Richard
Ragan (kulia) akipeana mkono na Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika,
Christopher Chiza(kushoto wa pili) jana jioni (juzi) mjini Dodoma mara
baada ya utiaji saini wa makubaliano ya ushirikiano wa ununuzi wa
mahindi kutoka kwa vikundi vya wakulima wenye lengo la kupanua masoko
kwa wakulima. Pia Chakula hicho kitawanufaisha watu milioni nane
wanaokabiliwa na uhaba wa chakula kwa msaada wa WFP katika nchi za
Afrika kipindi cha mwaka 2012/ 2013. Kushoto ni Katibu Mkuu wa Wizara
ya Kilimo, Chakula na Ushirika , Mohamed Muya na wa (pili kulia) ni
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Charles
Walwa .
Katibu
Mkuu wa Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika , Mohamed Muya(kushoto),
Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Charles
Walwa na Mwakilishi Mkazi na Mkurugenzi wa Shirika la Chakula la
Dunia(WFP), Richard Ragan (kulia) wakisaini mkataba wa makubaliano ya
ushirikiano wa ununuzi wa mahindi kutoka kwa vikundi vya wakulima
wenye lengo la kupanua masoko kwa wakulima. Pia Chakula hicho
kitawanufaisha watu milioni nane wanaokabiliwa na uhaba wa chakula kwa
msaada wa WFP katika nchi za Afrika kwa kipindi cha mwaka 2012/2013 .
Kushoto wa pili ni Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Christopher
Chiza akishuhudia utiaji saini huo katika Ofisi za wizara hiyo
jana(juzi) mjini Dodoma.Picha na Magreth Kinabo, MAELEZO.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)