POLISI WATAWANYA WANANCHI WALIOKUSANYIKA KUSHUHUDIA MISUKULE MKOANI IRINGA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

POLISI WATAWANYA WANANCHI WALIOKUSANYIKA KUSHUHUDIA MISUKULE MKOANI IRINGA

Wananchi wakiwa wamekusanyika eneo la Mwangata mjini Iringa baada ya uvumi kuwa kuna msukule kaonekana eneo hilo.
Polisi wakidumisha amani na kuwasaka walioeneza uvumi huo.
Shughuli zikiwa zimesimama baada ya taarifa hizo za kuwepo msukule.

ZIMEZUKA  habari  zenye utata ambazo hazijathibitishwa mkoani Iringa  kuwa mtoto mmoja anayedaiwa kufa na kuzikwa  kuonekana jana akidaiwa kuwekwa Msukule.

Tukio  hilo  limetokea eneo la Mwangata mjini Iringa  na kupelekea  polisi  kufika  kuwatawanya  wananchi waliokusanyika eneo hilo na kuwasaka  wale wanadaiwa kueneza uvumi huo. Hata  hivyo hakuna mwananchi hata mmoja kati ya  waliokuwepo eneo hilo ambaye amethibitisha  kuona msukule  huyo zaidi ya kila mmoja kusema amesikia.


Wananchi hao wameizunguka moja kati ya nyumba eneo hilo wakitaka  kuichoma moto kwa madai kuwa ndani kuna msukule  huyo.


Habari / Picha kwa hisani ya : FRANCIS GODWIN BLOG

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages