Rafiki Elimu Foundation Wazindua Mradi Wa Elimu Ya Ujasiriamali Mijini Na Vijijini " EUMIVI PROJECT " - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Rafiki Elimu Foundation Wazindua Mradi Wa Elimu Ya Ujasiriamali Mijini Na Vijijini " EUMIVI PROJECT "

Wajasiriamali  wakifanya  "  practical "  ya  kutengeneza  sabuni  ya  maji  kwa  vitendo  mara  baada  ya  kupokea  maelekezo  kutoka  kwa  waalimu  wa  ujasiriamali  kutoka  katika  Asasi  ya  RafikiElimu   Foundation. 
Mwanafunzi  wa  ujasiriamali  akitengeneza  sabuni  ya  unga  mwenyewe  mara  baada  ya  kupata  maelekezo  kutoka  kwa   waalimu  wa  ujasiriamali  kutoka  RafikiELIMU  Foundation.
Mwalimu  wa  Ujasiriamali  kutoka  katika  Taasisi  ya  RafikiElimu  Foundation, Mama  Ashankira  Lupembe  , akifundisha  kwa  vitendo  namna  ya  kutengeneza  sabuni   ya  maji.
Baadhi  ya  wajasiriamali  walio  hudhuria  katika   Uzinduzi  wa Mradi  wa  Elimu  Ya  Ujasiriamali  Mijini  &  Vijijini  uliofanyika   leo  jijini  Dar  Es  salaam. 

Akiulezea mradi huu, mratibu msaidizi wa mradi huo alisema kuwa mradi huu upo katika awamu kuu mbili. Awamu ya kwanza itafanyika kuanzia tarehe 01 Septemba 2012 hadi tarehe 29 Septemba 2012, na utafanyika katika mikoa ya Dar Es salaam, Arusha, Mwanza, Mbeya, Morogoro, Dodoma na Kilimanjaro, ambapo mbali na kutoa mafunzo ya ujasiriamali, asasi itatafuta vijana kumi na wawili kutoka katika hiyo mikoa saba kwa ajili ya kufanya kazi kama wajitoleaji " volunteers" katika awamu ya pili ya mradi itakayo anza rasmi tarehe 01 Novemba 2012 na kuchukua miaka miwili hadi Novemba 2014 ambapo ndipo itakapo kuwa tamati ya mradi huu.

Awamu ya kwanza ya mradi huu inafanyika katika mikoa ya Dar Es salaam, Arusha, Morogoro, Kilimanjaro, Dodoma, Mwanza na Mbeya. Jijini Dar Es salaam, mafunzo yanafanyika kwa siku tatu kuanzia tarehe 01 Septemba 2012 hadi tarehe 04 Septemba 2012 katika Shule ya Msingi Mlimani , iliyopo katika Chuo Kikuu Cha Dar Es salaam... Ratiba kamili ya awamu ya kwanza ya mafunzo haya ni kama ifuatavyo :

1. ARUSHA, MOSHI & MOROGORO : Mafunzo yatafanyika kuanzia tarehe 17 hadi 19 Septemba 2012.. Mwisho wa kujiandikisha katika " programme hii " kwa wakaazi wa ARUSHA, MOSHI na MOROGORO ni tarehe 15 Septemba 2012.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages