Mheshimiwa kawambwa aliyasema hayo katika mahafali ya kidato cha nne ya shule ya sekondari Jitegemee ya jijini Dar es Salaam, shule ambayo inamilikiwa na jeshi la kujenga taifa (JKT).
Kawambwa pia aliwataka wanafunzi kuepuka udanganyifu wa aina yoyote katika mitihani ijayo huku akisifu juhudi za serikali katika kuongeza ufaulu na wengi kujiunga na kidato cha tano.
"Nawaomba wazazi kuacha tabia ya kuwatafutia wanafunzi mitihani ya wizi kwani kufanya hivyo ni kuwadumaza watoto akili zao ambazo walimu wamezitayarisha kwa miaka minne na hivyo kuwa chanzo cha wanafunzi hao kufeli na hivyo kuwavurugia maisha yao kutokana na mipango ya kuhakikisha mtihani hauvuji." alisema Dr Kawambwa.
Picha na matukio na Vicent Manyanyika





No comments:
Post a Comment
Tafadhari Maoni Yenye Matusi Hayatakuwa Publish Tutoe Maoni Bila Kuumiza Wala Kujeruhi Hisia Za Mtu.....@(Sponsored By Lukaza Blog)