Timu ya Tanzania DMV watachuwana vikali na timu ya Ethiopia Kundi (B) - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Timu ya Tanzania DMV watachuwana vikali na timu ya Ethiopia Kundi (B)

Na Abou Shatry

Katika mchezo wa lingi ya 2011 Diaspora World Cup zinazoendelea katika viwanja vya Hyattsville na Germantown jijini Maryland Nchini Marekani, timu ya Tanzania DMV watachuwana vikali na timu ya Ethiopia Leo hii Jumamosi May 12, 2012 mida ya 12:PM (Mchana wa saa sita) katika kiwanja cha Greencastle, kiliopo Burtonsville, Maryland
  
Kundi (B) Timu ya wa Ethiopia katika mchezo wa awali walifungwa bao 3-0 na timu ya Malawi ndani ya uwanja cha  Greencastle, Burtonsville, Maryland, ambao leo watajianda vikali ili kutaka kurudisha nguvu zao kwa mchezo waliopoteza dhiti ya timu hiyo ya Malawi, ambao leo hii timu ya Malawi watapambana vikali  na timu ya Armenia mida ya saa 1:PM Mchana wa leo, kwa mechi ya kwanza timu ya Armenia waliwabamiza Nigeria bao 4-1 katika mchezo wa awali.

Pia timu ya waTanzania DMV katika mchezo wa kwanza siku ya Jumapili ya April 29,2012 walifanikiwa kuwabamiza timu ya Ghana bao 3-2 ndani ya uwanja wa SoccerPlex Stadium uliopo Ager Road Hyattsville Maryland.

Kama kawaida  yao timu ya waTanzania DMV inawaomba Watanzania wote ushirikiano wenu wa kila hali ili kuipa changamoto timu ya Watanzania DMV, mnaombwa pia kufika mapema mida ya saa 11:AM  kuzowea mazingira kabla ya mchezo huo kuanza.

Adress ya mchezo utakaochezwa leo hii ni Fairland Field 3928 Greencastle Rd. Burtonsville, Maryland  20866 Habari na http://swahilivilla.blogspot.com/

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages