Baadhi
ya maofisa Habari, Elimu na Mawasiliano wa Serikali wakiwa katika picha
ya pamoja baada ya kuwasili kwenye lango la kuingia Hifadhi ya Taifa ya
Serengeti mkoani Mara ikiwa ni moja ya mkakati wa kuhamasisha utalii
wa ndani nchini.
Maofisa
habari wakipata kifungua kinywa katika eneo la Lamadi lililopo mkoa
mpya wa Simiyu wakiwa njiani kuelekea katika hifadhi ya taifa ya
Serengeti.
Mfanyabiashara
wa supu katika eneo la Lamadi mkoani Simiyu Bw. Sobia Majuto
akiwahudumia baadhi ya wateja wake ambao ni maofisa Habari na
Mawasiliano wa Serikali walipokua njiani kuelekea katika hifadhi ya
Taifa ya Serengeti .
Wanyama
aina ya Twiga ambao ni moja ya kivutio kikubwa katika hifadhi ya taifa
ya Serengeti wakitembea kwa mstari ndani ya hifadhi hiyo.
Kundi kubwa la Nyumbu, wakiwa katikati ya Barabara ndani ya hifadhi hiyo na kuufanya msafara wa magari yaliyokuwa
maofisa Habari, Elimu na Mawasiliano wa serikali kwenda kwa mwendo wa
polepole, Kwa mujibu wa taratibu za hifadhi ni kosa kwa dereva kupiga
honi, kuendesha gari kwa mwendo kasi au kupiga honi ndani ya eneo la
hifadhi.
Mnyama
aina ya Simba maarufu kwa jina la mfalme wa mwitu akipanda mti ndani ya
hifadhi ya Taifa ya Serengeti na kuwafanya maofisa Habari na
Mawasiliano wa serikali kushangaa uwezo wa Simba huyo. Simba wa aina hii
wanaoishi ama kupanda juu ya miti hupatikana ndani ya Hifadhi ya
Serengeti pekee. Picha na Aron Msigwa – MAELEZO
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)