PICHA ZAIDI ZA RICK ROSS AKIFANYA MAKAMUZI KWENYE STAGE YA SERENGETI FIESTA 2012 NDANI YA LEADERS CLUB USIKU HUU - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

PICHA ZAIDI ZA RICK ROSS AKIFANYA MAKAMUZI KWENYE STAGE YA SERENGETI FIESTA 2012 NDANI YA LEADERS CLUB USIKU HUU

Mtu mzima Rick Ross “The Boss” kutoka nchini Marekani hivi sasa yuko jukwaani kwenye Tamasha la Serengeti Fiesta 2012 linalofanyika kwenye viwanja vya Leaders Kinondoni jijini Dar salaam ,anakamua ile mbaya na mashabiki wamepagawa vyakutosha kwa kila anachowaelekeza kufuata wanafuata jamaa amefunika mbaya, hiii ni mara yake ya kwanza kufanya onesho nchini Tanzania
Rick Ross hapa akiwaelekeza jambo mashabiki hawapo pichani wakati alipokuwa akiimba jukwaani usiku huu.
Rick Ross akiendelea kupagawisha mashabiki wake usiku huu kwenye viwanja vya Leaders
Watu wa usalama wakijaribu kudhibiti rapsha zilizokuwa zikijitokeza  kutokana na mashabiki wengi kuwa na hamu ya kumuona mwanamuziki Rick Ross
Bibi Cheka na Stiko kutoka pande za TMK nao wakafanya mambo makubwa,
Wadau kutoka Serengeti wakifyurahia jambo katika burudani ya muziki.
Kulia ni Mkurugenzi wa Masoko SBL Ephraim Mafuru na kutoka kushoto Meneja wa Masoko SBL Emmilian Rwejuna na Mdau Rawlence Mafuru pamoja na wadau wengine wakipozi kwa picha.
Wadau mbalimbali wakifuatilia burudani ya mwanamuziki Rick Ross wakati alipokuwa akitumbuiza,
Mkurugenzi wa Masoko wa kampuni ya bia ya Serengeti SBL Bw Ephraim Mafuru akitangaza mshindi wa bahati nasibu ya magari mawili kwa mkoa wa Dar es salaam iliyoendeshwa katika matamasha yote ya Serengeti Fiesta mwaka huu kutoka kulia ni Bw. Mrisho kutoka bodi ya michezo ya kubahatisha , Rugambo Rodney Meneja masoko wa Push Mobile na kushoto ni Mkurugenzi wa Clouds Entarteinment Bw Joseph Kusaga wakishuhudia tukio hilo
Pichani chini na juu mashabiki wakishangilia kwa nguvu wakati wanamuziki huyo akiimba jukwaani
Rachel Mwanamuziki wa Bongofleva kutoka kundi la THT akicheza na mmoja wa wacheza shoo wake  katika Tamasha la Serengeti Fiesta linalofanyika usiku kuu kwenye viwanja vya Leaders jijini Dar es salaam ambapo pamoja na wasanii mbalimbali wakali wa nyumbani, mwanamuziki maarufu wa Hiphop kutoka nchini Marekani Rick Ross “The Boss” atahitimisha tamasha hilo kwa shoo kali usiku huu.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages