Waziri
Mkuu Mizengo Pinda, akiweka wa jiwe la msingi katika jengo la Ofisi ya
Taifa ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali mjini Dodoma leo. Jengo
hilo jipya lenye urefu wa ghorofa nane, linatarajiwa kuwa Makao Makuu
ya Ofisi hiyo.
Waziri
Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na baadhi ya wafanyakazi wa Ofisi ya
Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, wakati alipowasili kwa
ajili ya kuweka jiwe la msingi katika Jengo hilo leo.
Waziri
Mkuu Mizengo Pinda , akipata maelezo kutoka kwa Meneja Ujenzi wa
jengo hilo, Casmil Muscbi. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dodoma
Dkt.Rehema Nchimbi, watatu kutoka kushoto ni Mwakilishi wa Mdhibiti
na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Athanas Pius .
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Dkt.Rehema Nchimbi, akishiriki kusebeneka na wasanii wa ngoma za asili, wakati wa hafla hiyo.
Waziri
Mkuu Mizengo Pinda akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuweka wa
jiwe la msingi katika jengo la Ofisi ya Taifa ya Mkaguzi Mkuu wa
Hesabu za Serikali mjini Dodoma litakalokuwa na urefu wa ghorofa nane na
linatarajiwa kuwa Makao Makuu ya Ofisi hiyo.Picha zote na Magreth Kinabo- Maelezo
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)