NMB NA SERENGETI ZAICHANGIA TWIGA STARS MILIONI THELATHINI - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

NMB NA SERENGETI ZAICHANGIA TWIGA STARS MILIONI THELATHINI

Katika kuendeleza soka Tanzania, leo hii Benki ya NMB kwa kushirikiana na kampuni ya Bia ya Serengeti imesaidia maandalizi  ya Twiga Stars kwa kutoa  jumla ya shilingi Milioni Thelathini. Pia NMB na Serengeti wamekabidhi vifaa  vyenye  thamani ya Milioni Tano kwa timu hiyo ya Twiga Stars.
 Naibu Mkurugenzi wa michezo, Bi. Juliana Yasoda (kulia) akipokea vifaa vya michezo kutoka kwa  Mkurugenzi wa Masoko wa Serengeti, Bw. Ephraim Mafuru (kati) na Mkuu wa Idara  ya  Masoko na Masiliano wa NMB, Bw. Imani Kajula (Kushoto). Wanaoshuhudia  tukio hilo ni Mkurugenzi wa Ufundi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Bw. Sunday Kayuni (pili kushoto) na kocha msaidizi wa Twiga Stars Bi. Nasra Mohamed.
 
Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo, Mkuu wa idara ya Masoko na Mawasiliano wa NMB Bw. Imani Kajula alisema; NMB imekua  mbele  katika  kuchangia soka Tanzania, leo hii NMB ikishirikiana na Serengeti tunachangia maandalizi ya Twiga Stars”.

NMB inatambua kuwa Twiga Stars ikiwezeshwa inaweza ikafanya vizuri zaidi. Ili kutimiza lengo hili, NMB Ikiwa ndiyo  benki yenye mtandao mpana wa matawi mengi Tanzania nzima pia imeanzisha akaunti maalum kwa ajili ya kuchangia Twiga Stars. Yeyote atakayeguswa kuchangia Twiga Stars anaweza kuchangia kupitia akaunti namba 22310001185 yenye jina CHANGIA TWIGA STARS ACCOUNT

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages