kipande cha Dar es salaam mpaka chalinze huwa kinakuwa na magari mengi sana hivyo sikutaka kwenda mwendo wa kasi bure nisije kupata ajali ya bila kujitakia  wakati naendelea kuendesha gari iliingia meseji kwenye simu yangu lakini sikutaka kuisoma kwanza kwani nikiwa naendesha gari hasa kwenye barabara kubwa kama ile morogoro road huwa sipeni kabisa kusoma meseji au kabisa hata kuwasiliana na mtu yoyote na simu ili kujiepusha na ajali zisizo na ulazima niliendelea na safari yangu huku nikiwa naskiliza nyimbo ya zilipendwa ya otto jazz ambao siku hizi wanaitwa msondo ngoma wosia kwa watoto, kwani ule wimbo mara zote ulikuwa ukinikumba enzi za zamani wakati baba yangu bado anafanya kazi katika mashamba ya mkonge kule hale muda mwingi alikuwa akiludi toka kazini basi alikuwa anawasha redio yake ya kanda kisha anauweka ule wimbo na kuniita mimi niusikilze,basi kwa kuwa nilikuwa naelekea nyumbani kila nilivyokuwa nausikiliza ulikuwa ukizidi kunipa hamu ya kufika nyumbani.
Nilipofika chalinze nilipaki gari njiani kwa ajili ya kununua bidhaa zingine za kwenda nazo nyumbani, wakati wale wafanya biashara wakiniwekea zile bidhaa kwenye gari ndipo nilipokumbuka ya kwamba kuna kipindi kuna ujumbe wa meseji uliingia kwenye simu yangu ya mkononi nilikuta ni ujumbe wa meseji kutoka kwa Yule mwanamke mweye kovu jeusi kama kawaida yake lakini akidai ya kwamba mpaka mimi ndio nilikuwa hatari katika kumfuatilia hivyo amejitahidi kunidhibiti kama niliendelea tena basi atanitoa uhai,niliguna huku nikiwa na hasira sana huku nikijiapiza nitakapoludi Dar-es-salaam nitaanza kumtafuta mwenyewe kwa siri nilitangaza kisasi nay eye mpaka nimpate kama ni uhai basi na mimi anitoe niliwasha gari nakuendelea na safari yangu taratibu sana.
                                               *******************************
Nyumbani niliwaelezea kisa chote ambapo walinionea huruma sana kisha mama akaniambia inanibidi niwe makini sana na watu wa mule ofisini kwani inawezekana kabisa tukawa tunachezeana mchezo kwa sabau ya wivu na kuona jinsi labda nilivyokuwa makini sana katika kazi zangu.sikiliza mwanangu katika hizi ofisi watu hawapendani kabisa bora utambue hilo huwezi jua itakuwa labda wametumia kigezo hicho ili kukuondoa ofisini alinieleza mama yangu huku tukiwa tumekaa varandani jioni tukinywa chai kwani nyumbani kwetu tulipenda sana kunywa chai jioni pamoja na chapatti mihogo,bagia,na nyama ya kusaga,basi pale mama alinihusia mambo mengi sana moja wapo likiwa ni kuoa kwani umri ulikuwa unanitupa mkono sana, alivyozungumza vile nilimkumbuka sana Jamila mwanamke shupavu ambaye tulikuwa tukifanya nae kazi lakini ilikuwa muda sasa akiwa masomoni akiwa ameenda kuoneza ujuzi wa elimu yake, nilimkumbuka kwa sababu alikuwa mwanamke mzuri sana mwaminifu mwenye heshima huku akiwa ni mtu aliyenijali sana japo kila nilipomuomba tuanzishe uhusiano alikuwa akikataa bila ya sababu za  muhimu eti ya kwamba alikuwa akinionea huruma.
Usiku ule nilijaribu kumuandikia barua pepe kwani ndio nji niliyokuwa naitumia kuwasiliana naye huku nikimpa mkasa mzima ulionikuta,nililala siku hiyo usiku sana kwani kwani muda mwingi niliutumia kuwa kwenye  net huku nikifungua kurasa mbalimbali kusoma njia mbalimbali za kiitellejensia zilizokuwa zinatolewa kwa njia ya mtandao nilijikuta nikijifunza njia mbalimbali za jinsi ya kuchunguza  na kufuatilia uhalifu ambazo kwangu niliona zingenisaidia sana .
Kesho yake baada ya kumaliza mizunguko ya hapa na pale huku nikipita sehemu mbalimbali kuona jinsi mkoa wangu wa Tanga ulivyokuwa umebadilika kwani sikuwa nimepata kwa muda mrefu,nilizunguka sana kwa kutumia gari yangu huku nikiwa na mdogo wangu wa kiume  William,
Jioni nilimwambia sio mbaya kama tukielekea raskazoni ambapo ndipo palikuwa na beach nzuri twende tukapunge upepo maana pia sehemu zile nilikuwa na muda sana sijapata kuhudhuria kwani kwa Dar-es-salaam muda mwingi nilikuwa nakuwa bize sana kaziBasi tuliona kuingia katika beach za Kiswahili isingekuwa vizuri sana hivyo basi tukaona ni bora tuingie Mkonge hotel ambapo pale tulikuwa tukipigwa na upepo moja kwa moja wa bahari huku tukiziona meli zilizokuwa zikiingia na kutoka katika banadri ya tanga tulikaa pale huku mdogo wangu yeye akiwa anatumia kilevi ila mimi sikutaka kunywa kwani akili yangu ilikuwa bado haijakaa sawa tuliendela kukaa pale huku nikitumia muda ule kumshauri mdogo wangu kwani nilipata malalamiko kutoka kwa mama kuhusu baadhi ya mienendo yake wakati tunaendelea na mazungumzonilitaka kumpigia simu mama kumjulisha ya kwamba chakula cha jioni wasituhesabu kwani tungeweza kuchelewa ndipo nilikumbuka ya kwamba nilisahau simu yangu moja niliisahau kwenye gari, nilimpa ufunguo wa gari yangu mdogo wangu na kumwambia aende kunichukulia simu yangu. Aliondoka pale tulipokuwa lakini baada ya kama dakika saba nilimuona akitokea kwenye kona huku akiwa analudi kasi sana pale nilipokuwa huku akiwa ananiita jina langu kuashiria kabisa hapakuwa salama.
Nilishituka na kumfuata ili tukutane nae njiani, alikuja kasi sana na aliponifikia alinishika huku akihema na kunielekeza tutoke nje haraka sana pombe zote ilionekana zilikuwa zimeshamtoka kichwani, kaka  kaka Mary nimekutana nae akitoka kweny gari yako, alizungumza huku akiwa anathema sana kiasi kwamba amneno yalikuwa yanatoka huku yakiwa yamekatika katika sana mpaka maneno mengine nikawa siwezi kuyasikia tulitoka nje mpaka kwenye parking ambapo tulikuta gari langu mlango wa mbele ukiwa wazi , mdogo wangu alianza kunieleza ya kwamba wakati anatoka nje alikutana na Mary akiwa kama vile anapekuwa kwenye lile gari langu na baada ya kumuona anatoka alichomoka haraka haraka sana na kuondoka huku akiwa ameondoka na simu yangu, nilimsikiliza kwa makini sana kisha nikamuuliza wewe unamjua huyo mtu? Alinjibu huku akili ikianza kumludi sawa baada ya zile pombe alizokuwa amekunywa kuanza kumuisha kichwani, ndio namjua japo sio sana kuna siku alinipigia simu na kukutana nae pale capchino ambapo ambapo tulizungumza nae mambo mbali mbali ya biashara. Mh niliguna baada ya kusikia mambo ya biashara kisha nikamwambia aendelee kunielezea, alidai ya kwamba Yule mwanamke ni mfanya biashara akiwa anajihusisha na biashara ya kuuza milungi akiitoa nchini Kenya hivyo basi alikuwa anataka nimsaidie kumkutanisha na wewe ili iwe rahisi kwake yeye kuwa anaiingiza Dar-es-salaam, sikuweza kupata muunganiko kati ya biashara na mimi gari yangu kusachiwa kisha kuondoka na simu yangu, niliingia ndani ya ili gari nakaiangalia angalia ndipo nilipokuja kugundua ya kwamba kumbe alikuwa ameweka kinasa sauti kidogo sana mbele ya gari kwenye ubao ulioshikilia kioo nahisi baada ya kumuona mdogo wangu alikurupuka ndio maana hakuweza hata kukiweka vizuri kile kinasa sauti, hapo hapo akili yangu iligutuka na kujua atakuwa tu Yule mwanaharamu, sasa nilianza kujiuliza je alijuaje kama mimi nimeenda nyumbani? Hapo ndipo palianza kunitatiza nilimpa pesa ya kulipia vinywaji mdogo wangu na kisha kumuambia ya kwamba yeye aende akalipe kisha aje tuelekee zetu nyumbani kwani siku yangu nilihisi ilikuwa imeshaharibika tayari.
Tuliondoka pale mkonge  hotel huku akili yangu ikiwa imezidi kuvurugika nilijihisi kama maisha yangu yanazidi kuwa hatarini hivyo nilikuwa nahitajika kuchukua hatua za tahadhari mapema sana.wakati tunakaribia kmitaa ya makataba mdogo wangu alinionyesha kwa mbali Yule mwanamke huku akiwa amevaa hijabu kabeba na mkoba akiteremka kuelekea bondeni ambapo palikuwa na barabara ya kuingia bandarini basi na sisi tuliongeza mwendo na kwenda kushika njia ya kuingia bandarini  tulifika pale bandarini ambapo palikuwa na harakati sana kwani kulikuwa na meli ya mizigo iliyokuwa inapakia sementi nilishika kwenye gari na kuwauliza wale walinzi wa bandari, kama wamemuona mdada mmoja akiingia mule walinijibu ndio Yule dada alikuwa akielekea shelisheli na ile meli ya sementi mume wake ndio alikuwa amechukua ule mzigo. Nilishangaa sana kusikia vile, mara kwa ndani nikamuona Yule mwanamke akiwa anazunguka mule ndani alipotuona tupo getni alijifanya kama kushituka vile ahalafu akaongeza mwendo kuelekea kwenye gati palipokuwa pamepaki ile meli ya mizigo na mimi niliona wale askari wa bandari walikuwa wananichelewesha wakati mbaya wangu namuona kwa mbele akipotea kwenye macho yangu nilitoa kitambulisho changu haraka haraka kisha nikamuachia mdogo wangu ufunguo wa gari kisha na mimi nikazama mule bandarini niliingia mule moja kwa moja mpaka kwenye ile meli na kuanza kumsaka huku nikiwa na tahadhari kubwa sana. Niliendelea kumsaka mule bila mafanikio mpaka mida ya saa 4 usiku huku nikiwa nasaidiwa na baadhi ya askari wa bandari, mwisho meli ilimaliza kupakia mizigo na kuanza kupiga honi kuahiria kwamba ilikuwa tayari kwa safari, sikuwa na jinsi zaidi ya kujikatia tama na kuanza kutoka nje wakati meli inaanza taratibu kuacha ardhi na kuelea baharini kwa muda kama dakika ishirini hivi huku nikiwa nimejisimamia nikiwa sina la kufanya ndipo nilipomuona kwa mbali Yule mwanamke kwenye ile meli ya mizigo akipanda ngazi kutokea chini akieleka juu roho ilinimua sana kwani kwa pale nisingeweza kumpata tena nilitoka mule bandarini nikiwa sina jinsi tena mungu wangu huyu adui kweli kama kucheza na akili yangu basi amefanikiwa sana tu,
                            *****************************
Kwa kuwa nilikuwa bado nipo likizo niliamua kufanya maamuzi magumu ya kwenda shelisheli kwani nilijua Yule mwanamke kule patakuwa ndipo panamakazi yake kwani nakumbuka hata mule pangoni katika zile hati za kusafiria tulizozikamata moja ilikuwa ikimtambulisha kama ni mtu wa visiwa vya shelisheli basi nilijua inaweza kuwa kweli kwa maana nilikusudia kumsaka mahala popote kwani salama yangu ilikuwa ni yeye kukamatwa kwani sasa ilibainika ya kwamba mimi pia nilikuwa nahusika na Yule mwanamke sasa ilinibidi kutumia juhudi zangu binafsi ili niweze kuwathibitishia ya kwamba sio mimi pale kazini walinisimamisha tu kutokana na chuki zao binafsi.siku ile ile asubuhi niliwaaga nyumbani kuwa niludi Dar-es-salaam kulikuwa na dharura imetokea kumbe upande wa pili nilikuwa nataka niende nikafanye utaratibu ili ikiwezekana siku ile ile niweze kupata visa ya visiwa vya sheli sheli ili jioni yake nianze safari ya kuelekea kule kwani nilijua kama nikiweza kupata usafiri wa ndege nilikuwa na uhakika kabisa wa kuiwahi ile meli kabla haijafika hivyo  basi ningeweza kumuona Yule mwanamke pindi ile meli ikiwa inashusha mizigo.nilifika Dar-es-salaam mida ya saa 5 asubuhi ambapo nilipitiliza mpaka kwenye ofisi za ubalozi wa shelisheli nchini niliingia pale na kukutana na afisa mmoja katika ule ubalozi nilimueleza ya kwamba nilikuwa naenda mapumziko mwezi mmoja, nashukuru kati ya nchi ambazo zilikuwa na uhusiano mzuri na Tanzania na ambazo hazikuwa na taratibu ngumu sana sisi kwenda Shelisheli nilogongewa pale visa yangu kisha moja kwa moja nikaelekea ofisi za afrifight agent ambazo zlikuwa ni ofisi za mawakala wa tiketi za ndege, niliwauliza wahudumu wa pale waliangalia kwenye computer kisha  waliijibu ya kwamba kwa siku ile kulikuwa na Kenya airways ambapo ilikuwa inanipasa niende mpaka Nairobi kisha niunge na ndege nyingine.ya shirika lile lile mpaka shelisheli basi baada kumaliza ile booking ya ile ndege ambayo walisema ilikuwa inaondoka saa kumi na moja jioni, basi sikuwa na jinsi zaidi ya kuelekea nyumbani kwangu kwenda kupaki gari langu kisha nichukue taxi iweze kuniwahisha uwanja wandege kwani muda uliokuwa umebakia ulikuwa ni mdogo sana kwani pale ilikuwa tayari imeshafika saa 8 na robo. Hivyo ilinipasa kuongeza mwendo.
                                 **************************************
Nilifika kwangu na kuchukua tu nguo zangu chache sana nikaziweka kwenye begi lagu dogo, laptop yangu, viatu na raba pea moja kisha nikachukua na atm yangu ya Barclays bank kwani sikutaka kubeba hela nyingi ule ulikuwa ni utaratibu wa kizamani sana ndio niliona hivyo nilichukua ile ya Barclays ili nikifika kule niweze tu kupata huduma kupitia visa card na master card nilikuwa nipo simple sana kiasi kwamba kama mtuangeniona asingezania kama nilikuwa na safiri.
Nilimaliza kupaki vitu vyangu huku muda ukiwa umeenda sana kisha nilitoka nje na kuchukua taxi kwani pale nyumba niliyokuwa naishi kwa nje kulikuwa na tax nyingi sana zilizokuwa zinapaki nilipanda kwenye taxi moja kisha na kumuambia dereva anikimbize uwanja wa ndege kwani muda ulikuwa ni saa tisa kasoro kama dakika kumi hivi dereva alitoka kwa mwendo mzuri sana huku akijaribu kupita sehemu zingine kwenye panya road ilimradi tu tuwahi kufika tulipofika stesheni tulikutana na foleni kubwa sana kwani trafiki pale alikuwa amkasirika kisa deriva daladala mmoja alimwambia kwa nin alikuwa akivuta magari ya upande mmoja tu?basi kwa hasira ule upande akaamua kuuacha kabisa kuruhusu magari kupita kwa muda wa zaidi ya saa sasa niliangalia pale ilikuwa tayari imeshafika saa kumi na robo. Mapigo ya moyo yalizidi kuongezeka kwani ndege ilikuwa inaondoka saa kumii na moja kamili na muda wa kufika ilikuwa na saa moja kabla basi pale pale nikaampa Yule dereva taxi elfu kumi kisha mimi nikashuka zangu nakupanda boda bodaili niwee kuwahi ndege kwani ilikuwaimefika kwenye saa kumi na dakika ishirini hivi.
Yule dereva wa boda boda aliniondoa  kwa kasi ya ajabu sana pale tazara huku akijitahidi kuvuka magari kwani yalikuwa mengi sana kutokana na ile foleni iliyosababishwa na yule trafiki pale kwenye mataa, nilifika uwanjani ilikuwa saa kumi na moja kasoro dakika ishirini, niliruka kwenye pikipiki kisha nikamkabidhi yule dereva wa boda boda kiasi cha shilingi elfu tano sikutaka hata kuulizui chenji kwani juda ulikuwa umeenda sana ,nilikimbia kama mtu aliyekuwa anakimbia hatari Fulani hivi nilifika mahali palipokuwa na wale wakaguzi walitazama tiketi yangu huku begi langu likipita mahala pa ukaguzi nilipita haraka na kuelekea kwenye line namba moja kwani ndipo ndege niliyokuwa nasafiri nayo ndipo ilikuwa imepaki ikijiandaa kupaa niliikimbilia ndege huku nikipiga kelele za wanisubili kwani jamaa walikuwa wanataka kufunga mlango sasa.Nashukuru sana mungu nilifanikiwa kuingia kwenye ndege japo kwa kuchelewa sana nilikaa kwenye seat huku ndege ikianza kuiacha ardhi taratibu.
                                           *****************************
Nilifika  visiwa vya shelisheli mida ya saa 7 usiku kwani tulichelewa sana uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta Nairobi nchini Kenya, kwani ndege nyingine tulikuwa tukiisubili kutokea Egpty ilichelewa sana, nilishuka pale uwanja wa ndege wa visiwa vya shelisheli uliokuwa ukijulikana kwa jina la aeropor intertanional de seyc pointe larue, uliopo kwenye mji mkuu wao unaojulikana kwa jina la Victoria basi nilienda mpaka mapokezi ambapo nilitoa hati yangu ya kusafiria yule dada wa pale uhamiaji aliikagua ambapo aliona nilikuwa nimeingia mule kama mtalii kisha akaigonga mhuri na kuniruhusu kuengia huku upande wa pili begi langu nalo pia likipita kwenye  mkanda wa kukagua mizigo ambapo pia hawakuona kitu. Nilipitia katika duka la kubadilisha fedha lililokuwa pale pale uwanja wa ndege ambapo nilibadili pesa zangu chache nilizokuwa nazo kutoka kwenye shilingi kwenda kwenye rupee kwani pale shelisheli walikuwa wanatumia rupee kisha nilitoka njen a kukuta taxi nyingi zikiwa zimepaki zikisubili abiria wanaoshuka kutoka kwenye ndege
Nilimuomba yule dereva wa taxi anipeleke kwenye hoteli ambayo haikuwa na gharama kubwa sana ili niweze kuzimudu kwa muda wote nitakaokuwa mule kwani sikuwa na kiasi kikubwa sana cha pesa na pia ile safari nilikuwa nimejigharamikia mimi mwenyewe kwa pesa yangu ya mfukoni, aliniskiliza kwa makini kwani nchi ile watu walikuwa wanatumia lugha mbili kiingereza na kifaransa sasa yule dereva ilionekana yeye alikuwa anajua sana kifaransa kuliko kiingereza kwani hata kunijibu kwake kulikuwa kwa wasiwasi japo alikuwa mchangamfu sana tulianza safari ya kutoka pale uwanja wa ndege na kuelekea kwenye hoteli ambayo ndio nilikuwa naenda kufikia iliyojulikana kwa jina la silhouette island hotels, moja ya hotel yenye hadhi nzuri huku ikiwa na bei ya kumudu kwa mtu yoyote yule huku ikiwa jirani na bandari kwani nilimdanganya ya kwamba mimi nilikuwa ni mfanyabiashara nilikuwa nasubili meli yamgu iwasili niweze kupakua mizigo, basi usiku ule niliweza kuuona ule mji wa Victoria kiukweli ulikuwa ni mji mzuri sana huku kuna sehemu kukiwa na  mifereji kutoka baharini na kuingia ardhini huku sehemu zingine kukiwa na madaraja tuliyotumia kuvuka kutoka kisiwa kimoja kwenda kingine yani ile nchi sikuwahi kuona ilikuwa nchi yenye visiwa vingi vidogo vidogo sana vingine vikiwa vimeungana vingine vikiwa vimeachana na kutenganishwa na mfereji mdogo wa maji ya bahari.
Nilimlipa yule dereva wa taxi pesa yake kisha mimi nikajivuta na kuingia kwenye ile hoteli nilikuta vyumba bado vikiwepo nilichukua chumba ambacho kilikuwa kipo juu ambapo nilikuwa na uwezo wa kuona shughuri zote zilizokuwa zinaendelea katika bandari yao ya pale Victoria nilifurahi sana kwani nilijua ya kwamba kupitia pale ningeweza kuifuatilia ile meli ambayo nilikuwa na uhakika siku ile asubuhi lazima ingewasili tu pale bandarini.
                                               *******************************
Kesho asubuhi na mapema baada ya kumaliza kunywa chain a kuosha mwili wangu niliamua sasa kuianza ile kazi moja kwa moja ya kumsaka yule mwanamke nilivaa kofia za wapanda farasi kisha nikaweka na miwani usoni ili kiasi kwamba isiwe rahisi kwa mtu kunitambua kirahisi kwa maana nilijua yule mtu ni hatari nisipokuwa makini itakuwa tatizo ukizingatia hata sikuwa nimeaga mtu yoyote nilitoka nje na kuanza kutembea taratibu kuelekea kule palipukuwa na bandari yao nilifika pale mapokezi na kujifanya naulizia kama kulikuwa na meli yoyote iliyokuwa inatikea Tanzania  kama ilikuwa imeshafika kwani kulikuwa na mzigo wangu yule dada wa pale mapokezi wa bandari alinitazama sana kisha akaguna na kunijibu ya kwamba mbona wao wanavyojua meli iliyokuwa imeenda kubeba simenti Tanzania ilikuwa imekodiwa yote  na mkodishaji alikuwa ni serikali ya pale shelisheli na ilikuwa imeende kubeba simenti kwa ajili ya kutekereza mpango wao wa kujenga nyumba za bei nafuu kwa wananchi wa shelisheli, nilijikuta Napata kigugumizi kisha nikamwambia ya kwamba niliwamomba na mimi nipakie mzigo wangu wa  machungwa kwa makubaliano maaalumu, yule dada alisema lile ni tatizo kwani kwa nchi yao pale itahesabika kama rushwa hivyo lazima yule msimamzi wa ile meli atakuwa hatianika kwani atakuwa amevunjwa sheria za nchi niliona yule dada maneno yakiwa mengi ndipo nikaamua kumwambia “ sawa basi nimekuelwea ila nachokuomba hapa ni kunijulisha tu lini hiyo meli inaingia lini hayo mengine itajulikana nikifika” alinijibu inaingia leo mchana kwani ilipita pia Mombasa kupakia sementi zingine  kutoka kiwanda cha East Africa Portland cement,hivyo basi itanipasa kugeuka pale mchana kuanzia mida ya saa tisa hivi,
Nilianza kuondoka pale huku nikiwa na wasiwasi baada ya kusika ile meli imepitia Mombasa kwani nilijua moja kwa moja inawezekana yule mwanamke akawa ameshukia Mombasa, nilianza kujiuliza maswali mengi sana  kuhusu yule mwanmake na ile meli uhusiano wao baada ya kuambiwa ya kwamba ilikuwa imekodiwa na serikali ya shelisheli, au inawezekana yule mwanamke atakuwa na uhusiano na kati ya nahodha au baharia katika ile meli ndio swali nililojiuliza kichwani,ok sawa yote yatajulikana ngoja kwanza hiyo meli ifike ndipo nitajua kipi cha kufanya, nilijirudisha katika ile hoteli niliyokuwa nimefikia ili niweze kupata chakula cha mchana kisha nikae dirishani kuangalia iyo meli kuona pindi itakapoanza kuingia, nilimazlia kula kisha nikasogelea computer iliyokuwa ipo mule chumbani kwangu  mahususi kwa ajili ya wateja kisha nikaiwasha na kuanza kufungua mitandao mbalimbali ya kitanzania ili niweze kitambua ni kipi kilikuwa kinaendelea nyumbani nilifungua barua pepe yangu ambapo nilikuta kuna ujumbe mbalimbali kutoka kwa rafiki zangu mbalimbali huku pia na kipenzi change Jamila akiwa amenijibu na kunijulisha ya kwamba baada ya wiki atakuwa ameshaludi nchini huku akiniambia alikuwa ameshamaliza mafunzo yake kule marekani huku akinipa pole sana kutokana na masahibu yaliyonikuta   na kuniomba ni bora niache kujishughurisha na kumfuatilia yule mwanamke mwisho na mimi nisije kupotea duniani bure wakati yeye akiwa bado ananihitaji, nilijitahidi kumjibu vizuri huku nikijitahidi kupangua zile hoja zake kwa njia tofauti kwamba hata kama yule mwanamke nikiachana naye ila kwa yale mauaji yake ya kutisha siku moja angeweza kuniua kama sio mimi basi hata yeye pia kwani alikuwa akifanya mauaji hovyo na hata bila ya kutoa sababu za msingi wala kusema ni kipi alichokuwa kikitaka.
