Na.Mwandishi wetu.
Mbunge
wa jimbo la Singida mjini, Mohammed Dewji amesema ataendelea kuhakisha
anapigania kumaliza tatizo la maji kwenye jimbo hilo ikiwemo kupambana
nalo mpaka ngazi ya juu wakiwemo wanaokwamisha mradi huo.
Dewji
alisema hayo mapema leo wakati alipotembelea mradi wa uboreshaji wa
huduma za Maji Safi na Salama Singida Mjini unaofadhiliwa na Benki
yaMaendeleo ya Kiarabu (BADEA), Serikali na mashirika mengine yakiwemo
Shirika la Mafuta ulimwenguni (OFID) unaogharimu dola za kimarekani
bilioni 17.2(SHILINGI 25,800,000,000,00) mpaka kukamilika kwa mradi huo.
Alisema
kua,mradi huo ambao ulianza kuombwa tokea miaka 10 iliyopita na kuja
kukubaliwa mwaka 2009, umekumbwa na changamoto mbalimbali hali
iliyopelekea kushindwa kukamilika kwa wakati hivyo kuahidi kuonana na
viongozi wa juu akiwemo Waziri mwenye dhamana na Rais ilikuondoa tatizo
lililokuwepo.
“Nimepokea
taarifa kutoka kwa Mamlaka ya Maji Singida (SUWASA) na kudai kuwa
miongoni mwa changamoto hizo kwa mradi huo ni kupita kwenye sehemu za
hifadhi ya barabara na katika makazi ya watu, suala hili
nitalishughulikia kuona tunafika wapi ikiwemo kuonana na waziri mwenye
dhamana” alisema Dewji.
Kwa
upande wake Injiania Isaack Nyakonji wa SUWASA alisema mbali
na
matatizo ya mradi huo kupita kwenye hifadhi ya barabara na makazi ya
watu, pia hali ya ukame na tatizo la umeme limechangia kusuaua kwa mradi
huo.
“Singida
ndani ya miaka miwili tulikuwa na ukame sambamba na ukatikaji wa umeme
hali hiyo ilipelekea mradi huu kusimama. Pia mabadiliko ya gharama ya
mradi huu yameongezeka kutokana na mazingira kuwa magumu” alisema
Eng.Nyakonji.
Katika
ziara hiyo, Dewji alitembelea sehemu mbalimbali ya mradi huo maarufu
kama BADEA na kujionea utendaji wa kazi ikiwemo eneo la visima Mwankoko
na sehemu ya tanki kubwa na la kisasa ambalo likikamilika litasaidia
kupunguza shida ya maji Singida Mjini.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)