Mke wa
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Asha Bilal,
akimpongeza kwa kumpa taji la maua mtoto wa dada yake, Musiba Mshimba,
aliyehitimu katika Chuo cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki baada
ya kutunukiwa cheti cha kuhitimu mafunzo ya Doctor Of Medicine wakati
wa mahafali ya 9 ya chuo hicho yaliyofanyika Ukumbi wa karimjee jijini
Dar es Salaam leo mchana.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Kumbukumbu ya Hubert Kairuki,
Dkt. Salim Ahmed Salim, akimtunuku, Musiba Mshimba, aliyehitimu katika
chuo hicho wakati wa maafali ya 9 ya chuo hicho yaliyofanyika katika
Ukumbi wa Karimjee jijini Dar es Salaam leo.
Mama Asha Bilal, Ndugu Jamaa na Marafiki
wakiendelea kumpongeza Musiba Mshimba.
Mama Asha Bilal, akipiga picha ya kumbukumbu na
Musiba pamoja na baadhi ya wanandugu.
Baadhi ya wahitimu wakila kiapo wakati
wa mahafali hayo walipokuwa wakitunukiwa vyeti.
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)