Makamu Wa Pili Wa Rais Balozi Seif Idd Apokea Ubani Kutoka PPF ili Kufariji Watu Waliopatwa na Maafa ya Kuzama na Meli ya M.V Spice Islanders. - LUKAZA BLOG

All You Want is Here | Chochote Unachohitaji Utakipata Hapa

Habari Mpya

Makamu Wa Pili Wa Rais Balozi Seif Idd Apokea Ubani Kutoka PPF ili Kufariji Watu Waliopatwa na Maafa ya Kuzama na Meli ya M.V Spice Islanders.


Mkurugenzi Mkuu wa mfuko wa Pencheni ya mashirika na taasisi za umma Bw, William Erio akimkabidhi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi hundi ya Sh, Milioni kumi kusaidia mfuko wa maafa wa Zanzibar kufuatia ajari ya meli ya Mv. Spice Islanders iliotokea hivi karibuni
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi akifafanua jambo mara baada ya kupokea hundi ya sh, milioni kumi kutoka kwa uongozi wa mfuko wa pencheni ya mashirika na taasisi za umma PPF kusaidia mfuko wa maafa wa Zanzibar kufuatia ajali ya mv spice. Pichani kushoto ni Mkurugenzi Mkuu wa PPF Bw William Erio akiwa na ofisa uhusiano wake Bibi Lulu Mengele
----
Na Othman Khamis Ame Ofisi ya Mkamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar
 
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi amepokea ubani kutoka kwa Uongozi wa Mfuko wa Pencheni ya Mashirika na Taasisi za Umma Tanzania {PPF } ili kufariji watu waliopatwa na maafa ya kuzama na Meli ya M.V Spice Islanders.
 
Mkurugenzi Mkuu wa PPF Bwana William Erio alimkabidhi Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi Hundi ya Jumla ya shilingi milioni kumi Kusaidia mfuko wa Maafa Zanzibar unaoratibu shughuli zote za Maafa Zanzibar. 


Bwana William amesema Maafa yaliyowapata wananchi hao yamegusa Taasisi yao na Jamii yote ya Watanzania. Amewataka waliokumbwa na Mtihani huo kuwa na subira katika kipindi hichi kigumu cha Janga hilo. Akipokea msaada huo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar ambae pia ni Mwenyekiti wa Kamati ya Taifa ya Maafa Balozi Seif Ali Iddi amezipongeza Taasisi na Jumuiya zote ndani na nje ya Nchi zinazoendelea kutoa misaada yao. Balozi Seif amesema misaada inayoendelea kutolewa inaashiria mshikamano uliopo kati ya Serikali, Taasisi tofauti pamoja na Wananchi.

No comments:

Post a Comment

Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)


Pages