Baada ya kumaliza kumjibu barua pepe Jamila ndipo nilipofungua mtandaa wa kijamii wa Darhotwire sikuamini nilipokutana na picha ya mwanaume aliyelala hku damu zikimtoka sehemu mbalimbali na pia kukiwa na alama nyeusi ikiwa imeziba sehemu zake nyeti huku kukiwa na kichwa cha habari “afisa wa polisi afanyiwa mauaji ya kutisha” akatwa na kisu nyeti zake sehemu za siri mwili ulianza kusisimka nakujihisi kupata kibaridi Fulani hivi cha woga baada ya kungalia picha ile kwani ilikuwa ni picha ya mkuu wangu wa kazi inspekta Thomas.
                                 *******************************
Mwili ulinisisimka sana nikajihisi kuishiwa nguvu huku machozi yakiwa yananitoka kwani nilijua kifo cha mkuu wangu wa kazi na hivi nilikuwa nipo kwenye mgogoro nay eye basi ungeniweka matatani kabisa kwani tulikuwa tupo kwenye mgogoro na yeye kabla ya kifo chake sasa kitendo cha yeye kufa tena kifo cha kutatanisha ilimaanisha kabisa ningehisiwa ni mimi nimefanya vile ili kuwakomoa au kuonyesha ya kwamba sio mimi japo wamenisimamisha kazi lakini bado mbona mauaji yanatokea, mwili ulinisismka sana nilijikuta nashindwa kuendelea kuisoma ile habari nakuludi na kukaa kwenye kochi lililokuwa mule kwenye chumba change na kuanza kufikiria ni kipi cha kufanya, baada ya kuwaza kwa muda kidogo niliona ngoja nijikaze kiume nilitoa kijitabu change kidogo ambacho kilikuwa kimejaa namba za watu mbalimbali kisha nikaangalia namba ya Gerald na kuamua kumpigia, simu iliita sana bila hata ya kupokelewa mpaka nikajikuta nakata tama ya kwamba labda atakuwa yupo msibani na yupo kwenye taratibu za mazishi, niliacha kuipiga ile namba na kuamia namba ya Amina nayo iliita pia bila kupokelewa nahisi wote waliogopa kuipokea baada ya kuona ni namba ngeni halafu ilikuwa sio namba ya ndani ya nchi basi nilijikuta nakaa tu bila ya kujua ni lipi la kufanya kwani watu wote niliokuwa nawategema kupata habari kutoka kwao ndio hivyo tena simu walikuwa hawpokei tena basi wakati najiandaa kutoka mule chumbani niludi kule bandarini ili kwenda kuangalia kama ile meli itakuwa tayari imeshawasili, mara simu ya mule chumbani kwangu ndipi ilipoanza kuita kwanza nilihisi labda watakuwa ni wale wahudumu wa mule labda kuna jambo wanataka kuniambia au kulikuwa na mtu yoyote alikuwa ananitafuta,lakini baada ya kuipokea ile namba mambo yalikuwa ndivyo sivyo kwani yule aliyekuwa amepiga simu alianza kwa kucheka sana tena kwa kicheko cha dharau sana,nilikuta nashituka kwani sauti nilihisi kama naijua ila ni sauti amabyo nilikuwa sijaisika muda mrefu sana, ile sauti y kike iliniambia ya kwamba nilikuwa najifanya mjanja wakati mimi ni mpumbavu sana, kuwa alinitega ili niondoke nchini ili yeye huku aendeleze mipango yake, aliniambia kuwa na Gerald alikuwa tayri ameshamteka anasubili siku yoyte aamue amfanye lolote, mwili ulisisimka na mapigo ya moyo yalianza kwenda kasi sana, kwani nilijua kwamba pale pia nilikuwa nimuzwa na yule mwanamke, niliikata simu kwa hasira kisha na kuangalia ile namba iliyokuwa imetumika kupiga nilikuta ni namba ya Gerald, nilizidi kuishiwa nguvu kwani nilijua ni kweli basi Gerald atakuwa ametekwa nayule mwanamke, nilijiona kama ni mpelelezi niliyekuwa situmii akili kwa kuuzwa kijinga kule Tanga mpaka nikakurupuka na kufunga safari mpaka kule visiwani huku mtuhumiwa nikiwa nimemuacha nchini, nilijjishangaaa sana lakini nikaona sio mbaya lazima nihakikisha nafanya uchunguzi kwanza kwenye ile meli nikisha jihkikisha ndipo niweze ondoka kule shelisheli.
Nilifika pale bandarini na kukuta meli ile ikiwa imeshafika huku wakisema ya kwamba itaanza kupakuwa mzigo kesho yake basi nilikaa sehemu na kuvizia kuona wafanyakzi wa ile meli pindi watakapopita basi mmoja wao nimuite niweze kuzungumza nae maneno mawili matatu. Nilijua ningeweza kupata kitu basi baada ya kukata tama kama baada ya saa zima ndipo nilipoona watu nilijua kabisa walikuwa wafanyakazi wa ile meli nilimuona mmoja ambaye alikuwa na rangi ya kiafrika zaidi tofauti na wale wengine ambao rangi zao zilikuwa ni mchanganyiko, alikuwa amevalia overolly la rangi ya blue huku akiwa ameshika begi lake la nguo mkononi, baaada ya kumuita kwanza alisita kisha ila nahisi baada yak union kwamba mimi ni mwafika mwenzake alikuja bila wasiwasi huku akiona kama mtu aliyekuwa na haraka sana, nilimsalimu kiingereza, alinijibu huku akiniuliza mimi ni mtu wa wapi nilijitambulisha kwamba ni mtanzania ambaye nilikuwa nipo mule visiwani kwenye utalii, alinichangamkia sana baada ya kusika hivyo aliniambia kwamba yeye alikuwa ni mmadagaska ila kutokana na kazi yake ya ubaharia ilimuwezesha kwenda sehemu mbalimbali ndani ya Afrika tulianza kuondoka naye yae maeneo huku tukuwa tunazugumza taratibu, aliniambia ya kwamba yeye kazunguka nchi nyingi lakini Tanzania ni wakarimu sana kuwa walikuwa Tanzania siku nne zilizopita, nilizidi kufurahi baada ya kuona mimi na yeye tumeanza kuelewana vile kwani ingenirahisishia mimi shughuri yangu ya kujua yule mwanamke ilikuwaje mpaka akapanda kwenye ile meli na yuppo wapi kwani kwa muda wote niokuwa pale langoni ikuweza kumuona akishuka pia nakumbuka alinipigia simu kupitia namba ya Gerald ya kwamba alikuwa ameniuza mimi niondoke ili yeye aweze kutimiza mipango yake mingine, yule kaka maybe baadaye nilikuja kugundua kwamba alikuwa naitwa Frednando aliendela kunuambia kuwa pamoja nayote ila wanawake wa Tanzania walikuwa wajanja sana, nilihisi kama aliuwa anataka kuja kwenye mada niliyokuwa naitaka,  “kwa nini?” nilijikuta namuuliza haraka haraka sana, kuna mwanmake mmoja rafiki yangu alimpata Tanga juzi lakini walipofika Mombasa yule mwanamke aliwatoroka bila ya wao kujua huku akiwa amebeba kiasi kikubwa sana cha pesa kutoka kwenye ile meli. Ambazo zilikuwa za nahodha nilijifanya nasononeka kisha nikamuuliza kwani alimjuaje? Aliniambia  ya kwamba yule mwanamke walikuta naye chichi club walipoenda siku moja kabla hawajondoka,huku akinimabia ya kwamba wakati anatoroka alidondosha pochi yake ambayo walifanikwa kukuta baadhi ya vitu vyake, nilimuuliza ni wapi tunaweza kuupaa hoa mzigo, alinitazama kisha akawa kama anajaribu kunijibu kwa lugha ya Kiswahili lakini kilionekana kumshinda kabisa,kisha ndipo akaniambia tu kwa lugha ya kiingereza kwamba vipi umetumwa au kakupigia simu ulifuatilie nini? Nilicheka kinafiki ili kupoteza lengo kwani yule kaka alianza kuinyesha kama kuchoka hivyo basi nikaona kama nisipokuwa mjanja basi sitojua lile begi lipo wapi, alinimbia ya kwamba hana uhakika ila anahisi litakuwa tu mule kwenye meli, kwani lilikuwa na vitu vya kike kike tu, tuliendelea kuzungumza mpaka tukafika barabarani ambapo yeye alipanda taxi na kuelekea hoteli ambayo ndio huwa wanafikia, nilipia hesabu ni vipi nitaweza kuingia kwenye ile meli bila ya kuonkena, basi pale pale wazo likanijia namimi nikakodi taxi na kuingia mjini kwenye maduka.
Jioni ile nilivaa overlloy la blue na viatu vigumu chini nikawa kama vile mmoja wa mabaharia nilifika getini pale bandarini na kujifanya kama na mimi nilikuwa baharia wa ile meli huku nikijifanya ya kwamba nimesahau ndani baadhi ya vitu vyangu ikiwemo hati yangu walinitazama kisha yule dada niliyemkuta mchana akanitazama kama vile alikuwa anafananisha kitu hivi, aliniuliza jina nikamtajia la yule jamaa yangu niliyekuana naye pale, walilitazama kwenye daftari la mabaharia walioshuka kisha akaniruhusu, sikuamini kwani mapigo ya moyo yalikuwa yakinienda kasi sana, niliondoka pale getini kwa kasi ya ajabu sana huku nikiwa naogopa hata kuangalia nyumna,niliingia kwenye ilemeli ambapo nilikuta shughuri ya upakiaji ikiwa bado inaendelea,wale wapakuaji hawakuwa na muda hata na mimi nilisogea mpaka kwenye mlango wa kuelekea kwenye chumba cha nahodha nilijaribisha kuufungua nikakuta upo wazi, basi nikaingia  huku nikitazama kila upande kama naonekana nilianza kufanya upekuzi haraka haraka sana mara kwenye kabati kwa juu nikaona mkoba mweusi wa kike basi nikajihakikishia kuwa ndio wenyewe niliuchukua na kuanza kuuweka kwenye mfuko mweusi niliokuwa nimeingia nao. Wakati namalizia kuuweka mara nikasikia vishindo na sauti ya watu wakielekea mule kwenye kile chumba nilichukuwamo..
Mapigo ya moyo yalianza kunienda mbio sana wale watu walizidi kusogea kwenye kile cumba huku wakiwa wanazungumza kifaransa, niliinuka na kuanza lutafuta mahali pa kujificha kwani niljua kama walikuwa ni baadhi ya wale ma baharia wangenitambua kuwa sio mwenzao hivyo ningekuwa matatani sana, nililisogeza kabati mule chumbani na kupenya kwa chini ambapo palikuwa na uvungu mkubwa tu kiasi kwamba kama wangeingia isingekuwa rahisi kwa wao kuniona, nilikaa mule kwa takiribani zaidi ya dakika kumi na tan bila ya mtu kuingia huku zile sauti zikionekana zikizidi kupotelezea, nilishusha pumzi kisha nikatoka mule uvunguni na kuanza kuangalia njia sasa ya kutoka nje kwani muda ulkuwa umeenda sana.
                                         **************************
Baada ya kuingia chumbani kwangu pale hotelini cha kwanza kabisa nilikuwa na hamu ya kujua je ni kipi kilichokuwepo ndani ya lile begi. Nililifungua lile begi na kukuta kuna vitu vya kike  tu kama nguo za ndani, marashi, sabuni, na mapambo mengine, roho iliniuma sana kwani nilijiona kama nimepoteza muda wangu na kujiweka hatarini bila ya sababu ya maana, nililitupa lile begi chini kwa hasira sana, nililipo anguka chini ndipo nikaona kama kuna vitu vikitoka kwenye zipu ya pembeni, basi nililiinua haraka tena lile begi kisha na kuanza klikagua tena kumbe lilikuwa na zipu ya pembeni niliifungua haraka haraka sana, nilikutana na kijiabu kikiwa na namba mbalimbali za simu baada ya kuanza kuzipia moja baada ya nyingine nilikuta namba karibia za wafanyakazi wote wa pale ofisini zikiwepo, nilishituka sana baada ya kuona hivyo, niliendelea kufunua kile kjitabu nikakutana na sehemu ambapo alikuwa ameandika kumbukumbu zake mbali mbali kila jambo na tukio nilishangaa sana baada yakukuta karibia kila tukio alilokuwa akifanya likiwa lipo kwenye kile kijitabu, mpaka tukio la mwisho ambalo lilikuwa ni kuonana na mimi kule Tanga, niliendelea kukikagua kile kitabu mwisho nilikuta na majina ya watu mbalimbali ambao walikuwa kwenyempango wake wa kuwaondoa duniani ambapo kulikuwa na mlolongo waa majina mbalimbali,nilishangaa baada ya kukta pia jina la marehemu bosi wangu huku jina la mwisho likiwa ni mkuu msaidizi wa idara ya mafunzo katika chuo cha mafunzo ya upolisi, mwili ulinisisimka sana kwani kwani kile kitabu kilikuwa kinaelezea kila mtu na sehemu anayoishi, vitu anavyopendelea na jinsi ya kumuondoa duniani, nilijikuta nashindwa kuendelea kukisoma kile kitabu na kukiweka pembeni kwani kilikuwa siri nyingi sana za yule mwanamke,
Niliendelea na kukagua kwenye ile zipu ya pembeni ambapo pia nilikutana na  nailony eyes za bandia pamoja na sura tatu za bandia, nilikuta na hati ya kusafiria ikimuonyesha kama ni raia wa shelisheli huku pia kukiwa na funguo ambazo zilionyesha kwamba zilikuwa za nyumba yake kwani kwenye key holder yake zilikuwa zinaonyesha kila ufunguo na mlango wake, nilijikuta nafurahi huku nikijua sasa kumbe ile safari yangu haikuwa ya bure kabisa nikajikuta sasa naanza kuvipanga vile vitu vizuri huku nikiviamisha kutoka kwenye begi lake kwenda kwenye begi langu vile nilivyohisi ni vya maana.
Nilimaliza na kuanza kulikung’uta lile begi Wakati naendelea na lile zoezi mara nikasikia kitu  kigumu kikianguka chini baada ya kukiangalia vizuri ilikuwa ni simu ya mkononi huku ikiwa imeviringishwa na pedi kiasi kwamba isingekuwa rahisi kuonekana, niliichukua ile simu  aina ya htc na kujaribisha kuiwasha lakini lionekana kutokuwa na chaji, nikaona sio mbaya nitatafuta chahi yake niichaji iliniweze kujua ni kipi kimehifadhiwa mule ndani, mpaka pale nilikuwa na matumani sana ya kuweza kumtambua yule mwanamke kutokana na vile baadhi ya vitu nilivyoweza kuvipata siku ilea ma kweli mtembea bure si sawa na mkaa bure.
                                           **********************************
Nilifika Dar es salaam salama kabisa nilitoka mule uwanja wa ndege mpaka barabarani kisha nikapanda zangu daladala kama vile nilikuwa ni mtu niliyekuwa katika mihangaiko yangu ya kila siku nilishuka mnazi mmoja kisha na kuelekea nyumbani kwangu, ambapo nilikuta papo kama ilivyokuwa nimepaacha tofauti na mwanzo nilivyokuwa nimefikiria kwamba nitakuta pamekaguliwa ila haikuwa hivyo basi jambo kwanza niliwasha simu zangu na kangalia ni nani walikuwa wamenitafuta kwa kipindi kile chote ambacho sikuwepo, uliingia ujumbe wa meseji  mbalimbali huku pia na namba za simu ambazo zilionekana kunitafuta kwa ule muda ambao sikuwepo, nilijaribu kuzipia nyingi zileonyesha tu zilikuwa zikinijulisha kuhusu msiba wa mkuu wetu wa kazi, sikuzijali sana kwani kama taarifa nilikuwa tayari naijua hivyo basi sikuona kama ni kitu kigeni sana.
Baada ya kumaliza kuosha mwili wangu naa kubadili nguo basi moja kwa moja nilitoka nje nikaingia mitaa ya nyuma ili nijirabu kutafuta chaji ya ile simu ili niweze kujua kulikuwa na nini niliingia maduka ya simu ya kariakoo muda ule ule wa jioni kwani navyojua mara nyingi yale maduka huwa ikifika jiona mara zote vitu huwa vinashuka bei kwani kuwa mwingine unakuta hajauza siku nzima hivyo hawezi kukataa pesa, basi baada ya kupita pita kwenye yale maduka mengi hayakuwa na chaji ya ile simu mpaka mwisho kabisa nilienda kuipata kwenye duka moja ambalo lilikuwa kwenye uchochoro mmoja uliokuwa ukitokea  mtaa wa Swahili nipo nilikuta mhindi mmoja akiwa nayo basi sikutaka sana kubishana nae sana kwenye bei nilimpatia pesa yake kisha nikaondoka zangu haraka sana kuludi nyumani kwani sikutaka nionekane sana kwani nilihofia kukutana na mtu yoyote ambaye nilikuwa namjua, basi baada yakuichaji ile simu na kuiwasha nikakkuta na password, nilijua tu yule mwanamke atakuwa amefanya vile ili isiwe rahisi watu kujua  je ni kipi kilikuwapo mule ndani, basi nika download programmer ya kiuwa ile password kwenye computer yangu ili niweze kujua mule ndani kulikuwa kuna nini niliiwasha kwa shauku kubwa sana ya kutaka kujua kilichokuwepo mule ndani, moja kwa moja niliaanza nu sehemu ya ujumbe mfupi ambapo pale sikuweza kukutana kitu chochote cha maana,sikupajali,nikaingia kwenye faili liliokuwa na picha na video, pale niliweza kukutana na picha za matukio mbali mbali pia niliweza kuuta baadhi ya picha za msichana mmoja akiwa amepiga kwenye nyumba moja hivi basi nilihisi moja kwa moja atakuwa ni yeye, niliachana na mahali pa picha nikijua kwa zile nilizokuwa nimeziona zinatosha kuweka kumtambua basi nikaamua kuhamia kwenye upande wa barua pepe kwenye ile simu yake, wakati nanaendelea na ile shughuli mara mlango wangu nikasikia ukigongwa kwa nguvu sana niliamka taraibu na kwenda kufuungua, mwili ulinyon’gonyea nilipokutana na baadhi ya wafanyakazi wenzangu wakiniambia ya kwamba nilikuwa natafutwa sana naitajika makao makuu kwa ajili ya mahojiano.
                       ****************************************
Niliguna baada ya kusikia vile nilijua moja kwa  moja nilikuwa nahisiwa kuhusika na kifo cha mkubwa wangu wa kazi,niliwaomba dakika kadhaa niweze kujiandaa kwani nilikuwa nipo kifua wazi huku nikiwa nimevaa suruali ya kulalia tu, waliniambia hukuna tatizo, nilijua ingekuwa ngumu kwa mimi kunipeleka kama watu wengine kwani baadhi yao pale nilikuwa nawazidi cheo ofisini, basi niingia ndani na kujiandaa kisha nikabeba na baadhi ya vitu kwenye mkoba wangu na kutoka kwa ajiliya kuanza safari ya kuelekea makao makuu muda ule ule wa jioni kwa ajili ya mahojiano kama wao walivyokuwa wamenambia, niliinia kwenye ile discover ya polisi na kuanza kuelekea makao makuu.mule ndani ya gari wale wafanyakazi wenzangu walionekana kama ni watu waliokuwa wakinihofia sana kwani hata mazungumzo na mimi walkuwa wanazungumza kwa kusita sit asana hasa baadhi ya maswali ambayo nilikuwa nahitako ufafanuzi wao na ushirikiano wao. Nilijua tu itakuwa ni sumu iliyokuwa imesabazwa kuwa mimi nilikuwa nikishirikiana na yule muuaji katika kufanya yale matukio,kitu ambacho mimi kilinishangaza sana kwani sikuona ushirikiano baina ya mimi na yule mwanamkepia sikuona umuhimu wake ule wa kuuwa watu hovyo basi sikuwa na jinsi nianza kujiona kama mpweke Fulani hivi na mtu ambaye nilikuwa ninategwa na jamii bila ya sababu zisizo na maana, sikuwa na jinsi niona njia ya kulitatua lile tatizo ni moj tu nalo ni kuhakikisha yule mwanamke namkamata na kumfiksiha mbele yao hiyo ndio itakuwa njia yangu mimi kujosha kwani tofauti na pale bado jamii na wafanyakazi wenzangu watahisi ni mimi.
Tulifika pale makao makuu ya iwzara ya mambo ya ndani, tulipanda moja kwa moja mpaka gorofa ya pili ambapo ndipo zilipokuwa ofisi za jeshi la polisi, baada kuingia mule ndani nilikutana na kamishina mkuu wa jehi la polishi idara ya upelelezi, akiwa yupo pamoja na wasaidizi wake watatu, alionekana kama mtu aliyekuwa na hasira sana ilyochanganyikana na hudhuni Fulani, nilihisi itakuwa sababu ya kifo cha yule mkuu wangu wa kazi kwani alikuwa ni rafiki yake sana hata pia ile nafasi ni yeye ndio aliyempatia kutokana na na kujuana kwao nilisika pia hata depo waliingia pamoja,nilkaa kwenye kiti pale mbele kisha wale wafanyakazi walionipeleka wao walitoka nje na kuniacha mule ndani nikiwa pamoja na wale ma ofisa wa pale makao makuuu, kamishina alinitazama kama dakika tano hvi bila ya kusema neon lolote huku machozi yakionekana kama yalikuwa yanamrenga renga, na mimi skitaka kuzungumza kitu kwanza niliendelea kusubli mpaka pale wao wenyewe watakapoamua kuanza mazungumzo, mara yule msaidizi wake akamwambia “mkuu tumuhoji basi haraka haraka ili tujue ni kipi cha kuendelea nacho” kamishina alionekana kama vile kushituka kama ni mtu aliyekuwa akiwaza mbali sana ndipo alipoanza kuniuliza maswali mbali mbali kuhsu yule mwanamke namjua vipi nahusika vipi kwa nini wenzangu wanishitumu kwamba namjua na nashirikiana nae katika kumpa habari, roho iliniuma sana baada ya kusikia kauli eti wenzangu wananishutumu.sikuamini kusikia vile, nilikaa kimua wakazungumza mule kwa takiribani dakika kumi na tano kisha na mimi ndipo nikafungua mdomo wangu kuanza kuwajibu, nilimueleza kila kitu ya kwamba yule mwanamke alikuwa ni mtu makini sana tofauti na sisi tulivyokuwa tunafikria, walitega sikio kwa makini kusikia kipi nilichokuwa nazungumza niliendelea kuwapasha ya kwamba mimi  naona kama nilikuwa tu nimetolewa kafara na mkuu wangu hasa baada ya kuona kazi inakuwa ngumu au kwa sababu matukio mengi yaliyokuwa yakimuhusu yule mwanamke nilikuwa nakutana nayo mimi au nahusika nayo,alinitazama usoni akionekana kabisa kuna kitu alikuwa akikisoma usoni kwangu kisha akaniambia ya kwamba na je ninajua vipi kuhusu kifo cha merehemu inspekta Thomas, nilimwambia kwa kweli mimi taarifa nilikuwa nazo lakini sikuwa najua lolote kuhusu kile kifo, alinitazama yena kisha hapo hapo akanipandishia swali jingine, je kwa nini nilikuwa sipatikani kwenye simu na kwenye msiba sikuwepo pia hata kwangu sikuwepo kama taarifa nilikuwa nazo, ilinibidi niwaeleze ukweli wote kwani nilijua kwamba bila vile wangeendelea kuwa na imani na mimi, niliwaeleza kila kitu kutoke siku ile nilipoambiwa ya kwamba nimesimamishwa kazi mpaka safari yangu ya Tanga na mwisho ile safari yangu ya visiwa vya shelisheli, niliwaeleza ya kuwa japo nilikuwa nimesimamishwa kazi lakini mimi kama ninilikuwa bado naendelea na ile kazi mwenyewe,walionekana kama vile walikuwa hawaniamini,basi kama nilikuwa najua nilitoa tiketi ya ndege kutoka kwenye moja ya bahasha niliyokuwa nimetoka nayo nyumbani pamoja na na risiti za hoteli kule  visiwa vya sheli sheli walionkena kuanza kujenga imani tena na mimi. Basi baada ya yale mazungumzo yule kamishina mkuu aliniambia ya kwamba sasa itanibidi mimi niendelee na ule upelelezi bila ya kumjulisha mtu yoyote hasa wale niokuwa nafanya nao kazi kisha niwe nalipoti kwake, aliniambia ya kwamba taarifa alizokuwa nazo ni kuwa Jamila analudi kesho hivyo basi nayeye atamuunganisha na mimi kufanya ile kazi bila ya kuingiliana na na akina Amina, nilimshukuru sana kwa kuonyesha ule uelwewa, basi pale pale nilitoa baadhi ya vifaa ambavyo nilkuwa nimevipta ambavyo nilivihisisha moja kwa moja na yule mwanamke, walivitazama sana, kisha nikamuona kamisjina akiguna baada ya kuona kile kitabu kilichokuwa na namba za simu “mh mbona huu mwandiko kama vile naujua” alizungumza alijaribu kuvuta kumbukumbu pale bila ya kukumbuka ila akendelea kusisitiza ya kwamba ule mwandiko anauhakika kabisa alikuwa anaujua, alishangaa sana baada ya kukutana na plani za watu waliokuwa kwenye malengo ya yule mwanamke walizidi kuhoka sana, ndipo mkuu akaanza kunisisitiza tena nijitahidi basi asije leta madhara zaidi ya pale kwani mpaka pale ilikuwa ni doa kubwa sana kwenye jeshi la polisi, nilimwambia hakuna shida ile kazi hata mimi nimedhamiria kuifanya kwa nguvu zote li kuondoa ile dhana iliyokuwa imejengeka kwa wafanyakazi wenzangu.basi tulimaliza yale mazungumo huku mkuu wangu akinihakikishia kunipa msaada wowote ule ambao ningeutaka lakini ahakikishe tu kina Amina wasijue kama na mimi nilikuwa nafuatilia ile kesi, pia walinishukuru sana kwa ule moyo wangu niliouonyesha mpaka kutumia gharama zangu binafsi kwenye mpaka visiwa vya sheli sheli kwenda kumfuatilia yule mwanamke.
                                ********************************
Baada ya kumaliza kujihakikishia upekuzi tena wa ile simu ya yule mwanamke nilielekea asubuhi na mapema kwenye ofisi za tume ya mawasiliano ambapo nilikutana tena na afisa huyu akiwa ni mwingine kabisa ambaye alikuwa ni kijana mdogo sana akionyesha kama ni mtu aliyekuwa ametoka masomoni sio muda mrefu sana, nilizungumza naye pale kisha nikatoa kitambulisho changu ambapo baada ya kukiona ndipo nikaanza kumuelezea  sababu za mimi kuwa pale ofisini kwake asubuhi yote ile  alinisikiliza kwa makini kisha akachuka ile namba ya simu ya yule mwanamke na kuiingiza kwenye laptop yake ambapo aliangalia location ambapo ile namba ilikuwa inasoma mara kwa mara ilionekana ilikuwa inasoma mitaa ya kimara, alizidi kupekuwa mpaka umbali wa mahali ilipokuwa inasoma ile namba kutokea kwenye mnara wa simu, baada ya pale aliiprinti karatasi ikionyesha umbali wa mahali ambapo ule mnara ulikuwa ukisoma alinikabidhi huku akinijulisha kwamba kama kukiwa na shida nyingine basi nisisite kumfuata tena,nilipokea ile karatasi na kumshukuru kisha nikatoka nje na kuanza safari ya kuelekea pale kimara baruti ambapo ndipo mahali ile namba ilikuwa ikisoma.
                            ******************************
Nilifika kimara na kisha kuelekea kule mahali nilipokuwa nahitaji kufika kwa ajili ya kuliona lile eneo nilitembea zaidi ya nusu saaa bila ya kuona ile ramani ambayo nilkuwa nayo mpaka ikanibidi niwauliza baadhi ya watu njiani ambao baada ya kunielekeza ndipo nikaendelea na safari yangu nilifika mpaka wenye ule mnara uliokuwepo kwenye ramani kisha nikatoa tena ramani yangu na kuanza kuangalia mwelekeo tena, niliiweza kuifuata mpaka nikafika kwenye ile nyumba kwani haikuwa mbali sana na ule mnara.
Nyumba yenyewe ilikuwa imejitenga kidogo huku ikionyesha dhahiri ya kwamba haikuwa na muda mrefu tokea imalizike ujenzi wake, basi nilijaribu kugonga moja kwa moja pale mlangoni kwani uzio wake haukuwa umekamilika vizuri hivyo hata geti ulikuwa bado haujawekewa, niligonga sana bila hata ya kupata majibu mwisho nikaelekea nyumba ya jirani ili niweze japo kupata habari mbili tatu kuhusu mkazi wa ile nyumba,niliweza kukutana na mlinzi mmoja wa kimasai wa ile nyumba ya jirani baada ya kumsalimia ndipo nilipoanza kumuulizia kwanza alikuwa anaonyesha tabu kujibu mara, hamjui mara yeye sio mlinzi wa iyo nyumba hivyo hajui kitu chochote lakini baada ya kumbembeleza sana huku nikimdanganya ya kwamba nilikuwa nimeambiwa ya kwamba dada yangu alikuwa ndio anakaa pale mimi ni mgeni nimetoka Morogoro nina mud asana nilkuwa sijafika dar hivyo basi baada ya kufika na kuulizia ndipo nilipoambiwa ya kwamba alikuwa amehamia kwenye nyumba ile, yule mmasai alinitazama kisha akaniambia ya kwamba, siku hizi hakuna cha bure nimpe hata pesa ya soda ndipo aweze kuniambia.
Sikuonyesha kusit kwani kwangu jambo muhimu lilikuwa ni kupata habari tu basi nilitoa shilingi elfu tano na kumpa, alishangaa sana kwani alijua labda nitampa elfu moja au mbili, basi hakuamin baada ya kumwambi ya kwamba achukue yote, aliifunga kwenye kona moja ya shuka lake la kimasai kisha ndipo akaanza kuniambia habari za kuhusu yule mwanamke alisema ya kwamba yeye hakuwa anamjua sana kwani huwa anaingia usiku au jioni huku akiwa na gari au piki piki na mara nyingi huwa anavaa anajifunika sana kiasi kwamba inakuwa vigumu sana kumuona, nilimuuliza mara ya mwisho kumuona ilikuwa ni lini aalinijibu ya kwamba kama siku tatu zilizopita na sio kawaida yake kwani mara nyingi huwa anapita kila siku,. Basi nilivuta pumzi na kisha kumuuliza kama akimuona kwa sura atamkumbuka, aalisita kisha akasema, sizani kwa maana ni mtu ambaye huwa anapita ahuk akiwa na haraka haraka sana nilimuuliza pia kama huwa kuna wageni wanakuja kumtembelea alisema toka yule mwanamke aanze kukaa ile nyumba hajawahi kuona mtu yoyote yani mimi ndio nilikuwa mtu wa kwanza kja na kumuulizia kwani inaonekana yule mwanamke huwa anakuwa yupo bize sana, basi nilimshkuru kisha nikaanza kuondoka, basi yule mmasai akaniuliza sasa kama akija nimuambie nani kaja, nilisimama kisha nikamsogelea na kuanza kumwambia kwa sauti ya taratibu ya kwamba asimwambie lolote kisha nikampa namba yangu na kumwambiaya kwamba wewe ukimuona amekuja wewe nibeep mimi  nitakuja pia kutakuwa na zawadi yako nono,yule mmasai alionekana kufurahi sana kusikia kuwa nitampa zawadi. “sasa mtu mwenyewe huwa akija hakai sana unaweza kuja na usimkute” alinimabia yule mmasai basi na mimi nikamjulisha ya kwamba asiwe na wasiwasi kwani mimi nilikuwa naishi mazingira yale yale jirani hivyo hofu aondoe kabisa.
                                ***********************************
Nilifika uwanja wa ndege mida ya asubuhi na mapema kwa ajil ya kwenda kumpokea Jamila ambaye alikuwa mafunzoni nje ya nchi huku akiwa ameenda kujifunza kozi fupi ya mambo ya social intelligence  nilipaki gari yangu sehemu ya kuegeshea magari kisha nikaenda moja kwa moja sehemu ya kusubilia wageni,nilikuwa nimewahi kama muda wa dakika arobaini hivi kabla ya muda wa ile ndege ya KLM kufika, basi baada ya muda ile ndege ilifika namimi nilijiamisha na kuhamia sehemu ya kutokea abiria, baada ya dakika tano nilimuona Jamila  akiteremka huku akiwa ameshika begi lake dogo akiliburuta na mkoba wake mingine ukiwa kwapani, basi nilimsogelea na kumkumbatia huku nay eye akionyesha tabasamu pana kidogo kisha tukasalimiana pale, Jamila alionekana kufurahia sana mimi muda ule wa asubuhi yote kuwa pale kwa ajili ya kumpokea, aliongea kwa utani,ulilala ukinota nini?  Basi tulipanda kwenye gari yangu na kuanza safari ya kuelekea nyumbani kwake alikokuwa amepanga alikuwa amepanga magomeni. Ndani ya gari tulizungumza  mambo mengi sana huku mimi nikimwambia afadhali ameludi kwani mwanamke mwenye kovu jeusi bado anaendelea kusumbua jiji, alinitazama kwa macho ya hudhuni Fulani huku akionekana kama ni mtu aliyehisi kitu Fulani kisha akaniambia, inamaana mmeshindwa kumdhibiti , nimitamzama kisha nikamwambia ya kwamba pale tulikuwa tukimsubili yeye nay eye pia ajalibu kumkamata kama ile kazi likuwa ni rahisi, nilimwambi kwani barua zangu pepe ulikuwa huzipati? Hali imekuwa mbaya sana juzi nilikuwa makao makuu waliniambia ya kwamba wewe ukifika tu utajumuika na mimi katika kufuatilia hili jambo kwa siri bila ya kuingiliana na kina Amina, aliguna kisha akajikuta anasema ya kwamba hapana katika hili jambo mimi mtanitaka radhi kabisa sitoweza kuifuatlia bora nipewe majukumu mengine, nilimmwambia kwa upole sasa Jamila hiyo kozi uliyokuwa umeenda kuisoma huko Marekani imekusaidia nini wakati mkuu wetu ameona ya kwamba wewe ndio utafaa zaidi halafu pia wewe huwa unakuwa shapu sana katika ufanyaji kazi ndio maana wamependekeza uifanye na mimi. Jamila alionekana kuafiki kwa shingo upande kuhusu kushirikiana na mimi katika lile jambo,
 basi tulifika kwake ambapo aliniacha mimi sebuleni kwake kisha yeye akaelekea chmbani kwake kwa ajili ya kujiandaa.
