SHULE YAKOSA CHOO MAGONJWA YA MLIPUKO YATISHIA, NA WATOTO WAKETI SAKAFUNI WAKIHITAJI ELIMU BORA. - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

SHULE YAKOSA CHOO MAGONJWA YA MLIPUKO YATISHIA, NA WATOTO WAKETI SAKAFUNI WAKIHITAJI ELIMU BORA.

Hiki ndicho choo wanachotumia wanafunzi wa shule ya msingi Mpakani iliyopo mjini Tunduma majaaliwa yao yakoje? wanasoma wakiwa wameketi sakafuni, Tunduma ni moja ya miji maarufu nchini kwa biashara kati ya Tanzania na nchi zilizopo kusini mwa Afrika, ni mji wenye msongamano mkubwa wa biashara.
Jamani haiwezekani kwa hili pia magonjwa ya Mlipuko kutishia eneo hili, Wizara husika tazameni kwa macho ya huruma na kutekeleza pia ahadi Mashuleni.
Huenda watoto hawa ni wa wafanyabiashara wanasoma kwa kuketi chini,wanaweza kuwa wazazi wao ndio wamiliki wa maduka yanayozunguka katika mji maarufu wa Tunduma, wametelekezwa?serikali iko wapi mbona imewatelekeza watoto hawa?
Serikali angalieni hili ili kutimiza Azima kuimalisha Sekta ya Elimu kwa lengo la kufuta Ujinga kwani watoto wanahitaji kupata Elimu bora sawa na wengine na hakuna lisilowezekana, kwani sehemu nyingine mmeweza kutekeleza uboreshaji wa Miundombinu. Haki sawa daima ili watoto wapate kusoma na kuandika kwa ufasaha.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages