African Barrick Gold (ABG) yatoa Msaada wa Chakula Shinyanga na Geita - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

African Barrick Gold (ABG) yatoa Msaada wa Chakula Shinyanga na Geita

 Kutoka Kushoto: Mkuu wa Wilaya ya Nyang'hwale, Ibrahim Marwa, Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya wakipokea msaada wa sehemu ya tani 200 za mahindi kutoka kwa Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu, Dennis Hoof (wa pili kulia)na Makamu wa Rais wa African Barrick Gold (ABG),Utekelezaji Muundo, Peter Gereta katika hafla iliyofanyika katika Kata ya bulyanhulu wilayani Kahama mkoa wa Shinyanga hivi karibuni. Maeneo yatakayonufaika na msaada huo uliogharimu kiasi cha milioni 163/- ni kwa wale waliokumbwa na uhaba wa chakula katika vijiji 14 vilivyoko Bugarama, Mwingiro na Bulyanhulu wilaya ya Kahama mkoa wa Shinyanga na Nyang'hwale Mkoa  mpya wa Geita. 
 Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya akipokea msaada wa tani 200 za mahindi kutoka kwa Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu, Dennis Hoof (wa pili kulia). Kushoto ni Diwani wa Kata ya Bulyanhulu, Joseph Makoba.
 Mkuu wa Wilaya ya Nyang'hwale, Ibrahim Marwa akihutubia kabla ya makabidhiano.
 Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya akihutubia kabla ya makabidhiano. Kulia ni Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu, Dennis Hoof  na Kushoto ni Diwani wa Kata ya Bulyanhulu, Joseph Makoba na Mkuu wa Wilaya ya Nyang'hwale, Ibrahim Marwa.
 Mbunge wa Msalala, Ezekiel Maige akibadilishana mawazo na Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu, Dennis Hoof (katikati), na Makamu wa Rais wa African Barrick Gold (ABG),Utekelezaji Muundo, Peter Gereta.
 Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu, Dennis Hoof akijadiliana jambo na  Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya.
 Kutoka Kushoto: Meneja Mkuu wa Mgodi wa Dhahabu wa Bulyanhulu, Dennis Hoof , Mkuu wa Wilaya ya Kahama, Benson Mpesya na Mkuu wa Wilaya ya Nyang'hwale, Ibrahim Marwa wakikagua sehemu ya shehena ya mahindi mara baada ya makabidhiano. 
Sehemu ya viongozi wa vijiji lengwa na msaada huo  waliohudhuria hafla hiyo.Picha Zote na Badi John

1 comment:

  1. Cha kushangaza ni kwamba mkoa unaopewa msaada ni mkoa unaoongoza kwa uzalishaji wa madini ya Almasi na Dhahabu Tanzania. Pia unaongoza kwa kuwa na wafugaji wengi zaidi wa Ng'ombe katika nchi yetu. Kama hiyo haitoshi, mkoa huu ni katika mikoa inayolima Mahindi, Mpunga, Mihogo na viazi kwa wingi ndani ya Tanzania yetu. Ni lini tutaacha kuingiza mambo ya siasa katika kila jambo tunalofanya? Ukiangalia picha hapo hao wanasiasa wanaona wamefanya jambo la kishujaa sana katika kupokea msaada. Wananchi either hawatambui nini kinaendelea au wanawaona jamaa wamewaona majuha kupitiliza. Tuache siasa nyingi!!!

    ReplyDelete

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages