Mahojiano Maalum kati ya Mh Waziri Mkuu na Urban Pulse kurushwa na STAR TV - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Mahojiano Maalum kati ya Mh Waziri Mkuu na Urban Pulse kurushwa na STAR TV

Mh Waziri MKuu Akifanya mahojiano na Baraka Baraka

Urban Pulse Creative wakishirikiana na Star tv wanakuletea Mahojiano Maalum na Mh. Waziri Mkuu Mizengo Pinda alipofanya ziara nchini Uingereza hivi karibuni. Mahojiano haya yalikuwa yamelenga zaidi kupata ufahamu na uchambuzi wa namna serikali yetu ya Tanzania inavyofanya kazi pamoja na changamoto zake.
 
Mbali na hapo tulijadiliana kuhusu Majukumu ya Waziri mkuu, Chakula, Nishati, Jumuiya ya Afrika Mashariki na mchakato wa katiba Mpya kuelekea kuazimisha miaka 50 ya uhuru.
 
Mahojiano haya yalifanywa na Baraka Baraka  Kutoka Urban Pulse na yatarushwa Hewani kupitia  kituo cha Star TV Jumapili ijayo Tarehe 30 octoba 2011 kuanzia saa 10.30 katika kipindi cha Medani za siasa.
 
Tafadhali usikose kuangalia kipindi hiki ili upate kujifunza mambo mbalimbali kuhusu Tanzania na Serikali yetu.
 
Asanteni,
 
Urban Pulse Creative

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages