Martin Sospeter Luhangisa, Meneja wa bendi ya Mashujaa.
BAADA
ya kukamilisha ziara ya kutambulisha wanamuziki wake wapya wa Mashujaa
Band, sasa ni zamu ya kuwapa burudani wapenzi wa bendi hiyo kwa siku ya
Idd Mosi na Idd Pili.
Meneja wa Bendi hiyo Martin Sospeter, alisema kuwa, siku ya Idd mosi watakuwa Msasani kwenye ukumbi wa Emirates.
Sospeter alisema kuwa, siku ya Idd pili watakuwa Mjini Mtwara katika ukumbi wa Makonde Beach ili kuwapa radha wakazi wa huko.
Bendi
hiyo ambayo hivi sasa ipo hivi chini ya Rais wake Chalz Baba, itatoa
burudani hiyo kwa ajili ya kutangaza kazi zao mpya kwa wapenzi wa nyimbo
zao na Bendi yao kwa ujumla.
Alisema,
pia kwa wale wanaoisikia Bendi ya Mashujaa kwenye vyombo vya Habari,
sasa ndiyo wakati wao wa kuiona bendi hiyo laivu katika Sherehe za Eid
El Fitri.
“Kama
tulivyowapagawisha wakazi wa Songea na Mbeya wiki iliyopita, sasa ni
zamu ya wakazi wa jiji la Dar es Salaam na Mtwara,” alisema Sospeter
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)