Waziri wa Elimu na Mafunzo ya
Ufundi Stadi Dk Shukuru Kawambwa
.................................
WAHITIMU WA MAFUNZO YA UALIMU 2011
Mhe.
Waziri wa Elimu na Mafunzo Ufundi, Shukuru Kawambwa, Tunaomba kwanza
kukupa pole kwa majukumu mazito uliyonayo katika ujenzi wa taifa letu.
Pia tunakupongeza kwa uimara na ushupavu wako katika kusimamia masuala
mbalimbali ya Elimu nchini.
Mhe. Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi lengo kuu la waraka huu kwako ni kukufikishia lalamiko letu moja kwa moja.
Sisi
ni wahitimu wa mafunzo ya ualimu tangu mwezi wa tano, mwaka huu mpaka
hivi leo ni miezi zaidi ya mitano inaelekea sita bado hatujui mstakabali
wetu kuhusu kupatiwa ajira . Katika shule nyingi za serikali, mambo si
shwari hata kidogo. Kuna upungufu mkubwa wa walimu
wenye
ujuzi wa kufundisha. Ni jambo la kusikitisha kuwa walimu wenye vyeti,
stashahada na shahada wametoka vyuoni hawajaweza kuajiriwa. Baadhi yetu
tunabangaiza ilimradi mkono uingie kinywani.
Zimetoka
habari mbalimbali katika vyombo vya habari zinazoleta mkanganyiko na
sisi kushindwa kuelewa mstakabali wa ajira zetu utakuwa vipi. Kwa mujibu
wa Gazeti la Mwananchi la tarehe 06 November. Naibu katibu mkuu
anayeshughulikia Elimu katika Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa (JUMANNE SAGINI) alisema, "ajira tayari zimekamilika
na tumepokea majina ya waalimu 23,027 na kwamba ifikapo November 15
mwaka huu ajira za waalimu zitakuwa zimetangazwa" Lakini tarehe hii
imepita hakuna kilichotangazwa..sasa tunashindwa kuelewa..Je huyu
kiongozi alidanganya umma?
Wakati
hilo likiendelea Gazeti la HabariLeo la tarehe 13 November likaandika.
"NAIBU Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, (PHILIPO MULUGO) amesema
serikali itaajiri walimu wapya 23,000 katika kipindi cha mwaka wa fedha
ujao" Sasa hapa ndio tunachanganykiwa zaidi mwaka
wa
fedha ujao unaanza Julai 2012. Sasa hatuelewi lipi ni lipi kwa sababu
kila kiongozi ameongea la kwake. Tunaomba Mh Waziri utoe tamko rasmi
kuhusu swala hili.
Mh.
Waziri wa Elimu tunatumaini kuwa lalamiko, kilio na ombi letu
utalipokea na kulifanyia kazi. Tunakutakia afya tele na mafanikio katika
shughuli mbalimbali za ujenzi wa taifa letu na kuinua kiwango cha elimu
nchini.
Ahsante sana
No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)