Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Atembelea Makazi ya padri Ambrose Mkenda Paroko wa kanisa katoliki la Mpendae Zanzibar na kuupa pole uongozi wa Kanisa hilo pamoja na Familia yake kufwatia ajali ya kupigwa risasi hivi karibuni na watu wasioujulikana - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Atembelea Makazi ya padri Ambrose Mkenda Paroko wa kanisa katoliki la Mpendae Zanzibar na kuupa pole uongozi wa Kanisa hilo pamoja na Familia yake kufwatia ajali ya kupigwa risasi hivi karibuni na watu wasioujulikana

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akiangalia gari ya Paroko wa Parokia ya Mpendae Padre Ambrose Mkenda ambayo alikuwa akiendesha na kuvamiwa kwa risasi ya watu wasiojuilikana
 Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar akipata maelezo kutoka kwa Uongozi wa Skuli ya Francis Maria Tomondo ambapo Padre Ambrose Mkenda wa Paroko ya Parokia ya Mpendae alijeruhiwa kwa risasi hivi karibuni
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akifuatana na Father Shayo wa Kanisa la Roman Catholic liliopo minara miwili baada kuwafariji na kutoa mkono wa pole kwa uongozi wa huo kufuatia kujeruhiwa kwa Paroko wa Parokia ya Mpendae Padre Ambrose Mkenda.
---
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alifika katika makazi ya padri Ambrose Mkenda wa Paroko wa parokia ya kanisa katoliki la Mpendae Zanzibar kuupa pole uongozi wa Kanisa hilo pamoja na Familia yake kufuatia ajali ya kupigwa risasi hivi karibuni na watu wasioujulikana. 
Tukio hilo la kusikitisha lililofanywa na watu wawili waliopakiana kwenye Vespa lilitokea langoni mwa Skuli ya Francis Maria iliyopo Tomondo Wilaya ya Magharibi ambapo ndio makaazi ya Padri Ambrose.

Balozi Seif akiufariji Uongozi huo alisema ni jambo baya na la kusikitisha lililofanywa na watu hao ambalo limetoa sura mbaya kwa Taifa na Serikali kupitia vyombo vyake vya ulinzi itaendelea kufanya uchunguzi wa tukio hilo na haitasita kuwachukuliwa hatua za kisheria watu watakaobainika kufanya uhalifu huo.
Alisema Serikali imesikitishwa na kulaani kitendo cha watu hao ambacho kinaashiria uvunjifu wa amani pamoja na kuwaweka wananachi katika hali ya wasi wasi usio wa lazima ndani ya harakati zao za kimaisha. 
Akitoa shukrani kwa niaba ya Uongozi na Familia ya Padre Ambrose Mkenda Kiongozi kutoka Kanisa la Roman Catholic Father Shayo aliiomba Serikali kuendelea kuimarisha ulinzi wa raia wema ili kupunguza hofu iliyotanda mioyoni mwao kutokana na matukio ya uvamizi.
Father Shayo alitahadharisha kwamba hulka mbaya iliyoanzishwa na baadhi ya watu kuwafundisha watoto wadogo tabia ya kukashifu watu wazima kwa sababu ya utofauti wa Kidini inawajengea maisha mabovu watoto hao. “ Watoto wadogo kufundishwa tabia ya kukashifu watu wengine tuelewe kwamba Taifa halitakuwa na muelekeo mwema wa jamii yake ya baadaye”. Alitahadharisha Father Shayo. 

  Na 
Othman Khamis Ame
Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais Zanzibar

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages