KIBAKA ANUSURIKA KUFA BAADA YA WALINZI KUMTOA MIKONONI MWA WANANCHI WENYE HASIRA KALI POSTA MPYA - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

KIBAKA ANUSURIKA KUFA BAADA YA WALINZI KUMTOA MIKONONI MWA WANANCHI WENYE HASIRA KALI POSTA MPYA

 Kichapo kinaendelea......
 Askari huyo akijitahidi kumuwahisha kumuingiza ndani ya geti....
Akifunga geti baada ya kufanikiwa kumuokoa kutoka katika msiti wa wananchi wenye hasira kali, huku wananchi hao wakipiga kelele kuwa waachiwe wammalize...
 Askari wa Kampuni ya Ulinzi anayelinda katika Jengo moja ya benki iliyopo Barabara ya Bibi Titi eneo la Posta Mpya jijini Dar es Salaam, alienda chini na Kibaka aliyekuwa akimuokoa kutoka mikononi mwa wananchi wenye hasira kali, baada wananchi hao kuanza kumpa kichapo cha haja baada ya kibaka huyu kukwapua Ipad katika moja ya gari lililokuwa katika foleni lililokuwa likiendeshwa na Mwanamama wa Kihindi na kudakwa na mmoja wa dereva aliyekuwa nyuma ya gari hilo wakati akijaribu kukimbia na kumuitia mwizi. Baada ya sauti hiyo ya kuitiwa mwizi wananchi waliitikiwa wito na kuanza kumuandamisha ambapo hakufanikiwa kufika mbali walimdaka na kuanza kumpa kichapo hadi alipoingilia kali askari huyo na kumuokoa kisha kumfungia ndani ya geti alilokuwa akilinda.Picha Kwa Hisani Ya Sufiani Mafoto Blog

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages