- LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Breaking

Home Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here
OFISI YA RAIS IKULU-UTAWALA BORA


TAARIFA KWA UMMA

TAMKO LA SERIKALI KUHUSU MPANGO WA UENDESHAJI WA SHUGHULI ZA SERIKALI KWA UWAZI (OPEN GOVERNMENT PARTNERSHIP - OGP)

          Tanzania imeridhia kujiunga na Mpango wa Uendeshaji wa Shughuli za Serikali kwa Uwazri (Open Government Partnership – OGP).  Mpango huu ni juhudi za kimatifa katika kuhimiza uendeshaji wa Serikali kwa uwazi zaidi, ushirikishwaji mkubwa wa wananchi, kudhibiti rushwa katika jamii na kuimarisha utoaji wa huduma bora.

          Vigezo vya nchi kuwa mwanachama wa Mapango huu ni pamoja na kuandaa Mpango Kazi wa Kitaifa (Country Action Plan) kwa kushirikiana na wadau mbalimbali zikiwemo Asasi za Kiraia, Sekta Binafsi na wananchi. 
          Kwa kuanzia, uandaaji wa utekelezaji wa Mpango huo utahusisha vipaumbele katika sekta tatu za Afya, Elimu na Maji ili kuimarisha uwazi, uadilifu na uwajibikaji katika utoaji wa huduma. 

          Mpango huu sasa unaboreshwa kwa kupokea maoni na ushauri kutoka kwa Wananchi na Wadau mbalimbali. Njia za kukusanya maoni pamoja na Tovuti ya Wananchi (www.wananchi.go.tz), barua kupitia Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Ikulu, S.L.P. 9120, Dar es Salaam, ujumbe bila malipo kupitia simu ya mkononi (SMS) namba 0658-999222, barua pepe:  ogp@ikulu.go.tz.

          Mpango Kazi wa OGP Tanzania unapatikana kwenye Tovuti ya Wananchi – www.wananchi.go.tz . Wananchi na Wadau wengine wanaimizwa  kushiri kikamilifu kutoa maoni yao katika kuboresha Mpango Kazi wa OGP Tanzania. Mwisho wa kupokea maoni/ushauri au mapendekezo ni tarehe 30/03/2012.



IMETOLEWA NA OFISI YA RAIS
IKULU – DAR ES SALAAM

TAREHE:.15 Februari 2012.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)

Post Bottom Ad

Responsive Ads Here

Pages