Mfuko wa Mashirika ya Umma (PPF)Kanda ya Ziwa Waipiga Tafu Mwauwasa Saccos - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Mfuko wa Mashirika ya Umma (PPF)Kanda ya Ziwa Waipiga Tafu Mwauwasa Saccos

 Mkopo huo umetolewa na PPF kwa Mwauwasa Saccos ni moja ya huduma zinazotolewa na PPF na wanachama wake ili kuwawezesha kiuchumi na kuwaondolea ugumu wa maisha unaotokana na kukosa kipato cha kutosha na pia kuwaandaa waweze kuwa na maisha bora wawapo katika ajira na mara baada ya kustaafu.

"Huu ni mpango mahususi wa PPF katika kuboresha maisha ya wanachama wake, mpaka sasa PPF imekwishatoa kiasi cha zaidi ya shilingi bilioni 40 kwa vyama vya kuweka na kukopa 36 kwa nchi nzima , na lengo la utoaji wa mikopo hiyo ni kuwawezesha wanachama wa PPF katika ujenzi wa nyumba, kulipa gharama za elimu, kujiendeleza katika kilimo, kujiendeleza kibiashara na kuwa na ufugaji bora”, alisema Meshack Bandawe (Pichani).
  Mwenyekiti wa Mwauwasa Saccos, Vedastus Pilla (Pichani) ameushukuru uongozi wa PPF kwa uamuzi iliouchukua ya kuiweza Mwauwasa Saccos ili iweze kuimarika kiuchumi na kuwawezesha wanachama wake kupata maisha bora.
Meneja wa MWAUWASA Saccos, akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa mfuko wa PPF pamoja na wanachama wa chama hicho cha kuweka na kukopa cha Mamlaka ya Maji safi na majitaka jijini Mwanza, muda mfupi baada ya kukabidhiwa mfano wa hundi ya shilingi milioni 900 za mkopo kwa wanachama wa saccos hiyo leo.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages