Picha ni kutoka maktaba yetu. Wanafunzi wa UDSM wakiandamana.
WANAFUNZI
41 wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam jana walirejeshwa rumande baada ya
kushindwa masharti ya dhamana katika kesi inayowakabili ya kufanya
mkusanyiko usio halali na kukaidi amri ya jeshi la Polisi. Awali
wanafunzi 50 wa chuo hicho walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi
Kisutu Dar es Salaam, wakikabiliwa na makosa hayo mbele ya Hakimu
Mkazi, Waliarwande Lema. Washitakiwa
hao walisomewa mashitaka na waendesha mashitaka mawakili wa Serikali,
Ledislaus Komanya na Shadrack Kimaro. Komanya alidai kuwa Novemba 11
mwaka huu, katika eneo la Mlimani, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,
washitakiwa wote kwa pamoja walifanya mkusanyiko usio wa halali na
kusababisha uvunjifu wa amani katika eneo hilo. Kosa la pili wakili
Komanya alidai washitakiwa hao wakiwa kwenye mkusanyiko huo haramu kwa
lengo la kufanya mgomo, askari wa jeshi la Polisi waliwazuia na
kuwaambia watawanyike lakini walikaidi amri hiyo.
Washitakiwa hao walikana
mashtaka hayo na Hakimu Lema alisema ili mshitakiwa apate dhamana, kila
mmoja anapaswa kuwa na mdhamini mmoja wa kuaminika ambaye atasaini
bondi ya Sh milioni moja. Hata hivyo ni washitakiwa tisa tu kati ya 50
ndiyo waliotimiza masharti na kupata dhamana na wengine walipelekwa
gerezani kwa kushindwa kutimiza masharti ya dhamana.
Washitakiwa waliopata dhamana ni
Rehema Mnuo, Glory Masawe, Happy Amulike, Elisia Mpangala, Frida
Timoth, Stela Msofe, Betwel Martin, Mmasi Stephano na Rugemalila
Venance. Baadhi ya waliokosa dhamana ni pamoja na Mwambapa Elias,
Everest Ambrose, Baraka Monas, Helen Moshi, Alphonce Lusako, Matrona
Babu, Rolanda Wilfred, Godfrey Derogations, Moris Denis, Evon Gumbi.
Wengine ni Lugiko Mathias,
Ndimbo Jabir, Evarist Wilson, Cornel Rwaga Mushi, Mlazi Kumbuka, Rehema
Munuo, Glory Masawe, Happy Amulike, Elias Mpangala, Frida Timothy,
Stella Mofe, Betwel Martin, Mmasi Stephen na Lugemalila Venance. Kesi
hiyo iliahirishwa hadi Novemba 28 mwaka huu itakapokuja kwa ajili ya
upande wa mashitaka kusoma maelezo ya awali baada ya jana kudai kuwa
uchunguzi wao umekamilika. Novemba 11 mwaka huu, wanafunzi wa chuo
hicho walianzisha mgomo kwa kile walichodai ni kuishinikiza bodi ya
Mikopo iwapatie mikopo baadhi ya wanafunzi wenzao ambao
walikosa.(Campasvibe)
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)