                               **************************
Ilikuwa ni mida ya saa mbili usiku wakati nipo zangu nyumbani kwangu nikitazama taarifa ya habari ndipo simu yangu ilipogiwa na namba ngeni, nilipopoke ile simu ikakata, basi nikaamua kuipigia ile namba mara akapokea kumbe alikuwa ni yule mmasai, “thatha yelo ulisema wewe nikikudeep utapiga thatha mona wapokea mpaka pesa yangu waimaliza yelo” alikuwa yule mmasai akilalamika baada ya mimi kupokea ile simu yangu. Nilimwambia asijali nitamtumia salio baada ya hapo kisha nikamwambia anijuze, ah nilikuwa nataka kukusalimu tu halafu huyu jirani ameingia muda huu basi fanya kuwahi kuja. Nilishituka kusikia vile halafu pia nlijiuliza ni vipi nitawahi kufika kule kwa maana kutoka mnazi mmoja mpaka kimara na kwa muda ule foleni ilikuwa ni kubwa sana.basi nilimjulisha ya kwamba hakuna shida nakuja, sawa usisahau zawadi yandu na vocha yangu, alimalizia yule mmasai.
Nilimpigia simu Jamila ili kumjulisha ajiandae nimpitie kwani kazi tayari ailikuwa imeshaanza kwa bahati mbaya simu yake ikawa haipatikani,nililaumu sana kwa kile kitendo kwani wakati naondoka kwake nilimwambia kuwa muda wowote ningeweza kumuhitaji kwa ajili ya ile kazi,basi nilijipakia mimi mwenyewe kwenye gari yangu huku nikiwa nimechukua bastola yangu moja
                            *******************************
Niliondoa gari pale kwangu kwa mwendo wa kasi sana huku nikijaribu kutanua sehemu zingine ili niweze kufika mapema, japo njiani kulikuwa na foleni kubwa sana lakini baada ya saa moja na robo nilkiuwatayari nimeshafika tayari maeneo ya jirani na ile nyumba nilipaki gari yangu umbali wa kama mita mia tano hivi kisha nikashuka na kisha kuanza kuelekea kwenye ile nyumba, nilisogea mpaka kwa nyuma ya ile nyumba kisha nikaangalia kama kulikuwa na upenyo wa kupita kuingia mule ndani, sikuona geti kwani nyumba ilikuwa imezungushiwa ukuta kwa kule nyuma na ulikuwa ni mrefu sana,nilihangaika nikaona kama nikifanya shambulizi la kushitkiza na kuingia mule ndani basi nitakuwa najiweka hatiani kwani yule mwanamke angewza kunisikia na kunidhuru kwa lolote lile ilinbidi nigahili kisha nihamie upande wa mbele wa ile nyumba nilipanda juu ya mti na kujibanza sehemu moja hivi ambapo palikuwa na kama tawi Fulani lililojaa majani mengi hivi, kupitia pale niliweza kuona kwa mbali mule ndani taa ikiwa imewaka huku yule mwanamke akionekana akizunguka mara huku mare kue mule ndani, nilijilaumu sana kwa kwenda peka yangu niliogopa yasije nikuta kama yale ya makaburini,nilijaribu kumpigia simu Jmila lakini ikawa haipatikani
Basi niliona njia pekee pale ni kwenda tu moja kwa moja getini na kugonga kisha kuludi na kujifisha ili niweze kuon ni kipi kitanedelea, nilishuka chini ya mti na kwenda kugonga lile geti kwa nguvu sana kisha nkaludi kujificha kama nilivyokuwa nimepanga,yule mwanamke alionekana kushituka mule ndani, nadhani alijua tu ni raia wa kawaida basi akaja mpaka pale getini na kuchungulia hakuweza kuona mtu kisha akajirudisha ndani nahisi aifikiria watakuwa ni watoto tu wakifanya fujo, mwili ulinisisimka sana kwani ile sura ilikuwa sio ngeni kabisa machoni mwangu, nilihisi kama naifananisha sijui kutokana na lile giza,basi nikaona sio mbaya ngoja kwanza niendelee kuwa mvumilivu ili niweze kujua ni kipi kitaendelea.mara baada ya kama nusu sasa nikaweza kumuona yule mwanamke akitoka mule ndani ilikuwa yapata kama mida ya saa sita usiku hivi kuangalia vizuri ile sura ilikuwa ni sura ya Jamila, nilishituka sana nikataka kumuita kisha nikasita alitoka mule ndani kwa kasi ana huku akiwa kama mtu aliyekuwana wasiwasi, baada ya kuondoka lile eneo, na mimi nilishuka juu ya ule mti na kuanza kuelekeakwenye gari langu kuanza safari ya kuludi kwangu, huku kichwani nikiwa na maswali mwengi kichwani je Jamila ndio yule mwanamke? Au baada ya kufika tu ameamua kuanza nay eye kumfuatilia kimya kimya yule mwanamke? Nilijikuta najihoji maswali mengi sana bila ya majibu, maana kila siku niliona jambo jipya likizuka kila siku, nilondoka pale huku nikiona njia nzuri ni kumtega tu Jamila ili kujua kila kitu kama ni yeye ndio muhusika au na yeye ndio alikuwa anafuatilia.nilijikuta nakosa jibu la uhakika zaidi pindi nitakapokutana naye ndio niliona naweza pata jibu.
                           ***************************************
Nilikutana na Jamila baada ya kumaliza mihangaiko yake ya mchana alikuja nyumbani kwangu ambapo alinikuta nikiwa bado nimelala sikuwa na haraka ya kuamka kwani kazini nilikuwa siendi hivyo muda mwingi nilikuwa nautumia tu kulala kama sina kazi nyingine ya kufanya.
Basi baada ya kuingia ndani kwangu alipitiliza mpaka chumbani kwangu, aliniomba ruhusa ya kukaa kwenye  kitanda changu ambapo na mimi bila ya hiyana nilimruhusu. Tulianza kuzungumza mambo mengi sana huku akinipa habari za hapa na pale,nilimuuliza kwa nini jana yake alizima simu usiku wakati nilikuwa namhitaji twende kumfuatilia mwanamke yule hatari alinijibu huku akiangalia pembeni yakwamba alikuwa amechoka sana hivyo basi ndio maana aliamua kuzima simu yake baada ya muda kumaliza kupata chakula cha mchana nilienda bafuni kuoga, wakati naludi nilimkuta Jamila akiwa kama kuna kitu akikisakanya mule chumbani kwangu ila baada ya kuniona akaacha, alijifanya kunipokea kwa maneno ya uongo na kweli huku macho yake yakiwa na wasiwasi sana. Mimi nilijifanya kama vile simuoni kisha nikamuomba anipishe nibadili nguo, aliondoka mule chumbani lakini akiwa na wasiwasi sana, baada ya mimi kumaliza kujiandaa nilimfuata pale sebuleni na kumuambia ya kwamba nilikuwa tayari hivyo kwa muda ule nilikuwa namuhitaji twende naye kimara kwenda kumfuatilia yule mwanamke, alinitazama kwa macho makali sana kisha akaniambia ya kwamba “hata kamishina nimemuambia ya kwamba mimi hiyo kazi siiwezi kabisa wewe endelea nayo peke yako tu” nilishangaa baada ya kusikia jibu lile kwani kusema kweli moja yaw au ambao tulikuwa tunawetegemea kwenye jeshi la polisi kaitka maswala ya upelelezi Jamila alikuwa ni mmoja wapo na dio maana hata jeshi liliamua kumpeleka nje yanchi kwenye ile kozi ya muda mfupi.
Nilisogea kwenye kochi alililokuwa amekaa kisha na kuanza kumueleza kwa taratibu umuhimu wake yeye katika ufuatiliaji wa ile kesi, alinisikiliza kwa umakini sana huku machozi yakiwa kama yanataka kumtoka, alinivuta taratibu na kuegemea kifuani kwake kisha na kuniuliza kwa sauti yenye upole uliochanganyika na simanzi ya kwamba. Kwani Siwah inamaana mpaka leo hii MWANAMKE MWENYE KOVU JEUSI BADO HUJAMTAMBUA? Niliitika kwa kichwa huku nikimkazia macho
Alinitazama sana kisha akaniambia basi leo utamjua ila naomba iwe siri yako na wewe ndio wa kumsaidia.
                                           *******************************
Jamila alianza kunieleza ya kwamba yeye ndio Mwanamke mwenye kovu jeusi, ambaye muda wot sisi tulikuwa tukimtafuta na hata yale mauaji ni yeye ndio alikuwa akiyafanya kutokana na moyo wake uliokuwa umejaa simanzi na makovu mengi, alianza kwa kunihadithia historia ya maisha yake kwa urefu sana toka alipozaliwa ya kuwa baba yake alimkataa katakata kitu kilichokuja kumletea matatizo mama yake ambapo alifukuzwa nyumabani kwao, alizaliwa huku mama yake akiwa yule kwa rafiki yake ambaye na yeye umri ulikuwa ni mdogo sana huku aiwa anajishughurisha na biashara ndogondogo. Aliendelea kunieleza ya kwamba baada ya mama yake kumzaa alipofikisha umri wa kwenda shule alianza kusoma kwa tabu sana kwani mama yake kipndi hicho ilimbidi afanye kazi ya kuuza pombe kwenye vilabu vya usiku, anakumbuka siku moja mama yake aliludi usiku sana huku akiwa ameambatana na mwanaume mmoja kwani siku zingine ilikuwa kawaida kwa mama yake kuja na wanaume mule kwenye kile chumba walichokuwa wamepanga na kulala nao mule huku yeye akitandikiwa mkeka na kulala chini. Anadai baada ya kuingia mule ndani kwa kuwa siku ile mama yake alikuwa amelewa sana basi baada tu ya kufika mule ndani alilala, fofofo ambapo yule mwanaume baada ya kumuona akiwa amelala pale chini alijikuta akianza kumtamani, ambapo alimsogelea na kumbaka, roho ilimuuma sana kwani alikuwa na umri mdogo sana na hata mama yake alipojaribu kumuambia alionekana kutokujali kile kitendo zaidi ya kumuambia ya kwamba naona umeanza kuku asana mwanangu.kiukweli ilimuachia kovu kubwa sana moyoni
Basi maisha yake yalikuwa ya hivyo hivyo ya kubangaiza hapa na pale baada ya kumaliza kidato cha nne aliweza kupata nafasi ya kujiunga na jeshi la polisi ambapo askari aliyesema atamuunganishia iyo nafasi nay eye pia alimtaka kimapenzi hakuwa na jinsi tena kwani maisha yalikuwa tayari yameshamtandika sana kwani hata sekondari nayo pia alisoma kwa shida shida sana. Alinitazama machoni Jamila huku machozi yakiwa yakimmtiririka kisha akaniambia ya kwamba tafadhari sana Siwah nakuomba unitunzie hii siri, sikuwa na kipingmizi kisha akendelea. Kuwa baada ya kuingia mafunzo ya polisi kuna siku moja alikuwa anaumwa hivyo basi yeye hakuenda kwenye mafunzo asubuhi ambapo baadaye mkuu msaidizi wa mafunzo alipita akiwa anakugua watu waliokuwa hawajaenda kwenye gwaride baada ya kumkuta alimfokea sana kisha akatishia kumuondoa kwa tatizo la uzembe, ilimbidi ambembeleze sana ambapo alimwambia sawa ila kama atakubali kulala na yeye( hapa nikavuta picha na majina yake yaliyokuwa kwenye orodha ya watu aliokuwa akitaka kuwauwa) alijifanya kunipokea kwa maneno ya uongo na kweli huku macho yake yakiwa na wasiwasi sana. Mimi nilijifanya kama vile simuoni kisha nikamuomba anipishe nibadili nguo, aliondoka mule chumbani lakini akiwa na wasiwasi sana, baada ya mimi kumaliza kujiandaa nilimfuata pale sebuleni na kumuambia ya kwamba nilikuwa tayari hivyo kwa muda ule nilikuwa namuhitaji twende naye kimara kwenda kumfuatilia yule mwanamke, alinitazama kwa macho makali sana kisha akaniambia ya kwamba “hata kamishina nimemuambia ya kwamba mimi hiyo kazi siiwezi kabisa wewe endelea nayo peke yako tu” nilishangaa baada ya kusikia jibu lile kwani kusema kweli moja yaw au ambao tulikuwa tunawetegemea kwenye jeshi la polisi kaitka maswala ya upelelezi Jamila alikuwa ni mmoja wapo na dio maana hata jeshi liliamua kumpeleka nje yanchi kwenye ile kozi ya muda mfupi.
Niliguna baada ya kusikia vile nilijua moja kwa  moja nilikuwa nahisiwa kuhusika na kifo cha mkubwa wangu wa kazi,niliwaomba dakika kadhaa niweze kujiandaa kwani nilikuwa nipo kifua wazi huku nikiwa nimevaa suruali ya kulalia tu, waliniambia hukuna tatizo, nilijua ingekuwa ngumu kwa mimi kunipeleka kama watu wengine kwani baadhi yao pale nilikuwa nawazidi cheo ofisini, basi niingia ndani na kujiandaa kisha nikabeba na baadhi ya vitu kwenye mkoba wangu na kutoka kwa ajiliya kuanza safari ya kuelekea makao makuu muda ule ule wa jioni kwa ajili ya mahojiano kama wao walivyokuwa wamenambia, niliinia kwenye ile discover ya polisi na kuanza kuelekea makao makuu.mule ndani ya gari wale wafanyakazi wenzangu walionekana kama ni watu waliokuwa wakinihofia sana kwani hata mazungumzo na mimi walkuwa wanazungumza kwa kusita siat asana hasa baadhi ya maswali ambayo nilikuwa nahitako ufafanuzi wao na ushirikiano wao.
 Nilijua tu itakuwa ni sumu iliyokuwa imesabazwa kuwa mimi nilikuwa nikishirikiana na yule muuaji katika kufanya yale matukio,kitu ambacho mimi kilinishangaza sana kwani sikuona ushirikiano baina ya mimi na yule mwanamkepia sikuona umuhimu wake ule wa kuuwa watu hovyo basi sikuwa na jinsi nianza kujiona kama mpweke Fulani hivi na mtu ambaye nilikuwa ninategwa na jamii bila ya sababu zisizo na maana, sikuwa na jinsi niona njia ya kulitatua lile tatizo ni moj tu nalo ni kuhakikisha yule mwanamke namkamata na kumfiksiha mbele yao hiyo ndio itakuwa njia yangu mimi kujosha kwani tofauti na pale bado jamii na wafanyakazi wenzangu watahisi ni mimi.
Tulifika pale makao makuu ya iwzara ya mambo ya ndani, tulipanda moja kwa moja mpaka gorofa ya pili ambapo ndipo zilipokuwa ofisi za jeshi la polisi, baada kuingia mule ndani nilikutana na kamishina mkuu wa jehi la polishi idara ya upelelezi, akiwa yupo pamoja na wasaidizi wake watatu, alionekana kama mtu aliyekuwa na hasira sana ilyochanganyikana na hudhuni Fulani, nilihisi itakuwa sababu ya kifo cha yule mkuu wangu wa kazi kwani alikuwa ni rafiki yake sana hata pia ile nafasi ni yeye ndio aliyempatia kutokana na na kujuana kwao nilisika pia hata depo waliingia pamoja,nilkaa kwenye kiti pale mbele kisha wale wafanyakazi walionipeleka wao walitoka nje na kuniacha mule ndani nikiwa pamoja na wale ma ofisa wa pale makao makuuu, kamishina alinitazama kama dakika tano hvi bila ya kusema neon lolote huku machozi yakionekana kama yalikuwa yanamrenga renga, na mimi skitaka kuzungumza kitu kwanza niliendelea kusubli mpaka pale wao wenyewe watakapoamua kuanza mazungumzo, mara yule msaidizi wake akamwambia “mkuu tumuhoji basi haraka haraka ili tujue ni kipi cha kuendelea nacho” kamishina alionekana kama vile kushituka kama ni mtu aliyekuwa akiwaza mbali sana ndipo alipoanza kuniuliza maswali mbali mbali kuhsu yule mwanamke namjua vipi nahusika vipi kwa nini wenzangu wanishitumu kwamba namjua na nashirikiana nae katika kumpa habari,
roho iliniuma sana baada ya kusikia kauli eti wenzangu wananishutumu.sikuamini kusikia vile, nilikaa kimua wakazungumza mule kwa takiribani dakika kumi na tano kisha na mimi ndipo nikafungua mdomo wangu kuanza kuwajibu, nilimueleza kila kitu ya kwamba yule mwanamke alikuwa ni mtu makini sana tofauti na sisi tulivyokuwa tunafikria, walitega sikio kwa makini kusikia kipi nilichokuwa nazungumza niliendelea kuwapasha ya kwamba mimi  naona kama nilikuwa tu nimetolewa kafara na mkuu wangu hasa baada ya kuona kazi inakuwa ngumu au kwa sababu matukio mengi yaliyokuwa yakimuhusu yule mwanamke nilikuwa nakutana nayo mimi au nahusika nayo,alinitazama usoni akionekana kabisa kuna kitu alikuwa akikisoma usoni kwangu kisha akaniambia ya kwamba na je ninajua vipi kuhusu kifo cha merehemu inspekta Thomas, nilimwambia kwa kweli mimi taarifa nilikuwa nazo lakini sikuwa najua lolote kuhusu kile kifo,
alinitazama na kisha hapo hapo akanipandishia swali jingine, je kwa nini nilikuwa sipatikani kwenye simu na kwenye msiba sikuwepo pia hata kwangu sikuwepo kama taarifa nilikuwa nazo, ilinibidi niwaeleze ukweli wote kwani nilijua kwamba bila vile wangeendelea kuwa na imani na mimi, niliwaeleza kila kitu kutoke siku ile nilipoambiwa ya kwamba nimesimamishwa kazi mpaka safari yangu ya Tanga na mwisho ile safari yangu ya visiwa vya shelisheli, niliwaeleza ya kuwa japo nilikuwa nimesimamishwa kazi lakini mimi kama ninilikuwa bado naendelea na ile kazi mwenyewe,walionekana kama vile walikuwa hawaniamini
,basi kama nilikuwa najua nilitoa tiketi ya ndege kutoka kwenye moja ya bahasha niliyokuwa nimetoka nayo nyumbani pamoja na na risiti za hoteli kule  visiwa vya sheli sheli walionkena kuanza kujenga imani tena na mimi. Basi baada ya yale mazungumzo yule kamishina mkuu aliniambia ya kwamba sasa itanibidi mimi niendelee na ule upelelezi bila ya kumjulisha mtu yoyote hasa wale niokuwa nafanya nao kazi kisha niwe nalipoti kwake, aliniambia ya kwamba taarifa alizokuwa nazo ni kuwa Jamila analudi kesho hivyo basi nayeye atamuunganisha na mimi kufanya ile kazi bila ya kuingiliana na na akina Amina, nilimshukuru sana kwa kuonyesha ule uelwewa,
 basi pale pale nilitoa baadhi ya vifaa ambavyo nilkuwa nimevipta ambavyo nilivihisisha moja kwa moja na yule mwanamke, walivitazama sana, kisha nikamuona kamisjina akiguna baada ya kuona kile kitabu kilichokuwa na namba za simu “mh mbona huu mwandiko kama vile naujua” alizungumza alijaribu kuvuta kumbukumbu pale bila ya kukumbuka ila akendelea kusisitiza ya kwamba ule mwandiko anauhakika kabisa alikuwa anaujua, alishangaa sana baada ya kukutana na plani za watu waliokuwa kwenye malengo ya yule mwanamke walizidi kuhoka sana, ndipo mkuu akaanza kunisisitiza tena nijitahidi basi asije leta madhara zaidi ya pale kwani mpaka pale ilikuwa ni doa kubwa sana kwenye jeshi la polisi, nilimwambia hakuna shida ile kazi hata mimi nimedhamiria kuifanya kwa nguvu zote li kuondoa ile dhana iliyokuwa imejengeka kwa wafanyakazi wenzangu.basi tulimaliza yale mazungumo huku mkuu wangu akinihakikishia kunipa msaada wowote ule ambao ningeutaka lakini ahakikishe tu kina Amina wasijue kama na mimi nilikuwa nafuatilia ile kesi, pia walinishukuru sana kwa ule moyo wangu niliouonyesha mpaka kutumia gharama zangu binafsi kwenye mpaka visiwa vya sheli sheli kwenda kumfuatilia yule mwanamke.
                                ********************************
Baada ya kumaliza kujihakikishia upekuzi tena wa ile simu ya yule mwanamke nilielekea asubuhi na mapema kwenye ofisi za tume ya mawasiliano ambapo nilikutana tena na afisa huyu akiwa ni mwingine kabisa ambaye alikuwa ni kijana mdogo sana akionyesha kama ni mtu aliyekuwa ametoka masomoni sio muda mrefu sana, nilizungumza naye pale kisha nikatoa kitambulisho changu ambapo baada ya kukiona ndipo nikaanza kumuelezea  sababu za mimi kuwa pale ofisini kwake asubuhi yote ile  alinisikiliza kwa makini kisha akachuka ile namba ya simu ya yule mwanamke na kuiingiza kwenye laptop yake ambapo aliangalia location ambapo ile namba ilikuwa inasoma mara kwa mara ilionekana ilikuwa inasoma mitaa ya kimara, alizidi kupekuwa mpaka umbali wa mahali ilipokuwa inasoma ile namba kutokea kwenye mnara wa simu, baada ya pale aliiprinti karatasi ikionyesha umbali wa mahali ambapo ule mnara ulikuwa ukisoma alinikabidhi huku akinijulisha kwamba kama kukiwa na shida nyingine basi nisisite kumfuata tena,nilipokea ile karatasi na kumshukuru kisha nikatoka nje na kuanza safari ya kuelekea pale kimara baruti ambapo ndipo mahali ile namba ilikuwa ikisoma.
Nilifika kimara na kisha kuelekea kule mahali nilipokuwa nahitaji kufika kwa ajili ya kuliona lile eneo nilitembea zaidi ya nusu saaa bila ya kuona ile ramani ambayo nilkuwa nayo mpaka ikanibidi niwauliza baadhi ya watu njiani ambao baada ya kunielekeza ndipo nikaendelea na safari yangu nilifika mpaka wenye ule mnara uliokuwepo kwenye ramani kisha nikatoa tena ramani yangu na kuanza kuangalia mwelekeo tena, niliiweza kuifuata mpaka nikafika kwenye ile nyumba kwani haikuwa mbali sana na ule mnara.
Nyumba yenyewe ilikuwa imejitenga kidogo huku ikionyesha dhahiri ya kwamba haikuwa na muda mrefu tokea imalizike ujenzi wake, basi nilijaribu kugonga moja kwa moja pale mlangoni kwani uzio wake haukuwa umekamilika vizuri hivyo hata geti ulikuwa bado haujawekewa, niligonga sana bila hata ya kupata majibu mwisho nikaelekea nyumba ya jirani ili niweze japo kupata habari mbili tatu kuhusu mkazi wa ile nyumba,niliweza kukutana na mlinzi mmoja wa kimasai wa ile nyumba ya jirani baada ya kumsalimia ndipo nilipoanza kumuulizia kwanza alikuwa anaonyesha tabu kujibu mara, hamjui mara yeye sio mlinzi wa iyo nyumba hivyo hajui kitu chochote lakini baada ya kumbembeleza sana huku nikimdanganya ya kwamba nilikuwa nimeambiwa ya kwamba dada yangu alikuwa ndio anakaa pale mimi ni mgeni nimetoka Morogoro nina mud asana nilkuwa sijafika dar hivyo basi baada ya kufika na kuulizia ndipo nilipoambiwa ya kwamba alikuwa amehamia kwenye nyumba ile, yule mmasai alinitazama kisha akaniambia ya kwamba, siku hizi hakuna cha bure nimpe hata pesa ya soda ndipo aweze kuniambia.
Sikuonyesha kusit kwani kwangu jambo muhimu lilikuwa ni kupata habari tu basi nilitoa shilingi elfu tano na kumpa, alishangaa sana kwani alijua labda nitampa elfu moja au mbili, basi hakuamin baada ya kumwambi ya kwamba achukue yote, aliifunga kwenye kona moja ya shuka lake la kimasai kisha ndipo akaanza kuniambia habari za kuhusu yule mwanamke alisema ya kwamba yeye hakuwa anamjua sana kwani huwa anaingia usiku au jioni huku akiwa na gari au piki piki na mara nyingi huwa anavaa anajifunika sana kiasi kwamba inakuwa vigumu sana kumuona, nilimuuliza mara ya mwisho kumuona ilikuwa ni lini aalinijibu ya kwamba kama siku tatu zilizopita na sio kawaida yake kwani mara nyingi huwa anapita kila siku,.
Basi nilivuta pumzi na kisha kumuuliza kama akimuona kwa sura atamkumbuka, aalisita kisha akasema, sizani kwa maana ni mtu ambaye huwa anapita ahuk akiwa na haraka haraka sana nilimuuliza pia kama huwa kuna wageni wanakuja kumtembelea alisema toka yule mwanamke aanze kukaa ile nyumba hajawahi kuona mtu yoyote yani mimi ndio nilikuwa mtu wa kwanza kja na kumuulizia kwani inaonekana yule mwanamke huwa anakuwa yupo bize sana,
 basi nilimshkuru kisha nikaanza kuondoka, basi yule mmasai akaniuliza sasa kama akija nimuambie nani kaja, nilisimama kisha nikamsogelea na kuanza kumwambia kwa sauti ya taratibu ya kwamba asimwambie lolote kisha nikampa namba yangu na kumwambiaya kwamba wewe ukimuona amekuja wewe nibeep mimi  nitakuja pia kutakuwa na zawadi yako nono,yule mmasai alionekana kufurahi sana kusikia kuwa nitampa zawadi. “sasa mtu mwenyewe huwa akija hakai sana unaweza kuja na usimkute” alinimabia yule mmasai basi na mimi nikamjulisha ya kwamba asiwe na wasiwasi kwani mimi nilikuwa naishi mazingira yale yale jirani hivyo hofu aondoe kabisa.
                                ***********************************
Nilifika uwanja wa ndege mida ya asubuhi na mapema kwa ajil ya kwenda kumpokea Jamila ambaye alikuwa mafunzoni nje ya nchi huku akiwa ameenda kujifunza kozi fupi ya mambo ya social intelligence  nilipaki gari yangu sehemu ya kuegeshea magari kisha nikaenda moja kwa moja sehemu ya kusubilia wageni,nilikuwa nimewahi kama muda wa dakika arobaini hivi kabla ya muda wa ile ndege ya KLM kufika, basi baada ya muda ile ndege ilifika namimi nilijiamisha na kuhamia sehemu ya kutokea abiria, baada ya dakika tano nilimuona Jamila  akiteremka huku akiwa ameshika begi lake dogo akiliburuta na mkoba wake mingine ukiwa kwapani, basi nilimsogelea na kumkumbatia huku nay eye akionyesha tabasamu pana kidogo kisha tukasalimiana pale, Jamila alionekana kufurahia sana mimi muda ule wa asubuhi yote kuwa pale kwa ajili ya kumpokea, aliongea kwa utani,ulilala ukinota nini?  Basi tulipanda kwenye gari yangu na kuanza safari ya kuelekea nyumbani kwake alikokuwa amepanga alikuwa amepanga magomeni. Ndani ya gari tulizungumza  mambo mengi sana huku mimi nikimwambia afadhali ameludi kwani mwanamke mwenye kovu jeusi bado anaendelea kusumbua jiji, alinitazama kwa macho ya hudhuni Fulani huku akionekana kama ni mtu aliyehisi kitu Fulani kisha akaniambia, inamaana mmeshindwa kumdhibiti , nimitamzama kisha nikamwambia ya kwamba pale tulikuwa tukimsubili yeye na yeye pia ajalibu kumkamata kama ile kazi likuwa ni rahisi,
nilimwambi kwani barua zangu pepe ulikuwa huzipati? Hali imekuwa mbaya sana juzi nilikuwa makao makuu waliniambia ya kwamba wewe ukifika tu utajumuika na mimi katika kufuatilia hili jambo kwa siri bila ya kuingiliana na kina Amina, aliguna kisha akajikuta anasema ya kwamba hapana katika hili jambo mimi mtanitaka radhi kabisa sitoweza kuifuatlia bora nipewe majukumu mengine, nilimmwambia kwa upole sasa Jamila hiyo kozi uliyokuwa umeenda kuisoma huko Marekani imekusaidia nini wakati mkuu wetu ameona ya kwamba wewe ndio utafaa zaidi halafu pia wewe huwa unakuwa shapu sana katika ufanyaji kazi ndio maana wamependekeza uifanye na mimi. Jamila alionekana kuafiki kwa shingo upande kuhusu kushirikiana na mimi katika lile jambo,
 basi tulifika kwake ambapo aliniacha mimi sebuleni kwake kisha yeye akaelekea chmbani kwake kwa ajili ya kujiandaa.
                               **************************
Ilikuwa ni mida ya saa mbili usiku wakati nipo zangu nyumbani kwangu nikitazama taarifa ya habari ndipo simu yangu ilipogiwa na namba ngeni, nilipopoke ile simu ikakata, basi nikaamua kuipigia ile namba mara akapokea kumbe alikuwa ni yule mmasai, “thatha yelo ulisema wewe nikikudeep utapiga thatha mona wapokea mpaka pesa yangu waimaliza yelo” alikuwa yule mmasai akilalamika baada ya mimi kupokea ile simu yangu. Nilimwambia asijali nitamtumia salio baada ya hapo kisha nikamwambia anijuze, ah nilikuwa nataka kukusalimu tu halafu huyu jirani ameingia muda huu basi fanya kuwahi kuja. Nilishituka kusikia vile halafu pia nlijiuliza ni vipi nitawahi kufika kule kwa maana kutoka mnazi mmoja mpaka kimara na kwa muda ule foleni ilikuwa ni kubwa sana.basi nilimjulisha ya kwamba hakuna shida nakuja, sawa usisahau zawadi yandu na vocha yangu, alimalizia yule mmasai.
Nilimpigia simu Jamila ili kumjulisha ajiandae nimpitie kwani kazi tayari ailikuwa imeshaanza kwa bahati mbaya simu yake ikawa haipatikani,nililaumu sana kwa kile kitendo kwani wakati naondoka kwake nilimwambia kuwa muda wowote ningeweza kumuhitaji kwa ajili ya ile kazi,basi nilijipakia mimi mwenyewe kwenye gari yangu huku nikiwa nimechukua bastola yangu moja
Niliondoa gari pale kwangu kwa mwendo wa kasi sana huku nikijaribu kutanua sehemu zingine ili niweze kufika mapema, japo njiani kulikuwa na foleni kubwa sana lakini baada ya saa moja na robo nilkiuwatayari nimeshafika tayari maeneo ya jirani na ile nyumba nilipaki gari yangu umbali wa kama mita mia tano hivi kisha nikashuka na kisha kuanza kuelekea kwenye ile nyumba, nilisogea mpaka kwa nyuma ya ile nyumba kisha nikaangalia kama kulikuwa na upenyo wa kupita kuingia mule ndani, sikuona geti kwani nyumba ilikuwa imezungushiwa ukuta kwa kule nyuma na ulikuwa ni mrefu sana,nilihangaika nikaona kama nikifanya shambulizi la kushitkiza na kuingia mule ndani basi nitakuwa najiweka hatiani kwani yule mwanamke angewza kunisikia na kunidhuru kwa lolote lile ilinbidi nigahili kisha nihamie upande wa mbele wa ile nyumba nilipanda juu ya mti na kujibanza sehemu moja hivi ambapo palikuwa na kama tawi Fulani lililojaa majani mengi hivi, kupitia pale niliweza kuona kwa mbali mule ndani taa ikiwa imewaka huku yule mwanamke akionekana akizunguka mara huku mare kue mule ndani, nilijilaumu sana kwa kwenda peka yangu niliogopa yasije nikuta kama yale ya makaburini,nilijaribu kumpigia simu Jmila lakini ikawa haipatikani
Basi niliona njia pekee pale ni kwenda tu moja kwa moja getini na kugonga kisha kuludi na kujifisha ili niweze kuon ni kipi kitanedelea, nilishuka chini ya mti na kwenda kugonga lile geti kwa nguvu sana kisha nkaludi kujificha kama nilivyokuwa nimepanga,yule mwanamke alionekana kushituka mule ndani, nadhani alijua tu ni raia wa kawaida basi akaja mpaka pale getini na kuchungulia hakuweza kuona mtu kisha akajirudisha ndani nahisi aifikiria watakuwa ni watoto tu wakifanya fujo, mwili ulinisisimka sana kwani ile sura ilikuwa sio ngeni kabisa machoni mwangu, nilihisi kama naifananisha sijui kutokana na lile giza,basi nikaona sio mbaya ngoja kwanza niendelee kuwa mvumilivu ili niweze kujua ni kipi kitaendelea.
mara baada ya kama nusu sasa nikaweza kumuona yule mwanamke akitoka mule ndani ilikuwa yapata kama mida ya saa sita usiku hivi kuangalia vizuri ile sura ilikuwa ni sura ya Jamila, nilishituka sana nikataka kumuita kisha nikasita alitoka mule ndani kwa kasi ana huku akiwa kama mtu aliyekuwana wasiwasi, baada ya kuondoka lile eneo, na mimi nilishuka juu ya ule mti na kuanza kuelekeakwenye gari langu kuanza safari ya kuludi kwangu, huku kichwani nikiwa na maswali mwengi kichwani je Jamila ndio yule mwanamke? Au baada ya kufika tu ameamua kuanza nay eye kumfuatilia kimya kimya yule mwanamke? Nilijikuta najihoji maswali mengi sana bila ya majibu, maana kila siku niliona jambo jipya likizuka kila siku, nilondoka pale huku nikiona njia nzuri ni kumtega tu Jamila ili kujua kila kitu kama ni yeye ndio muhusika au na yeye ndio alikuwa anafuatilia.nilijikuta nakosa jibu la uhakika zaidi pindi nitakapokutana naye ndio niliona naweza pata jibu.
                           ***************************************
Nilikutana na Jamila baada ya kumaliza mihangaiko yake ya mchana alikuja nyumbani kwangu ambapo alinikuta nikiwa bado nimelala sikuwa na haraka ya kuamka kwani kazini nilikuwa siendi hivyo muda mwingi nilikuwa nautumia tu kulala kama sina kazi nyingine ya kufanya.
Basi baada ya kuingia ndani kwangu alipitiliza mpaka chumbani kwangu, aliniomba ruhusa ya kukaa kwenye  kitanda changu ambapo na mimi bila ya hiyana nilimruhusu. Tulianza kuzungumza mambo mengi sana huku akinipa habari za hapa na pale,nilimuuliza kwa nini jana yake alizima simu usiku wakati nilikuwa namhitaji twende kumfuatilia mwanamke yule hatari alinijibu huku akiangalia pembeni yakwamba alikuwa amechoka sana hivyo basi ndio maana aliamua kuzima simu yake baada ya muda kumaliza kupata chakula cha mchana nilienda bafuni kuoga, wakati naludi nilimkuta Jamila akiwa kama kuna kitu akikisakanya mule chumbani kwangu ila baada ya kuniona akaacha, 

Nilisogea kwenye kochi alililokuwa amekaa kisha na kuanza kumueleza kwa taratibu umuhimu wake yeye katika ufuatiliaji wa ile kesi, alinisikiliza kwa umakini sana huku machozi yakiwa kama yanataka kumtoka, alinivuta taratibu na kuegemea kifuani kwake kisha na kuniuliza kwa sauti yenye upole uliochanganyika na simanzi ya kwamba. Kwani Siwah inamaana mpaka leo hii MWANAMKE MWENYE KOVU JEUSI BADO HUJAMTAMBUA? Niliitika kwa kichwa huku nikimkazia macho
Alinitazama sana kisha akaniambia basi leo utamjua ila naomba iwe siri yako na wewe ndio wa kumsaidia Jamila alianza kunieleza ya kwamba yeye ndio Mwanamke mwenye kovu jeusi ila alikuwa akiomba msaada wangu kuniepusha na mikono ya haki.

MWISHO WA KWANZA WA HII HADITHI NDIO LEO JIANDAE NA SEHEMU YA PILI YA
                              “MWANAMKE MWENYE KOVU JEUSI”
0717-376735

1 comment:

  1. hello,
    Hii ni kuwajulisha wananchi kwa ujumla kuwa Bibi, kiutamaduni matumaini binafsi mkopo wakopeshaji ina kufungua nafasi mpya za fedha kwa kila mtu katika haja ya msaada wowote wa kifedha. Sisi kutoa mkopo saa 2% riba kwa watu binafsi, makampuni na makampuni chini ya sheria wazi na ya kueleweka na hali hiyo. wasiliana nasi leo na e-mail (merithope6@gmail.com)

    ReplyDelete

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages