NCHI MBALIMBALI ZAENDELEA KUTANGAZA WAWAKILISHI WAO MISS EAST AFRICA 2012 - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

NCHI MBALIMBALI ZAENDELEA KUTANGAZA WAWAKILISHI WAO MISS EAST AFRICA 2012

Miss Lula Teklehaimanot (19) kutoka Ethiopia


Warembo watakaoziwakilisha Nchi zao katika mashindano ya Miss East Africa mwaka huu wanaendelea kupatikana kutoka katika Nchi mbalimbali zinazoshiriki mashindano hayo.

Mrembo mwingine aliyeingia fainali ni Miss Lula Teklehaimanot (19) kutoka Nchini Ethiopia ambae alipatikana mwishoni mwa wiki baada ya kuwashinda warembo wenzake waliojitokeza kutaka kuiwakilisha Ethiopia katika fainali hizo.

Miss Lula Teklehaimanot ana urefu wa 1.79m na uzito wa 52kg ni mwanafunzi wa mwaka wa kwanza katika chuo cha St. Merry University cha jijini Addis Ababa, Ethiopia ampapo anasomea degree ya Marketing

Pia Mrembo huyo ni miongoni mwa wanamitindo maarufu  wanaochipukia kwa kasi Nchini Ethiopia.

Fainali za mashindano ya Miss East Africa 2012 zitafanjika tarehe 07 mwezi September mwaka huu jijini Dar es salaam ambapo zitashirikisha Nchi za Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Somalia, Djibouti, Eritrea, Sudan, Ethiopia, Malawi, Madagascar, Reunion, Comoros, Seychelles, na Mauritius.

Mashindano ya Miss East Africa yanaandaliwa na kumilikiwa na kampuni ya Rena Events Ltd ya jijini Dar es salaam

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages